< Waamuzi 6 >

1 Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
Or les enfants d'Israël firent ce qui déplaît à l'Eternel; et l'Eternel les livra entre les mains de Madian pendant sept ans.
2 Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
Et la main de Madian se renforça contre Israël, [et] à cause des Madianites les enfants d'Israël se firent des creux qui sont dans les montagnes, et des cavernes, et des forts.
3 Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
Car il arrivait que quand Israël avait semé, Madian montait avec Hamalec et les Orientaux, et ils montaient contre lui.
4 Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
Et faisant un camp contr'eux ils ravageaient les fruits du pays jusqu'à Gaza, et ne laissaient rien de reste en Israël, ni vivres, ni menu bétail, ni bœufs, ni ânes.
5 Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
Car eux et leurs troupeaux montaient, et ils venaient avec leurs tentes en aussi grand nombre que des sauterelles, tellement qu'eux et leurs chameaux étaient sans nombre; et ils venaient au pays pour le ravager.
6 Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
Israël donc fut fort appauvri par Madian, et les enfants d'Israël crièrent à l'Eternel.
7 Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
Et il arriva que quand les enfants d'Israël eurent crié à l'Eternel à l'occasion de Madian,
8 Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
L'Eternel envoya un Prophète vers les enfants d'Israël, qui leur dit: Ainsi a dit l'Eternel le Dieu d'Israël: Je vous ai fait monter hors d'Egypte, et je vous ai retirés de la maison de servitude;
9 Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
Et vous ai délivrés de la main des Egyptiens, et de la main de tous ceux qui vous opprimaient, et les ai chassés de devant vous, et vous ai donné leur pays.
10 Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
Je vous ai dit aussi: Je suis l'Eternel votre Dieu, vous ne craindrez point les dieux des Amorrhéens, au pays desquels vous habitez; mais vous n'avez point obéi à ma voix.
11 Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
Puis l'Ange de l'Eternel vint, et s'assit sous un chêne qui était à Hophra, appartenant à Joas Abihézérite. Et Gédeon son fils battait le froment dans le pressoir, pour le sauver de devant Madian.
12 Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
Alors l'Ange de l'Eternel lui apparut, et lui dit: Très-fort et vaillant homme, l'Eternel est avec toi.
13 Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
Et Gédeon lui répondit: Hélas mon Seigneur! [est-il possible] que l'Eternel soit avec nous? et pourquoi donc toutes ces choses nous sont-elles arrivées? Et où sont toutes ces merveilles que nos pères nous ont récitées, en disant: L'Eternel ne nous a-t-il pas fait monter hors d'Egypte? car maintenant l'Eternel nous a abandonnés, et nous a livrés entre les mains des Madianites.
14 Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
Et l'Eternel le regardant lui dit: Va avec cette force que tu as, et tu délivreras Israël de la main des Madianites; ne t'ai-je pas envoyé?
15 Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
Et il lui répondit: Hélas, mon Seigneur! par quel moyen délivrerai-je Israël? Voici, mon millier est le plus pauvre qui soit en Manassé, et je suis le plus petit de la maison de mon père.
16 Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
Et l'Eternel lui dit: Parce que je serai avec toi, tu frapperas les Madianites comme s'ils n'étaient qu'un seul homme.
17 Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
Et il lui répondit: Je te prie, si j'ai trouvé grâce devant toi, de me donner un signe [pour montrer] que c'est toi qui parles avec moi.
18 Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
Je te prie, ne t'en va point d'ici jusqu'à ce que je revienne à toi, et que j'apporte mon présent, et que je le mette devant toi. Et il dit: J'y demeurerai jusqu'à ce que tu reviennes.
19 Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
Alors Gédeon rentra, et apprêta un chevreau de lait, et des gâteaux sans levain d'un Epha de farine; mit la chair dans un panier, le bouillon dans un pot, et il les lui apporta sous le chêne, et les lui présenta.
20 Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
Et l'Ange de Dieu lui dit: Prends cette chair et ces gâteaux sans levain, et mets-les sur ce rocher, et répands le bouillon; et il le fit ainsi.
21 Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
Alors l'Ange de l'Eternel ayant étendu le bâton qu'il avait en sa main, toucha la chair et les gâteaux sans levain, et le feu monta du rocher, et consuma la chair et les gâteaux sans levain; puis l'Ange de l'Eternel s'en alla de devant lui.
