< Waamuzi 20 >

1 Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
C’est pourquoi tous les enfants d’Israël sortirent, et s’étant réunis ensemble comme un seul homme, depuis Dan jusqu’à Bersabée, ils se rendirent, ainsi que la terre de Galaad, vers le Seigneur, à Maspha;
2 Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
Tous les chefs du peuple et toutes les tribus d’Israël vinrent ensemble dans l’assemblée du peuple de Dieu, quarante mille combattants à pied.
3 (Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
(Et les enfants de Benjamin n’ignorèrent pas que les enfants d’Israël étaient montés à Maspha.) Et le Lévite, mari de la femme qui avait été tuée, interrogé comment un si grand crime avait été commis,
4 Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
Répondit: Je vins dans la ville de Gabaa de la tribu de Benjamin avec ma femme, et j’y logeai;
5 Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
Et voilà que des hommes de cette ville environnèrent pendant la nuit la maison dans laquelle je demeurais, voulant me tuer, et tourmentant ma femme avec une fureur incroyable inspirée par la passion; enfin elle est morte.
6 Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
L’ayant prise, je la coupai par morceaux, et j’envoyai les parts dans tous les confins de votre possession, parce que jamais une action si horrible et un si grand forfait n’ont été commis dans Israël.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
Vous êtes tous ici présents, enfants d’Israël, décidez ce que vous devez faire.
8 Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
Et tout le peuple qui était là, répondit comme avec la voix d’un seul homme: Nous ne retournerons point dans nos tabernacles, ni personne n’entrera en sa maison;
9 Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
Mais voici ce que nous ferons tous ensemble contre Gabaa:
10 Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
Qu’on choisisse dix hommes sur cent d’entre toutes les tribus d’Israël, cent sur mille, et mille sur dix mille, afin qu’ils portent à l’armée des vivres, et que nous puissions combattre contre Gabaa de Benjamin, et lui rendre selon son crime, ce qu’elle mérite.
11 Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
Ainsi, tout Israël se rendit auprès de la ville, comme un seul homme, dans un même esprit, et une même résolution.
12 Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
Et ils envoyèrent des messagers à toute la tribu de Benjamin, pour dire: Pourquoi une action si horrible s’est-elle trouvée parmi vous?
13 Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
Livrez-nous les hommes de Gabaa qui ont commis cette infamie, afin qu’ils meurent et que le mal soit enlevé d’Israël. Les Benjamites ne voulurent point entendre l’ordre de leurs frères les enfants d’Israël;
14 Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
Mais ils vinrent de toutes les villes qui étaient de leur lot, à Gabaa pour la secourir, et pour combattre contre tout le peuple d’Israël.
15 Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
Et il se trouva vingt-cinq mille Benjamites, tirant le glaive, outre les habitants de Gabaa,
16 Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
Qui étaient sept cents hommes très vaillants, combattant de la main gauche comme de la droite, et jetant les pierres dans les frondes avec tant de sûreté, qu’ils pouvaient frapper même un cheveu, sans que le coup de la pierre portât le moins du monde en un autre endroit.
17 Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
Il se trouva aussi, sans les enfants de Benjamin, quarante mille hommes d’Israël, tirant le glaive et préparés au combat,
18 Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
Et qui, se levant, vinrent à la maison de Dieu, c’est-à-dire à Silo; et ils consultèrent Dieu, et dirent: Qui sera dans notre armée le prince du combat contre les enfants de Benjamin? Le Seigneur leur répondit: Que Juda soit votre chef.
19 Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
Et aussitôt les enfants d’Israël, se levant dès le matin, campèrent près de Gabaa;
20 Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
Et de là s’avançant au combat contre Benjamin, ils commencèrent à assiéger la ville.
21 Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
Mais les enfants de Benjamin étant sortis de Gabaa, tuèrent en ce jour-là vingt-deux mille hommes des enfants d’Israël.
22 Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
Les enfants d’Israël, se confiant en leur force et en leur nombre, se rangèrent de nouveau en bataille, dans le même lieu dans lequel ils avaient combattu auparavant;
23 Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
De manière cependant qu’auparavant ils montèrent et pleurèrent devant le Seigneur jusqu’à la nuit, qu’ils le consultèrent et dirent: Dois-je aller encore en avant pour combattre contre les enfants de Benjamin, mes frères, ou non? le Seigneur leur répondit: Montez à eux, et engagez la bataille.
24 Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
Et lorsque le jour suivant, les enfants d’Israël se furent avancés au combat contre les enfants de Benjamin,
25 Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
Les enfants de Benjamin sortirent avec impétuosité des portes de Gabaa, et les rencontrant, ils en firent un si grand carnage, qu’ils tuèrent dix-huit mille hommes, tirant le glaive.
26 Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
C’est pourquoi tous les enfants d’Israël vinrent à la maison de Dieu, et, assis, ils pleuraient devant le Seigneur. Ils jeûnèrent ce jour-là jusqu’au soir, et ils lui offrirent des holocaustes et des victimes pacifiques;
27 Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
Et ils le consultèrent sur leur situation. En ce temps-là l’arche du Seigneur était en ce lieu,
28 na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
Et Phinéès, fils d’Eléazar, fils d’Aaron était préposé sur la maison de Dieu. Ils consultèrent donc le Seigneur et dirent: Devons-nous sortir encore au combat contre les enfants de Benjamin, nos frères, ou rester en repos? Le Seigneur leur répondit: Montez, car demain je les livrerai en vos mains.
