< Waamuzi 4 >

1 Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni pa Bwana.
Les enfants d'Israël firent encore ce qui est mal aux yeux de Yahweh, après la mort d'Aod.
2 Hivyo Bwana akawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu
Et Yahweh les vendit entre les mains de Jabin, roi de Chanaan, qui régnait à Asor; le chef de son armée était Sisara, et il habitait à Haroseth-Goïm.
3 Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli wakamlilia Bwana wakaomba msaada.
Les enfants d'Israël crièrent vers Yahweh, car Jabin avait neuf cents chars de fer et, depuis vingt ans, il opprimait durement les enfants d'Israël.
4 Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye alikuwa anaamua Israeli wakati ule.
En ce temps-là, Débora, prophétesse, femme de Lapidoth, rendait la justice en Israël.
5 Debora alikuwa akiketi chini ya Mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama na Betheli katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakaja kwake ili awaamue.
Elle siégeait sous le palmier de Débora, entre Rama et Béthel, dans la montagne d'Ephraïm; et les enfants d'Israël montaient vers elle pour être jugés.
6 Akatuma wamwite Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali na kumwambia, “Bwana, Mungu wa Israeli, anakuagiza: ‘Nenda, chukua wanaume 10,000 toka Naftali na Zabuloni, mwende Mlima Tabori.
Elle envoya appeler Barac, fils d'Abinoëm, de Cédés en Nephthali, et elle lui dit: " N'est-ce pas l'ordre qu'a donné Yahweh, le Dieu d'Israël? Va, rends-toi sur le mont Thabor, et prends avec toi dix mille hommes des fils de Nephthali et des fils de Zabulon.
7 Nitamshawishi Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake na jeshi lake, hadi Mto Kishoni na kumtia mikononi mwako.’”
Je t'amènerai, au torrent de Cison, Sisara, le chef de l'armée de Jabin, avec ses chars et ses troupes, et je le livrerai entre tes mains. "
8 Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami nitakwenda, lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”
Barac lui dit: " Si tu viens avec moi, j'irai; mais si tu ne viens pas avec moi, je n'irai pas. "
9 Debora akamwambia, “Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini njia unayoiendea haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.” Hivyo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi,
Elle répondit: " Oui, j'irai avec toi, mais, dans l'expédition que tu vas faire, la gloire ne sera pas pour toi; car Yahweh livrera Sisara entre les mains d'une femme. " Et Débora se leva et elle se rendit avec Barac à Cédès.
10 mahali ambapo Baraka aliwaita Zabuloni na Naftali. Watu 10,000 wakamfuata Baraka, na Debora pia akaenda pamoja naye.
Barac convoqua Zabulon et Nephthali à Cédès; et dix mille hommes partirent à sa suite, et Débora partit avec lui.
11 Basi Heberi, Mkeni, alikuwa amejitenga na Wakeni wengine, yaani, wazao wa Hobabu, mkwewe Mose, naye akapiga hema lake karibu na ule mti mkubwa wa mwaloni ulioko Saananimu, karibu na Kedeshi.
Héber, le Cinéen, s'était emparé des Cinéens, des fils de Hobab, beau-frère de Moïse, et il avait dressé sa tente jusqu'au chêne de Sennim, prés de Cédès.
12 Sisera alipoambiwa kuwa Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa amepanda Mlima Tabori,
On informa Sisara que Barac, fils d'Abinoëm, était parti vers le mont Thabor;
13 Sisera akakusanya pamoja magari yake yote 600 ya chuma na watu wote waliokuwa pamoja naye, kuanzia Haroshethi-Hagoyimu mpaka Mto wa Kishoni.
et Sisara, fit venir d'Haroseth-Goïm, vers le torrent de Cison, tous ses chars, neuf cents chars de fer, et tout le peuple qui était avec lui.
14 Ndipo Debora akamwambia Baraka, “Nenda! Hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera mikononi mwako. Je, Bwana hakukutangulia mbele yako?” Hivyo Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori, akifuatwa na watu 10,000.