22 Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
Et Gédeon vit que c'était l'Ange de l'Eternel, et il dit: ha, Seigneur Eternel; est-ce pour cela que j'ai vu l'Ange de l'Eternel face à face?
23 Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
Et l'Eternel lui dit: Il va bien pour toi; ne crains point, tu ne mourras point.
24 Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
Et Gédeon bâtit là un autel à l'Eternel, et l'appela L'ETERNEL DE PAIX. Et cet autel est demeuré jusqu'à aujourd'hui à Hophra des Abihézérites.
25 Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
Or il arriva en cette nuit-là que l'Eternel lui dit: Prends un taureau d'entre les bœufs qui sont à ton père, savoir le deuxième taureau, de sept ans; et démolis l'autel de Bahal qui est à ton père, et coupe le bocage qui est auprès;
26 Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
Et bâtis un autel à l'Eternel ton Dieu sur le haut de ce fort, en un lieu convenable. Tu prendras ce deuxième taureau, et tu l'offriras en holocauste avec les arbres du bocage que tu couperas.
27 Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
Gédeon donc ayant pris dix hommes d'entre ses serviteurs, fit comme l'Eternel lui avait dit; et parce qu'il craignait la maison de son père et les gens de la ville, s'il l'eût fait de jour, il le fit de nuit.
28 Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
Et les gens de la ville se levèrent de bon matin, et voici, l'autel de Bahal avait été démoli, et le bocage qui était auprès, était coupé, et le deuxième taureau était offert en holocauste sur l'autel qu'on avait bâti.
29 Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
Et ils se disaient les uns aux autres: Qui a fait ceci? Et s'en étant informés, et ayant cherché, ils dirent: Gédeon le fils de Joas a fait ceci.
30 Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
Puis les gens de la ville dirent à Joas: Fais sortir ton fils, et qu'il meure; car il a démoli l'autel de Bahal, et a coupé le bocage qui était auprès.
31 Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
Et Joas répondit à tous ceux qui s'adressèrent à lui: Est-ce vous qui prendrez la cause de Bahal? Est-ce vous qui le sauverez? Quiconque aura pris sa cause, sera mis à mort d'ici au matin. S'il est Dieu, qu'il défende sa cause, de ce qu'on a démoli son autel.
32 Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
Et en ce jour-là il appela Gédeon Jérubbahal, et dit: Que Bahal défende sa cause de ce que [Gédeon] a démoli son autel.
33 Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
Or tous les Madianites, les Hamalécites, et les Orientaux s'assemblèrent tous, et ayant passé le Jourdain ils se campèrent en la vallée de Jizréhel.
34 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
Et l'Esprit de l'Eternel revêtit Gédeon; lequel sonna de la trompette, et les Abihézérites s'assemblèrent auprès de lui.
35 Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
Il envoya aussi des messagers par toute [la Tribu de] Manassé, qui s'assembla aussi auprès de lui; puis il envoya des messagers en Aser, en Zabulon, et en Nephthali, lesquels montèrent pour aller au-devant d'eux.
36 Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
Et Gédeon dit à Dieu: Si tu dois délivrer Israël par mon moyen, comme tu l'as dit,
37 tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
Voici, je m'en vais mettre une toison dans l'aire; si la rosée est sur la toison seule, et que le sec soit dans toute la place, je connaîtrai que tu délivreras Israël par mon moyen, selon que tu m'en as parlé.
38 Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
Et la chose arriva ainsi, car s'étant levé de bon matin le lendemain, et ayant pressé cette toison, il en fit sortir pleine une tasse d'eau de rosée.
39 Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
Gédeon dit encore à Dieu: Que ta colère ne s'enflamme point contre moi, et je parlerai seulement cette fois; je te prie, que je fasse un essai en la toison encore cette fois seulement; je te prie qu'il n'y ait rien de sec que la toison, et fais que la rosée soit sur toute la place [de l'aire].
40 Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.
Et Dieu fit ainsi cette nuit-là; car il n'y eut rien de sec que la toison, et la rosée fut sur toute la place de l'aire.

< Waamuzi 6 >