< Waamuzi 6 >

1 Waisraeli wakafanya tena yaliyo maovu mbele za Bwana, naye kwa miaka saba Bwana akawatia mikononi mwa Wamidiani.
Les enfants d’Israël firent ce qui est mal aux yeux de Yahweh, et Yahweh les livra entre les mains de Madian, pendant sept ans.
2 Mkono wa Midiani ukawa na nguvu dhidi ya Israeli na kwa ajili ya Wamidiani, Waisraeli wakajitengenezea mahali pa kujificha milimani, kwenye mapango na ngome.
La main de Madian fut puissante contre Israël. À cause de Madian, les enfants d’Israël se firent les antres qui sont dans les montagnes, les cavernes et les hauteurs fortifiées.
3 Kila wakati Waisraeli walipopanda mazao mashambani, Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki walivamia nchi yao.
Quand Israël avait semé, Madian montait avec Amalec et les fils de l’Orient, et ils marchaient contre lui.
4 Wakapiga kambi katika mashamba yao na kuharibu mazao ya nchi yote hadi kufikia Gaza, wala hawakuacha kiumbe chochote kilicho hai kwa Waisraeli, iwe kondoo au ngʼombe au punda.
Campés en face d’ Israël, ils dévastaient les productions de le terre jusque près de Gaza, et ne laissaient aucune subsistance en Israël, ni brebis, ni bœufs, ni ânes.
5 Walipanda na mifugo yao na mahema yao, mfano wa makundi ya nzige. Ilikuwa haiwezekani kuwahesabu watu na ngamia zao; wakavamia nchi ili kuiharibu.
Car ils montaient avec leurs troupeaux et leurs tentes, et venaient nombreux comme des nuées de sauterelles; eux et leurs chameaux étaient innombrables, et ils venaient dans le pays pour le dévaster.
6 Waisraeli wakafanywa kuwa maskini sana na Wamidiani, hata Israeli wakamlilia Bwana kuomba msaada.
Israël fut très affaibli à cause de Madian, et les enfants d’Israël crièrent vers Yahweh.
7 Waisraeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Wamidiani,
Lorsque les enfants d’Israël eurent crié vers Yahweh au sujet de Madian,
8 Bwana akawapelekea nabii, ambaye aliwaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: Niliwapandisha mtoke Misri, toka nchi ya utumwa.
Yahweh envoya un prophète aux enfants d’Israël. Il leur dit: « Ainsi parle Yahweh le Dieu d’Israël: Je vous ai fait monter de l’Égypte, et je vous ai fait sortir de la maison de servitude.
9 Nikawanyakua kutoka mikononi mwa Wamisri na kutoka mikononi mwa watesi wenu wote. Nikawafukuza watoke mbele yenu nami nikawapa ninyi nchi yao.
Je vous ai délivrés de la main des Égyptiens et de la main de tous vos oppresseurs; je les ai chassés devant vous, et je vous ai donné leur pays.
10 Nikawaambia, ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; msiiabudu miungu ya Waamori, ambayo mnakaa katika nchi yao!’ Lakini ninyi hamkuitii sauti yangu.”
Je vous ai dit: je suis Yahweh, votre Dieu; vous ne craindrez point les dieux des Amorrhéens dans le pays desquels vous habitez. Mais vous n’avez pas écouté ma voix. »
11 Malaika wa Bwana akaja akaketi chini ya mti wa mwaloni huko Ofra, ambao ulikuwa mali ya Yoashi, Mwabiezeri, ambako Gideoni mwanawe alikuwa akipepeta ngano penye shinikizo la kukamulia zabibu, ili kuificha Wamidiani wasiione.
Et l’Ange de Yahweh vint, et il s’assit sous le térébinthe d’Ephra, qui apporterait à Joas, de la famille d’Abiéser. Gédéon, son fils, battait le froment dans le pressoir, pour le mettre à l’abri de Madian.
