< Waamuzi 5 >

1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
And Delbora and Barach, sone of Abynoen, sungen in that dai, and seiden,
2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
Ye men of Israel, that `offriden wilfuli youre lyues to perel, blesse the Lord.
3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
Ye kingis, here, ye princes, perceyueth with eeris; Y am, Y am the womman, that schal synge to the Lord; Y schal synge to the Lord God of Israel.
4 “Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
Lord, whanne thou yedist out fro Seir, and passidist bi the cuntrees of Edom, the erthe was moued, and heuenes and cloudis droppiden with watris; hillis flowiden fro the `face of the Lord,
5 Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
and Synai fro the face of the Lord God of Israel.
6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
In the daies of Sangar, sone of Anach, in the daies of Jahel, paththis restiden, and thei that entriden bi tho yeden bi paththis out of the weie.
7 Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
Stronge men in Israel cessiden, and restiden, til Delbora roos, a modir in Israel.
8 Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
The Lord chees newe batels, and he destriede the yatis of enemyes; scheeld and spere apperiden not in fourti thousynde of Israel.
9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
Myn herte loueth the princes of Israel; ye that offriden you to perel bi youre owyn wille,
10 “Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
blesse ye the Lord; speke ye, that stien on schynynge assis, and sitten aboue in doom, and goen in the wey.
11 juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
Where the charis weren hurtlid doun to gidere, and the oost of enemyes was straunglid, there the `riytfulnessis of the Lord be teld, and mercy among the stronge of Israel; thanne the `puple of the Lord cam doun to the yatis, and gat prinsehod.
12 ‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
Rise, rise thou, Delbora, rise thou, and speke a song; rise thou, Barach, and thou, sone of Abynoen, take thi prisoneris.
13 “Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
The relikis of the puple ben sauyd; the Lord fauyt ayens stronge men of Effraym.
14 Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
He dide awei hem in Amalech, and aftir hym of Beniamyn in to thi puplis, thou Amalech. Princes of Machir and of Zabulon yeden doun, that ledden oost to fiyte.
15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
The duykis of Isachar weren with Delbora, and sueden the steppis of Barach, which yaf hym silf to perel, as in to a dich, and in to helle. While Ruben was departid ayens hym silf; the strijf of greet hertyd men was foundun.
16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
Whi dwellist thou bitwixe `tweyne endis, that thou here the hissyngis of flockis? While Ruben was departid ayens hym silf, the strijf of greet hertid men was foundun.
17 Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
Gad restide biyendis Jordan, and Dan yaf tent to schippis. Aser dwellide in the `brenke of the see, and dwellide in hauenes.
18 Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
Forsothe Zabulon and Neptalym offriden her lyues to deeth, in the cuntre of Morema, `that is interpretid, hiy.
19 “Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
Kyngis camen, and fouyten; kyngis of Canaan fouyten in Thanath, bisidis the watris of Magedon; and netheles thei token no thing bi prey.
20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
Fro heuene `me fauyt ayens hem; sterris dwelliden in her ordre and cours, and fouyten ayens Sisara.
21 Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
The stronde of Cyson drow `the deed bodies of hem, the stronde of Cadymyn, the stronde of Cyson. My soule, to-trede thou stronge men.
22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
The hors howis felden, while the strongeste of enemyes fledden with bire, and felden heedli.
23 Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
Curse ye the lond of Meroth, seide the `aungel of the Lord, curse ye `the dwelleris of hym, for thei camen not to the help of the Lord, `in to the help of the strongeste of hym.
24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
Blessyd among wymmen be Jahel, the wijf of Aber Cyney; blessid be sche in hir tabernacle.
25 Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
To Sisara axynge watir sche yaf mylk, and in a viol of princes sche yaf botere.
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
Sche puttide the left hond to a nail, and the riyt hond to the `hameris of smyythis; and sche smoot Sisara, and souyte in the heed a place of wounde, and perside strongli the temple.
27 Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
He felde bitwixe `the feet of hir, he failide, and diede; he was waltryd bifor hir feet, and he lay with out soule, and wretchidful.
28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
His modir bihelde bi a wyndow, and yellide; and sche spak fro the soler, Whi tarieth his chaar to come ayen? Whi tarieden the feet of his foure horsid cartis?
29 Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
Oon wisere than `othere wyues of hym answeride these wordis to the modir of hir hosebonde,
30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
In hap now he departith spuylis, and the faireste of wymmen is chosun to hym; clothis of dyuerse colouris ben youun to Sisara in to prey, and dyuerse aray of houshold is gaderid to ourne neckis.
31 “Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
Lord, alle thin enemyes perische so; sotheli, thei that louen thee, schyne so, as the sunne schyneth in his risyng. And the lond restide fourti yeer.

< Waamuzi 5 >