< Waamuzi 3 >
1 Haya ndiyo mataifa Bwana aliyoyaacha ili kuwajaribu Waisraeli wote ambao hawakujua vita vyovyote vya Kanaani
上主保留的民族 這是上主為考驗那些不曉得客納罕一切戰事的以色列人,所留下來的民族,
2 (alifanya hivi ili tu kuwafundisha wazao wa Waisraeli ambao hawakuwa wamejua vita hapo awali):
叫以色列子民的後代,至少那些以前不曉得這些戰事的人,知道和學習作戰。
3 wafalme watano wa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, Wahivi waishio katika milima ya Lebanoni kuanzia Mlima wa Baal-Hermoni hadi Lebo-Hamathi.
這些民族就是培勒舍特人的五個酋長,一切客納罕人、漆冬人和住在黎巴嫩山上,即從巴耳赫爾孟山直到哈瑪特關口的希威人。
4 Waliachwa ili kuwajaribu Waisraeli kuona kama wangetii amri za Bwana, alizokuwa amewapa baba zao kwa mkono wa Mose.
他們留在那裏是為考驗以色列人,看他們是否聽從上主藉梅瑟吩咐他們祖先的那些誡命。
5 Waisraeli wakaishi miongoni mwa Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
以色列子民就住在客納罕人、赫特人、阿摩黎人、培黎齊人、希威人和耶步斯人中間,
6 Wakawaoa binti zao, nao wakawatoa binti zao waolewe na wana wa hayo mataifa, na kuitumikia miungu yao.
竟然娶了他們的女子為妻,也把自己的女兒嫁給他們的兒子,事奉了他們的神。敖特尼耳民長
7 Waisraeli wakafanya maovu machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana Mungu wao na kutumikia Mabaali na Maashera.
以色列子民行了上主視為惡的事,忘卻了上主他們的天主,而事奉了巴耳諸神和阿舍辣諸女神;
8 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli, hivyo akawauza na kuwatia mikononi mwa Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu-Naharaimu ambaye Israeli walikuwa chini yake wakimtumikia kwa muda wa miaka minane.
因此上主對以色列大發忿怒,將他們交在厄東王雇商黎沙塔殷手中,以色列子民遂服事了雇商黎沙塔殷八年。
9 Waisraeli walipomlilia Bwana, yeye akawainulia mwokozi, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu, ambaye aliwaokoa.
當以色列子民向上主呼籲時,上主給以色列子民興起了一個拯救他們的救星,即加肋布的弟弟刻納次的兒子敖特尼耳。
10 Roho wa Bwana akaja juu yake, hivyo akawa mwamuzi wa Israeli, akaenda vitani. Bwana akamtia Kushan-Rishathaimu mfalme wa Aramu mikononi mwa Othnieli, naye akamshinda.
上主的神降在他身上,他作了以色列的民長,出去作戰;上主把厄東王雇商黎沙塔殷交在他手中,他的`能力勝過了雇商黎沙塔殷。
11 Hivyo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arobaini, mpaka Othnieli mwana wa Kenazi alipofariki.
於是四境平安了四十年。厄胡得民長刻納次的兒子敖特尼耳去世後,
12 Waisraeli wakafanya maovu mbele za Bwana tena, kwa kuwa walifanya maovu hayo Bwana akamtia nguvu Egloni mfalme wa Moabu dhidi ya Israeli.
以色列子民又行了上主視為惡的事,上主就強化摩阿布王厄革隆去打以色列,因為他們行了上主視為惡的事。
13 Egloni akawataka Waamoni na Waamaleki waungane naye, akaja kuishambulia Israeli, nao wakatwaa Mji wa Mitende
他聯合了阿孟子民和阿瑪肋克人,前來擊敗以色列,佔據了棕樹城;
14 Waisraeli wakawa chini ya Egloni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka kumi na minane.
以色列遂服事了摩阿布王厄革隆十八年。
15 Waisraeli wakamlilia tena Bwana, naye akawapa mwokozi: Ehudi, mtu wa shoto, mwana wa Gera, Mbenyamini. Waisraeli wakatuma kwa Egloni mfalme wa Moabu ushuru kwa mkono wa Ehudi.
當以色列子民向上主呼籲時,上主給他們興起了一位拯救者,就是本雅明人革辣的兒子厄胡得,他是左右手能兼用的人;以色列子民便派他給摩阿布王厄革隆獻貢物。
16 Basi Ehudi alikuwa ametengeneza upanga wenye ukatao kuwili, urefu wake ni kama dhiraa moja, akaufunga upanga huo ndani ya nguo yake kwenye paja lake la mkono wa kuume.