12 Malaika wa Bwana alipomtokea Gideoni, akamwambia, “Bwana yu pamoja nawe, Ewe shujaa mwenye nguvu.”
L’Ange de Yahweh lui apparut et lui dit: « Yahweh est avec toi, vaillant héros. »
13 Gideoni akajibu, “Ee Bwana wangu, kama Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametutokea? Yako wapi basi yale matendo yake makuu baba zetu waliyotusimulia juu yake waliposema, ‘Je, Bwana hakutupandisha kutoka Misri?’ Lakini sasa Bwana ametuacha na kututia katika mkono wa Midiani.”
Gédéon lui dit: « Ah! mon seigneur, si Yahweh est avec nous, pourquoi toutes ces choses nous sont-elles arrivées? Et où sont tous ses prodiges que nos pères nous ont racontés, en disant: Yahweh ne nous a-t-il pas fait monter de l’Égypte? Et maintenant Yahweh nous abandonne et nous livre entre les mains de Madian. »
14 Bwana akamgeukia na kusema “Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli kutoka mikononi mwa Wamidiani. Je, si mimi ninayekutuma wewe?”
Yahweh se tourna vers lui et dit: « Va avec cette force que tu as, et délivre Israël de la main de Madian; ne t’ai-je pas envoyé? »
15 Gideoni akauliza, “Ee Bwana wangu, nitawezaje kuwaokoa Israeli? Ukoo wangu ndio dhaifu kuliko zote katika Manase, nami ndiye mdogo wa wote katika jamaa yangu.”
Gédéon lui dit: « Ah! Seigneur, avec quoi délivrerai-je Israël? Voici, ma famille est la plus pauvre en Manassé, et je suis le plus petit dans la maison de mon père. »
16 Bwana akamjibu, “Nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kana kwamba walikuwa ni mtu mmoja.”
Yahweh lui dit: « Je serai avec toi, et tu battras Madian comme un seul homme. »
17 Gideoni akajibu, “Kama basi nimepata kibali machoni pako, nipe ishara kuonyesha kweli kwamba ni wewe unayesema nami.
Gédéon lui dit: « Si j’ai trouvé grâce à vos yeux, donnez-moi un signe que c’est vous qui me parlez.
18 Tafadhali ninakuomba usiondoke hapa mpaka nitakaporudi na kukuletea sadaka yangu na kuiweka mbele yako.” Naye Bwana akamwambia, “Nitangoja mpaka utakaporudi.”
Ne vous éloignez point d’ici jusqu’à ce que je revienne auprès de vous, que j’apporte mon offrande et que je la dépose devant vous. » Et Yahweh dit: « Je resterai jusqu’à ce que tu reviennes. »
19 Gideoni akaingia ndani ya nyumba yake na kuandaa mwana-mbuzi pamoja na kuoka mikate isiyotiwa chachu kutokana na efa moja ya unga. Akaweka nyama kwenye kikapu na mchuzi kwenye chungu, akamletea huyo malaika hapo nje chini ya mti wa mwaloni na kumpa.
Gédéon, étant entré, apprêta un chevreau et, avec un épha de farine, il fit des pains sans levain; puis, ayant mis la chair dans une corbeille et le jus dans un vase, il les lui apporta sous le térébinthe et les lui offrit.
20 Malaika wa Mungu akamwambia, “Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uviweke juu ya mwamba huu na umimine huo mchuzi juu yake.” Gideoni akafanya hivyo.
L’Ange de Yahweh lui dit: « Prends la chair et les pains sans levain, pose-les sur ce rocher, et verse le jus. » Et il fit ainsi.
21 Malaika wa Bwana akainyoosha fimbo iliyokuwa mkononi mwake, ncha yake ikagusa ile nyama na ile mikate isiyotiwa chachu, nao moto ukatoka kwenye mwamba ukateketeza ile nyama na ile mikate. Malaika wa Bwana akatoweka kutoka machoni pake.
