< Waamuzi 4 >

1 Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni pa Bwana.
Men da Ehud var død, blev Israeliterne ved at gøre, hvad der var ondt i HERRENS Øjne.
2 Hivyo Bwana akawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu
Derfor gav han dem til Pris, for Kana'anæerkongen Jabin, som herskede i Hazor; hans Hærfører var Sisera, som boede i Harosjet-Haggojim.
3 Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli wakamlilia Bwana wakaomba msaada.
Da raabte Israeliterne til HERREN. Thi Jabin havde 900 Jernvogne, og han trængte Israeliterne haardt i tyve Aar.
4 Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye alikuwa anaamua Israeli wakati ule.
Profetinden Debora, Lappidots Hustru, var paa den Tid Dommer i Israel;
5 Debora alikuwa akiketi chini ya Mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama na Betheli katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakaja kwake ili awaamue.
hun sad under Deborapalmen imellem Rama og Betel i Efraims Bjerge, og Israeliterne drog op til hende med deres Retstrætter.
6 Akatuma wamwite Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali na kumwambia, “Bwana, Mungu wa Israeli, anakuagiza: ‘Nenda, chukua wanaume 10,000 toka Naftali na Zabuloni, mwende Mlima Tabori.
Hun sendte nu Bud efter Barak, Abinoams Søn fra Kedesj i Naftali, og sagde til ham: »Har ikke HERREN, Israels Gud, budt: Bryd op, drag hen paa Tabors Bjerg og tag 10 000 Mand af Naftali og Zebulon med dig;
7 Nitamshawishi Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake na jeshi lake, hadi Mto Kishoni na kumtia mikononi mwako.’”
saa skal jeg drage Jabins Hærfører Sisera med hans Vogne og Hærstyrke hen til dig ved Kisjonbækken og give ham i din Haand!«
8 Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami nitakwenda, lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”
Barak svarede hende: »Hvis du vil gaa med, vil jeg gaa; men hvis du ikke gaar med, gaar jeg ikke!«
9 Debora akamwambia, “Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini njia unayoiendea haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.” Hivyo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi,
Da sagde hun: »Vel, jeg gaar med, men saa faar du ikke Æren af den Færd, du begiver dig ud paa, thi HERREN vil overgive Sisera i en Kvindes Haand!« Saa brød Debora op og drog af Sted til Kedesj med Barak.
10 mahali ambapo Baraka aliwaita Zabuloni na Naftali. Watu 10,000 wakamfuata Baraka, na Debora pia akaenda pamoja naye.
Barak stævnede nu Zebulon og Naftali sammen i Kedesj, og 10 000 Mand fulgte med ham derop; ogsaa Debora gik med. —
11 Basi Heberi, Mkeni, alikuwa amejitenga na Wakeni wengine, yaani, wazao wa Hobabu, mkwewe Mose, naye akapiga hema lake karibu na ule mti mkubwa wa mwaloni ulioko Saananimu, karibu na Kedeshi.
Men Keniten Heber havde skilt sig fra Keniterne, Moses's Svigerfader Hobabs Sønner, og slaaet Telt i Egnen hen imod Elon-Beza'anannim ved Kedesj.
12 Sisera alipoambiwa kuwa Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa amepanda Mlima Tabori,
Da Sisera fik Melding om, at Barak, Abinoams Søn, var draget op paa Tabors Bjerg,
13 Sisera akakusanya pamoja magari yake yote 600 ya chuma na watu wote waliokuwa pamoja naye, kuanzia Haroshethi-Hagoyimu mpaka Mto wa Kishoni.
stævnede han alle sine Stridsvogne, 900 jernbeslagne Vogne, og hele sin Krigsstyrke fra Harosjet Haggojim til Kisjonbækken.
14 Ndipo Debora akamwambia Baraka, “Nenda! Hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera mikononi mwako. Je, Bwana hakukutangulia mbele yako?” Hivyo Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori, akifuatwa na watu 10,000.
Da sagde Debora til Barak: »Bryd nu op! Thi det er i Dag. HERREN vil give Sisera i din Haand. Er HERREN ikke draget foran dig?« Barak steg da ned fra Tabors Bjerg, fulgt af de 10 000 Mand.
