< Waamuzi 5 >

1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
Et Debora chanta, en ce jour-là, avec Barak, fils d’Abinoam, en disant:
2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
Parce que des chefs se sont mis en avant en Israël, parce que le peuple a été porté de bonne volonté, bénissez l’Éternel!
3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
Rois, écoutez! princes, prêtez l’oreille! Moi, moi, je chanterai à l’Éternel; je chanterai un hymne à l’Éternel, le Dieu d’Israël.
4 “Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
Éternel! quand tu sortis de Séhir, quand tu t’avanças des champs d’Édom, la terre trembla, et les cieux distillèrent, et les nuées distillèrent des eaux.
5 Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
Les montagnes se fondirent devant l’Éternel, ce Sinaï, devant l’Éternel, le Dieu d’Israël.
6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
Aux jours de Shamgar, fils d’Anath, aux jours de Jaël, les chemins étaient délaissés, et ceux qui allaient par les grands chemins allaient par des sentiers détournés;
7 Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
Les villes ouvertes étaient délaissées en Israël, elles étaient délaissées, – jusqu’à ce que je me suis levée, moi Debora, jusqu’à ce que je me suis levée, une mère en Israël.
8 Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
On choisissait de nouveaux dieux, alors la guerre était aux portes! On ne voyait ni bouclier ni pique chez quarante milliers en Israël.
9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
Mon cœur est aux gouverneurs d’Israël qui ont été portés de bonne volonté parmi le peuple. Bénissez l’Éternel!
10 “Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
Vous qui montez sur des ânesses blanches, vous qui êtes assis sur des tapis, et vous qui allez par les chemins, méditez!
11 juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
À cause de la voix de ceux qui partagent [le butin], au milieu des lieux où l’on puise l’eau: là, ils racontent les justes actes de l’Éternel, ses justes actes envers ses villes ouvertes en Israël. Alors le peuple de l’Éternel est descendu aux portes.
12 ‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
Réveille-toi, réveille-toi, Debora! Réveille-toi, réveille-toi, dis un cantique! Lève-toi, Barak, et emmène captifs tes captifs, fils d’Abinoam!
13 “Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
Alors descends, toi, le résidu des nobles, [comme son] peuple; Éternel! descends avec moi au milieu des hommes forts.
14 Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
D’Éphraïm [sont venus] ceux dont la racine est en Amalek; derrière toi [vient] Benjamin, au milieu de tes peuples. De Makir sont descendus les gouverneurs, et de Zabulon sont venus ceux qui tiennent le bâton du commandant.
15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
Et les princes d’Issacar ont été avec Debora, et Issacar, comme Barak; [il a été] envoyé sur ses pas dans la vallée. Aux divisions de Ruben, grandes considérations de cœur!
16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
Pourquoi es-tu resté entre les barres des étables, à écouter le bêlement des troupeaux? Aux divisions de Ruben, grandes délibérations de cœur!
17 Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
Galaad est demeuré au-delà du Jourdain; et Dan, pourquoi a-t-il séjourné sur les navires? Aser est resté au bord de la mer, et il est demeuré dans ses ports.
18 Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
Zabulon est un peuple qui a exposé son âme à la mort, Nephthali aussi, sur les hauteurs des champs.
19 “Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
Les rois sont venus, ils ont combattu; alors les rois de Canaan ont combattu à Thaanac, près des eaux de Meguiddo; [mais], de butin d’argent, ils n’en ont pas emporté.
20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
On a combattu des cieux; du chemin qu’elles parcourent, les étoiles ont combattu contre Sisera.
21 Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
Le torrent de Kison les a emportés, le torrent des anciens temps, le torrent de Kison. Mon âme, tu as foulé aux pieds la force!
22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
Alors les talons des chevaux battirent [le sol] à cause de la course rapide, de la course rapide de leurs [hommes] vaillants.
23 Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
Maudissez Méroz, dit l’Ange de l’Éternel; maudissez, maudissez ses habitants! car ils ne sont pas venus au secours de l’Éternel, au secours de l’Éternel, avec les hommes forts.
24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
Bénie soit, au-dessus des femmes, Jaël, femme de Héber, le Kénien! Qu’elle soit bénie au-dessus des femmes qui se tiennent dans les tentes!
25 Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
Il a demandé de l’eau, elle lui a donné du lait; dans la coupe des nobles elle lui a présenté du caillé.
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
Elle a étendu sa main vers le pieu, et sa droite vers le marteau des ouvriers; elle a frappé Sisera, elle lui a brisé la tête, elle lui a fracassé et transpercé la tempe.
27 Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
Entre ses pieds il s’est courbé, il est tombé, il s’est étendu [par terre]; entre ses pieds il s’est courbé, il est tombé; là où il s’est courbé, là il est tombé anéanti.
28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
La mère de Sisera regarde par la fenêtre, et s’écrie à travers le treillis: Pourquoi son char tarde-t-il à venir? Pourquoi la marche de ses chars est-elle si lente?
29 Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
Les sages d’entre ses princesses lui répondent; elle s’est donné la réponse à elle-même.
30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
N’ont-ils pas trouvé, n’ont-ils pas divisé le butin? Une jeune fille, deux jeunes filles par tête d’homme; du butin de vêtements de couleur pour Sisera, du butin de vêtements de couleur brodés, deux vêtements de couleur brodés, pour le cou des captives!
31 “Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
Qu’ainsi périssent tous tes ennemis, ô Éternel! mais que ceux qui t’aiment soient comme le soleil quand il sort dans sa force! Et le pays fut en repos 40 ans.

< Waamuzi 5 >