< Waamuzi 5 >

1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
and to sing Deborah and Barak son: child Abinoam in/on/with day [the] he/she/it to/for to say
2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
in/on/with to lead leader in/on/with Israel in/on/with be willing people to bless LORD
3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
to hear: hear king to listen to rule I to/for LORD I to sing to sing to/for LORD God Israel
4 “Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
LORD in/on/with to come out: come you from Seir in/on/with to march you from land: country Edom land: country/planet to shake also heaven to drip/prophesy also cloud to drip/prophesy water
5 Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
mountain: mount to flow from face: before LORD this Sinai from face: before LORD God Israel
6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
in/on/with day Shamgar son: child Anath in/on/with day Jael to cease way and to go: walk path to go: walk way crooked
7 Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
to cease villager in/on/with Israel to cease till which/that to arise: rise Deborah which/that to arise: rise mother in/on/with Israel
8 Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
to choose God new then war gate shield if: surely no to see: see and spear in/on/with forty thousand in/on/with Israel
9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
heart my to/for to decree Israel [the] be willing in/on/with people to bless LORD
10 “Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
to ride she-ass tawny to dwell upon garment and to go: walk upon way: road to muse
11 juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
from voice: sound to shoot between well there to recount righteousness LORD righteousness villager his in/on/with Israel then to go down to/for gate people LORD
12 ‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
to rouse to rouse Deborah to rouse to rouse to speak: promise song to arise: rise Barak and to take captive captive your son: child Abinoam
13 “Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
then to go down survivor to/for great people LORD to go down to/for me in/on/with mighty man
14 Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
from Ephraim root their in/on/with Amalek after you Benjamin in/on/with kinsman your from Machir to go down to decree and from Zebulun to draw in/on/with tribe: staff secretary
15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
and ruler my in/on/with Issachar with Deborah and Issachar so Barak in/on/with valley to send: depart in/on/with foot his in/on/with division Reuben great: large decree heart
16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
to/for what? to dwell between: among [the] sheepfold to/for to hear: hear piping flock to/for division Reuben great: large search heart
17 Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
Gilead in/on/with side: beyond [the] Jordan to dwell and Dan to/for what? to sojourn fleet Asher to dwell to/for coast sea and upon landing his to dwell
18 Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
Zebulun people to taunt soul: life his to/for to die and Naphtali upon height land: country
19 “Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
to come (in): come king to fight then to fight king Canaan in/on/with Taanach upon water Megiddo unjust-gain silver: money not to take: recieve
20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
from heaven to fight [the] star from highway their to fight with Sisera
21 Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
torrent: river Kishon to sweep away them torrent: river ancient torrent: river Kishon to tread soul my strength
22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
then to smite heel horse from rushing rushing mighty: stallion his
23 Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
to curse Meroz to say messenger: angel LORD to curse to curse to dwell her for not to come (in): come to/for help LORD to/for help LORD in/on/with mighty man
24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
to bless from woman Jael woman: wife Heber [the] Kenite from woman in/on/with tent to bless
25 Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
water to ask milk to give: give in/on/with bowl great to present: bring curd
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
hand her to/for peg to send: reach and right her to/for hammer labour(er) and to smite Sisera to destroy head his and to wound and to pass temple his
27 Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
between foot her to bow to fall: kill to lie down: lay down between foot her to bow to fall: kill in/on/with in which to bow there to fall: kill to ruin
28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
about/through/for [the] window to look and to cry mother Sisera about/through/for [the] lattice why? be ashamed chariot his to/for to come (in): come why? to delay beat chariot his
29 Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
wise princess her to answer also he/she/it to return: reply word her to/for her
30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
not to find to divide spoil womb womb to/for head great man spoil dye to/for Sisera spoil dye embroidery dye embroidery to/for neck spoil
31 “Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
so to perish all enemy your LORD and to love: friend him like/as to come out: (sun)rise [the] sun in/on/with might his and to quiet [the] land: country/planet forty year

< Waamuzi 5 >