29 Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
Alors les enfants d’Israël placèrent des embuscades autour de la ville de Gabaa.
30 Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
Et pour la troisième fois, comme pour la première et la seconde, ils firent avancer leur armée contre les enfants de Benjamin.
31 Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
Mais les enfants de Benjamin aussi sortirent audacieusement de la ville et poursuivirent très loin leurs ennemis qui fuyaient; en sorte qu’ils en blessèrent, comme au premier et au second jour, qu’ils taillèrent en pièces ceux qui prenaient la fuite par les deux chemins, dont l’un se prolongeait jusqu’à Béthel, et l’autre jusqu’à Gabaa, et qu’ils tuèrent environ trente hommes;
32 Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
Car ils pensaient qu’ils les tailleraient en pièces comme de coutume. Mais les enfants d’Israël, feignant adroitement une fuite, avaient le dessein de les éloigner de la ville, et de les attirer, en paraissant fuir, dans les susdits chemins.
33 Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
C’est pourquoi tous les enfants d’Israël s’étant levés de leurs postes, étendirent leurs lignes dans le lieu qui est appelé Baalthamar. L’embuscade aussi qui était autour de la ville, commença à se montrer peu à peu,
34 Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
Et à s’avancer par la partie occidentale de la ville. Mais de plus, dix autres mille hommes, choisis entre tout Israël, provoquaient les habitants de la ville au combat. Ainsi, la guerre contre les enfants de Benjamin augmenta; et ils ne comprirent point que la mort les pressait de toute part.
35 Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
Le Seigneur donc les frappa en présence des enfants d’Israël, qui tuèrent, en ce jour-là, vingt-cinq mille et cent hommes, tous guerriers, tirant le glaive.
36 Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
Or, les enfants de Benjamin, lorsqu’ils virent qu’ils étaient inférieurs, commencèrent à fuir. Ce qu’apercevant les enfants d’Israël, ils leur firent place pour fuir, afin qu’ils arrivassent à l’embuscade préparée près de la ville.
37 Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
Et ceux qui étaient embusqués, s’étant levés soudainement de leur retraite, et ayant taillé en pièces Benjamin qui fuyait, entrèrent dans la ville et la frappèrent du tranchant du glaive.
38 Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
Or les enfants d’Israël avaient donné pour signal à ceux qu’ils avaient mis en embuscade, qu’après qu’ils auraient pris la ville, ils allumeraient un feu, afin que, la fumée s’élevant en haut, ils montrassent que la ville avait été prise.
39 ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
Lorsque les enfants d’Israël placés au milieu du combat s’en aperçurent (car les enfants de Benjamin pensèrent qu’ils fuyaient, et ils les poursuivaient plus vivement, après avoir taillé en pièces trente hommes de leur armée),
40 Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
Et qu’ils virent comme une colonne de fumée s’élever de la ville, tandis que Benjamin aussi regardant en arrière, s’aperçut que la ville était prise, et que les flammes étaient portées dans les airs,
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
Les Israélites qui auparavant avait feint une fuite, faisant volte-face, résistaient plus fortement. Ce qu’ayant vu, les enfants de Benjamin prirent la fuite,
42 Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
Et commencèrent à aller dans la voie du désert, les ennemis les poursuivant même jusque-là; mais en outre ceux qui avaient incendié la ville, vinrent à leur rencontre.
43 Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
Et ainsi il arriva que de l’un et de l’autre côté, ils étaient taillés en pièces par les ennemis et on ne faisait nullement de quartier aux mourants. Ils tombèrent, et restèrent terrassés, au côté oriental de la ville de Gabaa.
44 Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
Or, il y eut qui furent tués en ce même lieu, dix-huit mille hommes, et tous très forts combattants.
45 Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
Ce qu’ayant vu ceux qui étaient restés de Benjamin, ils s’enfuirent dans le désert, et ils allaient vers le rocher dont le nom est Remmon. Dans cette fuite aussi, comme ils étaient errants çà et là, prenant divers chemins, les enfants d’Israël en tuèrent cinq mille; et comme ils passaient plus loin, ils les poursuivirent, et en tuèrent encore deux autres mille.
46 Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
Et ainsi il arriva que tous ceux de Benjamin qui tombèrent en divers lieux, étaient au nombre de vingt-cinq mille, guerriers très portés à la guerre.
47 Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
C’est pourquoi de toute l’armée de Benjamin, il resta qui purent s’échapper et s’enfuir dans le désert, six cents hommes; et ils demeurèrent au rocher de Remmon pendant quatre mois.
48 Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.
Mais les enfants d’Israël étant revenus, frappèrent du glaive tout ce qui restait dans la ville, depuis les hommes jusqu’aux bêtes; mais toutes les villes et les bourgades, une flamme dévorante les consuma.

< Waamuzi 20 >