厄胡得預備了一把一肘長的雙刃刀,插在右腿衣服底下,
17 Akamkabidhi ushuru Egloni mfalme wa Moabu, ambaye alikuwa mtu mnene sana.
來到摩阿布王厄革隆前獻貢物─厄革隆原是極肥胖的人。
18 Baada ya Ehudi kumkabidhi ule ushuru, wale watu waliokuwa wameubeba huo ushuru aliwaruhusu waende zao.
獻完貢物以後,就把抬貢物的人打發走,
19 Yeye mwenyewe akafuatana nao hadi kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe karibu na Gilgali, ndipo yeye akarudi, akafika kwa Egloni na kusema, “Ee Mfalme, ninao ujumbe wa siri kwa ajili yako.” Mfalme akasema, “Nyamazeni kimya!” Nao wale waliomhudumia wote wakamwacha, wakatoka nje.
自己卻由基耳加耳柱像那裏退回,說:「王呀! 我有機密事要對你說。」王說:「退下! 」於是侍立左右的人都退去。
20 Ndipo Ehudi akamsogelea alipokuwa ameketi peke yake kwenye chumba cha juu cha jumba lake la kifalme la majira ya kiangazi, na kusema, “Ninao ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yako.” Mfalme alipokuwa anainuka kutoka kwenye kiti chake,
厄胡得來到他跟前,他正獨自坐在涼台上的房子裏;厄胡得說:「我有神諭告訴你! 」王就從自己的座位上起立;
21 Ehudi akaunyoosha mkono wake wa kushoto na kuufuta ule upanga aliokuwa ameufunga kwenye paja lake la kulia, akamdunga Mfalme Egloni tumboni mwake.
厄胡得遂伸左手從右腿上拔出刀來,刺入他的腹部,
22 Hata mpini nao ukazama tumboni pamoja na upanga wenyewe, nao upanga ukatokea mgongoni mwake. Ehudi hakuuchomoa huo upanga, nayo mafuta yakashikamana juu ya upanga.
柄和刀都刺了進去,脂肪遂包住了刀子,他沒有從肚子裏把刀抽出來;
23 Ehudi akatoka nje barazani; akamfungia milango ya chumba cha juu na kuifunga kwa funguo.
厄胡得出來到了走廊,把涼台上的門關上,上了鎖。
24 Baada ya kuondoka, watumishi wakaja na kukuta milango ya chumba cha juu imefungwa kwa funguo. Wakasema, “Bila shaka amejipumzisha kwenye chumba cha ndani cha nyumba yake ya majira ya kiangazi.”
他出去之後,王臣前來,看見涼台的房門關著,就說:「他一定在涼台上的內室裏便溺。」
25 Wakangoja hata wakawa na fadhaa, basi wakati hakufungua milango ya chumba, wakachukua funguo na kuifungua. Tazama wakaona bwana wao amelala sakafuni, amekufa.
待他們等煩了,看見沒有人來開涼台上的門,他們就拿鑰匙把門開了,見他們的主子躺在地上死了。
26 Walipokuwa wangali wanangoja, Ehudi akatoroka, akapita hapo kwenye sanamu ya kuchora kwenye mawe na kukimbilia Seira.
在他們猶豫的時候,厄胡得已經逃走,繞過柱像,而逃往色依辣。
27 Alipofika huko, akapiga tarumbeta katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakateremka pamoja naye kutoka vilimani, yeye akiwa anawaongoza.
他到了那裏,就在厄弗辣因山地吹號角,以色列子民就同他由山地下來,他在他們前面,
28 Akawaagiza, “Nifuateni, kwa kuwa Bwana amewatia Moabu, adui zenu, mikononi mwenu.” Kwa hiyo wakateremka wakamfuata, wakavishika vivuko vya Yordani kuelekea Moabu, wala hawakuacha mtu yeyote kuvuka.
對他們說:「你們緊跟著我,因為上主把你們的仇敵摩阿布人已交於你們手中! 」他們遂跟他下去,佔據了摩阿布對面的約但河渡口,不許一人渡過。
29 Wakati huo wakawaua Wamoabu watu waume wapatao 10,000 ambao wote walikuwa wenye nguvu na mashujaa; hakuna mtu yeyote aliyetoroka.
就在那個時候,他們擊殺了摩阿布人約有一萬,都是壯丁和兵士,沒有一個人逃脫。
30 Siku ile Moabu wakashindwa na Israeli, nayo nchi ikawa na amani kwa miaka themanini.
從那天起,摩阿布驅服於以色列手下;境內平安了十八年。沙默加爾民長
31 Baada ya Ehudi akaja Shamgari mwana wa Anathi, aliyewapiga Wafilisti 600 kwa fimbo iliyochongoka ya kuongozea ngʼombe. Naye pia akawaokoa Waisraeli.
在他以後,有阿納特的兒子沙默加爾,他意趕牛棒擊殺了六百培肋舍人,拯救了以色列。