Alors Débora dit à Barac: " Lève-toi, car voici le jour où Yahweh a livré Sisara entre tes mains. Est-ce que Yahweh n'est pas sorti devant toi? " Et Barac descendit du mont Thabor, ayant dix mille hommes à sa suite.
15 Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, pamoja na jeshi lake lote kwa upanga mbele ya Baraka, naye Sisera akaliacha gari lake na kukimbia kwa miguu.
Yahweh mit en déroute Sisara, tous ses chars et toute son armée, par le tranchant de l'épée, devant Barac; et Sisara descendit de son char et s'enfuit à pied.
16 Lakini Baraka akafuata magari pamoja na jeshi mpaka Haroshethi-Hagoyimu. Jeshi lote la Sisera likaanguka kwa upanga, wala hakuna hata mtu mmoja aliyesalia.
Barac poursuivit les chars et l'armée jusqu'à Haroseth-Goïm, et toute l'armée de Sisara tomba sous le tranchant de l'épée; pas un homme n'échappa.
17 Sisera, hata hivyo, akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli, mkewe Heberi, Mkeni, kwa sababu palikuwa na uhusiano wa kirafiki kati ya Yabini mfalme wa Hazori na ukoo wa Heberi, Mkeni.
Sisara se réfugia à pied dans la tente de Jahel, femme de Héber, le Cinéen; car il y avait paix entre Jabin, roi d'Asor, et la maison de Héber, le Cinéen.
18 Yaeli akaenda kumlaki Sisera na kumwambia, “Karibu, bwana wangu, karibu ingia ndani kabisa. Usiogope.” Basi Sisera akaingia ndani ya hema ya Yaeli, naye akamfunika kwa blanketi nene.
Jahel sortit au-devant de Sisara et lui dit: " Entre, mon seigneur, entre chez moi, ne crains point. " Il entra chez elle dans la tente, et elle le cacha sous une couverture.
19 Akamwambia, “Nina kiu, tafadhali nipe maji ya kunywa.” Ndipo akafungua kiriba cha maziwa na kumpa akanywa, kisha akamfunika.
Il lui dit: " Donne-moi, je te prie, un peu d'eau à boire, car j'ai soif. " Elle ouvrit l'outre du lait, lui donna à boire et le couvrit.
20 Naye Sisera akamwambia, “Simama mlangoni pa hema na mtu yeyote akija na kukuuliza, ‘Je, kuna mtu yeyote hapa?’ sema, ‘Hapana.’”
Il lui dit: " Tiens-toi à l'entrée de la tente et, si l'on vient l'interroger, en disant: Y a-t-il un homme ici? tu répondras: Non. "
21 Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akachukua nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akiwa amelala usingizi, akiwa amechoka. Akakigongomea kile kigingi kwenye paji la uso wake, kikapenya hata kuingia ardhini, naye akafa.
Jahel, femme de Héber, saisit un pieu de la tente et, ayant pris en main le marteau, elle s'approcha de lui doucement et lui enfonça dans la tempe le pieu, qui pénétra dans le sol, car il dormait profondément, étant accablé de fatigue; et il mourut.
22 Baraka akakaribia akimfuatia Sisera, Yaeli akatoka kumlaki. Akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Hivyo wakaingia ndani ya hema wakiwa wamefuatana na tazama Sisera alikuwa amelala humo, akiwa amekufa, na hicho kigingi cha hema kikiwa kimegongomewa kupitia paji la uso wake.
Et voici, comme Barac poursuivait Sisara, Jahel sortit à sa rencontre et lui dit: " Viens, et je te montrerai l'homme que tu cherches. " Il entra chez elle et vit Sisara étendu mort, le pieu dans la tempe.
23 Basi siku ile Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani, mbele ya Israeli.
En ce jour, Dieu humilia Jabin, roi de Chanaan, devant les enfants d'Israël.
24 Nao mkono wa Waisraeli ukaendelea kuwa na nguvu zaidi na zaidi dhidi ya Yabini, mfalme wa Kanaani, mpaka wakamwangamiza.
Et la main des enfants d'Israël s'appesantit de plus en plus sur Jabin, roi de Chanaan, jusqu'à ce qu'ils eussent détruit Jabin, roi de Chanaan.

< Waamuzi 4 >