L’Ange de Yahweh étendit l’extrémité du bâton qu’il avait à la main, et toucha la chair et les pains sans levain. Aussitôt le feu s’éleva du rocher, et consuma la chair et les pains sans levain, et l’Ange de Yahweh disparut à ses yeux.
22 Gideoni alipotambua kuwa ni malaika wa Bwana, akapiga kelele kwa mshangao, akasema, “Ole wangu, Bwana Mwenyezi! Kwa kuwa nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso!”
Gédéon vit que c’était l’Ange de Yahweh et Gédéon dit: « Malheur à moi, Seigneur Yahweh, car j’ai vu l’Ange de Yahweh face à face. »
23 Lakini Bwana akamwambia, “Amani iwe kwako! Usiogope. Hutakufa.”
Yahweh lui dit: « Sois en paix, ne crains point, tu ne mourras pas. »
24 Hivyo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu mahali pale na kupaita, Yehova-Shalom. Mpaka leo ingalipo imesimama huko Ofra ya Waabiezeri.
Gédéon bâtit là un autel à Yahweh et l’appela: « Yahweh-Schalôm; » cet autel existe encore aujourd’hui à Ephra d’Abiéser.
25 Usiku ule ule Bwana akamwambia, “Mchukue ngʼombe dume wa baba yako, yaani, yule wa pili mwenye miaka saba, na ubomoe madhabahu ya Baali aliyo nayo baba yako, na ukaikate Ashera iliyo karibu nayo.
Cette nuit-là, Yahweh dit à Gédéon: « Prends le jeune taureau de ton père, et le second taureau de sept ans. Renverse l’autel de Baal qui est à ton père, et coupe l’aschéra qui est auprès.
26 Kisha mjengee Bwana Mungu wako, madhabahu halisi, kwa taratibu zake, juu ya huu mwamba. Kwa kutumia kuni za hiyo nguzo ya Ashera uliyoikatakata, mtoe sadaka huyo dume wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
Tu bâtiras ensuite, au sommet de ce lieu fort, un autel à Yahweh, ton Dieu, et tu le disposeras; tu prendras le second taureau et tu offriras un holocauste avec le bois de l’aschéra que tu auras coupée. »
27 Basi Gideoni akawachukua watumishi wake kumi na kufanya kama Bwana alivyomwambia. Lakini kwa kuwa aliwaogopa jamaa yake na watu wa mji, akafanya haya usiku badala ya mchana.
Gédéon prit dix hommes parmi ses serviteurs, et exécuta ce que Yahweh lui avait dit: mais, comme il n’osait le faire de jour par crainte de la maison de son père et des gens de la ville, il le fit de nuit.
28 Watu wa mji walipoamka asubuhi, tazama madhabahu ya Baali imebomolewa na nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwakatwa na yule ngʼombe wa pili ametolewa sadaka juu ya madhabahu yaliyojengwa upya!
Lorsque les gens de la ville se levèrent le lendemain matin, voici que l’autel de Baal était renversé, que l’aschéra qui était auprès était coupée, et que le second taureau était offert en holocauste sur l’autel récemment bâti.
29 Wakaulizana, “Ni nani aliyetenda mambo haya?” Walipochunguza kwa makini, wakaambiwa, “Ni Gideoni mwana wa Yoashi, ndiye alitenda hivi.”
Ils se dirent l’un à l’autre: « Qui a fait cela? » et ils s’informèrent et firent des recherches. On leur dit: « C’est Gédéon, fils de Joas, qui a fait cela. »
30 Watu wa mji wakamwambia Yoashi, “Mlete mwanao hapa. Ni lazima afe, kwa sababu amebomoa madhabahu ya Baali na kukatakata nguzo ya Ashera iliyokuwa karibu nayo.”
Alors les gens de la ville dirent à Joas: « Fais sortir ton fils et qu’il meure, car il a renversé l’autel de Baal et coupé l’aschéra qui était auprès. »
31 Lakini Yoashi akauambia ule umati uliokuwa umezunguka ukiwa kinyume naye, “Je, ninyi mtamtetea Baali? Mnajaribu kumwokoa? Yeyote mwenye kumpigania atauawa kufikia kesho asubuhi! Kama Baali ni mungu kweli, anaweza kujitetea mwenyewe wakati mtu anapobomoa madhabahu yake.”
