< Waamuzi 5 >

1 Ndipo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
Then Deborah and Barak the son of Abinoam sang on that day, saying,
2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Bwana!
That the leaders took the lead in Israel, that the people offered themselves willingly, bless ye Jehovah.
3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Bwana, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli.
Hear, O ye kings. Give ear, O ye rulers. I, even I, will sing to Jehovah. I will sing praise to Jehovah, the God of Israel.
4 “Ee Bwana, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
Jehovah, when thou went forth out of Seir, when thou marched out of the field of Edom, the earth trembled, the heavens also dropped, yea, the clouds dropped water.
5 Milima ilitetemeka mbele za Bwana, hata ule wa Sinai, mbele za Bwana, Mungu wa Israeli.
The mountains quaked at the presence of Jehovah, even yon Sinai at the presence of Jehovah, the God of Israel.
6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
In the days of Shamgar the son of Anath, in the days of Jael, the highways were unoccupied, and the travelers walked through byways.
7 Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma mpaka mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
The rulers ceased in Israel, they ceased, until that I, Deborah, arose, that I arose a mother in Israel.
8 Walipochagua miungu migeni, vita vilikuja katika malango ya mji, hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa mashujaa 40,000 katika Israeli.
They chose new gods, then war was in the gates. Was there a shield or spear seen among forty thousand in Israel?
9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, pamoja na wale wanaojitoa wenyewe kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Bwana!
My heart is toward the governors of Israel, who offered themselves willingly among the people. Bless ye Jehovah.
10 “Nanyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mtembeao barabarani, fikirini
Tell, ye who ride on white donkeys, ye who sit on rich carpets, and ye who walk by the way.
11 juu ya sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Bwana, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Bwana walipoteremka malangoni pa mji.
Far from the noise of archers, in the places of drawing water, there they shall rehearse the righteous acts of Jehovah, the righteous acts of his rule in Israel. Then the people of Jehovah went down to the gates.
12 ‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
Awake, awake, Deborah, awake, awake, utter a song. Arise, Barak, and lead away thy captives, thou son of Abinoam.
13 “Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wenye nguvu, watu wa Bwana, wakashuka dhidi ya mashujaa wenye nguvu.
Then a remnant of the nobles and the people came down. Jehovah came down for me against the mighty.
14 Kutoka Efraimu wakaja watu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini akiwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
Out of Ephraim, those whose root is in Amalek, after thee, Benjamin, among thy peoples, out of Machir, came down governors, and out of Zebulun those who handle the marshal's staff.
15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
And the princes of Issachar were with Deborah, as was Issachar, so was Barak, into the valley they rushed forth at his feet. By the watercourses of Reuben there were great resolves of heart.
16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
Why did thou sit among the sheepfolds, to hear the pipings for the flocks? At the watercourses of Reuben there were great searchings of heart.
17 Gileadi alikaa ngʼambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
Gilead abode beyond the Jordan. And Dan, why did he remain in ships? Asher sat still at the haven of the sea, and abode by his creeks.
18 Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
Zebulun was a people who jeopardized their lives to the death, and Naphtali, upon the high places of the field.
19 “Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua fedha wala nyara.
The kings came and fought. Then the kings of Canaan fought in Taanach by the waters of Megiddo. They took no gain of money.
20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
From heaven the stars fought; from their courses they fought against Sisera.
21 Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
The river Kishon swept them away, that ancient river, the river Kishon. O my soul, march on with strength.
22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
Then the horse hoofs stamped by reason of the prancings, the prancings of their strong ones.
23 Malaika wa Bwana akasema, ‘Merozi alaaniwe. Walaaniwe watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Bwana, kumsaidia Bwana dhidi ya hao wenye nguvu.’
Curse ye Meroz, said the agent of Jehovah. Curse ye bitterly the inhabitants of it, because they did not come to the help of Jehovah, to the help of Jehovah against the mighty.
24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote waishio kwenye mahema.
Blessed above women shall Jael be, the wife of Heber the Kenite. Blessed shall she be above women in the tent.
25 Aliomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
He asked water. She gave him milk. She brought him butter in a lordly dish.
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
She put her hand to the tent-pin, and her right hand to the workmen's hammer. And with the hammer she smote Sisera; she struck through his head. Yea, she pierced and struck through his temples.
27 Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Pale alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
At her feet he bowed, he fell, he lay. At her feet he bowed, he fell. Where he bowed, there he fell down dead.
28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa?’
Through the window she looked forth, and cried-the mother of Sisera through the lattice-Why is his chariot so long in coming? Why do the wheels of his chariots delay?
29 Wanawake wenye busara kuliko wengine wote wakamjibu; naam, husema moyoni mwake,
Her wise ladies answered her, yea, she returned answer to herself,
30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: yote haya yakiwa nyara?’
Have they not found, have they not divided the spoil? A damsel, two damsels to every man, to Sisera a spoil of dyed garments, a spoil of dyed garments embroidered, of dyed garments embroidered on both sides, on the necks of the spoil?
31 “Adui zako wote na waangamie, Ee Bwana! Bali wote wakupendao na wawe kama jua lichomozavyo kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
So let all thine enemies perish, O Jehovah, but let those who love him be as the sun when he goes forth in his might. And the land had rest forty years.

< Waamuzi 5 >