15 Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, pamoja na jeshi lake lote kwa upanga mbele ya Baraka, naye Sisera akaliacha gari lake na kukimbia kwa miguu.
Og foran Barak bragte HERREN Uorden iblandt alle Siseras Stridsvogne og i hele hans Hær. Sisera sprang af sin Vogn og flygtede til Fods;
16 Lakini Baraka akafuata magari pamoja na jeshi mpaka Haroshethi-Hagoyimu. Jeshi lote la Sisera likaanguka kwa upanga, wala hakuna hata mtu mmoja aliyesalia.
men Barak satte efter Vognene og Hæren lige til Harosjet Haggojim, og hele Siseras Hær faldt for Sværdet, ikke een blev tilbage.
17 Sisera, hata hivyo, akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli, mkewe Heberi, Mkeni, kwa sababu palikuwa na uhusiano wa kirafiki kati ya Yabini mfalme wa Hazori na ukoo wa Heberi, Mkeni.
Sisera var imidlertid flygtet til Fods til Keniten Hebers Hustru Jaels Telt, thi der var Fred imellem Kong Jabin af Hazor og Keniten Hebers Slægt.
18 Yaeli akaenda kumlaki Sisera na kumwambia, “Karibu, bwana wangu, karibu ingia ndani kabisa. Usiogope.” Basi Sisera akaingia ndani ya hema ya Yaeli, naye akamfunika kwa blanketi nene.
Da gik Jael Sisera i Møde og sagde til ham: »Tag dog ind hos mig, Herre, du har intet at frygte!« Han tog da ind i Teltet hos hende, og hun dækkede ham til med et Tæppe.
19 Akamwambia, “Nina kiu, tafadhali nipe maji ya kunywa.” Ndipo akafungua kiriba cha maziwa na kumpa akanywa, kisha akamfunika.
Og han sagde til hende: »Giv mig lidt Vand at drikke, thi jeg er tørstig!« Da aabnede hun Mælkesækken og gav ham at drikke og dækkede ham atter til.
20 Naye Sisera akamwambia, “Simama mlangoni pa hema na mtu yeyote akija na kukuuliza, ‘Je, kuna mtu yeyote hapa?’ sema, ‘Hapana.’”
Saa sagde han til hende: »Stil dig hen i Teltdøren, og hvis der kommer en og spørger, om der er nogen herinde, saa sig nej!«
21 Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akachukua nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akiwa amelala usingizi, akiwa amechoka. Akakigongomea kile kigingi kwenye paji la uso wake, kikapenya hata kuingia ardhini, naye akafa.
Men Jael, Hebers Hustru, greb en Teltpæl og tog en Hammer i Haanden, listede sig ind til ham og slog Pælen igennem hans Tinding, saa den trængte ned i Jorden; thi han var faldet i dyb Søvn, træt som han var; saaledes døde han.
22 Baraka akakaribia akimfuatia Sisera, Yaeli akatoka kumlaki. Akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Hivyo wakaingia ndani ya hema wakiwa wamefuatana na tazama Sisera alikuwa amelala humo, akiwa amekufa, na hicho kigingi cha hema kikiwa kimegongomewa kupitia paji la uso wake.
Og se, Barak, søm forfulgte Sisera, kom forbi. Da gik Jael ham i Møde og sagde til ham: »Kom, jeg skal vise dig den Mand, du søger efter!« Saa kom han ind til hende. Og se, der laa Sisera død med Teltpælen gennem Tindingen.
23 Basi siku ile Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani, mbele ya Israeli.
Saaledes lod Gud paa den Dag Kana'anæerkongen Jabin bukke under for Israeliterne;
24 Nao mkono wa Waisraeli ukaendelea kuwa na nguvu zaidi na zaidi dhidi ya Yabini, mfalme wa Kanaani, mpaka wakamwangamiza.
og Israeliternes Haand faldt haardere og haardere paa Kana'anæerkongen Jabin, til de fik ham tilintetgjort.

< Waamuzi 4 >