Joas dit à tous ceux qui se tenaient là contre lui: « Est-ce à vous de prendre parti pour Baal? Ou bien est-ce à vous de le secourir? Quiconque prendra parti pour Baal sera mis à mort avant demain matin. Si Baal est Dieu, que lui-même prenne en main sa cause, puisqu’on a renversé son autel! »
32 Basi siku ile wakamwita Gideoni “Yerub-Baali,” yaani, “Baali na ashindane naye,” kwa sababu alibomoa madhabahu yake.
En ce jour, un donna à Gédéon le nom de Jérobaal, en disant: « Que Baal se défende contre lui, puisqu’il a renversé son autel! »
33 Basi Wamidiani wote, Waamaleki na mataifa mengine ya mashariki wakaunganisha majeshi yao, wakavuka ngʼambo ya Yordani na kupiga kambi katika Bonde la Yezreeli.
Tout Madian, Amalec et les fils de l’Orient se rassemblèrent et, ayant passé le Jourdain, ils campèrent dans la plaine de Jezraël.
34 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Gideoni, akapiga tarumbeta, akiwaita Waabiezeri ili wamfuate.
L’Esprit de Yahweh revêtit Gédéon; il sonna de la trompette, et les Abiésérites s’assemblèrent pour marcher à sa suite.
35 Akatuma wajumbe waende katika Manase yote, akiwataka wachukue silaha na pia katika Asheri, Zabuloni na Naftali, nao wakakwea ili kukutana nao.
Il envoya des messagers dans tout Manassé, qui s’assembla aussi pour le suivre. Il envoya des messagers dans Aser, dans Zabulon et dans Nephtali, et ils montèrent à leur rencontre.
36 Gideoni akamwambia Mungu, “Kama utawaokoa Waisraeli kwa mkono wangu, kama ulivyoahidi:
Gédéon dit à Dieu: « Si vous voulez sauver Israël par ma main, comme vous l’avez dit,
37 tazama, nitaweka ngozi ya kondoo kwenye kiwanja cha kupuria nafaka, na kama utakuwepo umande juu ya ngozi tu, nayo ardhi yote ikiwa kavu, ndipo nitakapojua kuwa utaokoa Israeli kwa mkono wangu, kama ulivyosema.”
voici, je mettrai une toison de laine sur l’aire: si la toison seule se couvre de rosée, et que tout le sol alentour reste sec, je connaîtrai que vous délivrerez Israël par ma main, comme vous l’avez dit. »
38 Hivyo ndivyo ilivyotokea. Gideoni akaamka asubuhi na mapema kesho yake, akaikamua ile ngozi, umande ukatoka, maji ya kujaa bakuli.
Et il arriva ainsi. Le jour suivant, s’étant levé de bon matin, il pressa la toison, et en fit sortir la rosée, plein une coupe d’eau.
39 Kisha Gideoni akamwambia Bwana, “Usinikasirikie. Ninaomba nifanye ombi moja lingine. Niruhusu nifanye jaribio jingine moja kwa ngozi hii. Wakati huu uifanye ngozi hii kavu na ardhi yote ifunikwe na umande.”
Gédéon dit à Dieu: « Que votre colère ne s’enflamme pas contre moi; que je puisse encore parler une fois: je voudrais une fois encore seulement faire une épreuve avec la toison: que la toison seule reste sèche, et que la rosée tombe sur tout le sol alentour. »
40 Usiku ule Mungu akafanya hivyo. Ngozi ile ilikuwa kavu, nayo ardhi yote ikafunikwa na umande.
Et Dieu fit ainsi cette nuit-là: la toison seule resta sèche, et tout le sol se couvrit de rosée.

< Waamuzi 6 >