< Waamuzi 20 >

1 Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
Et de Dan à Beerséba et au pays de Galaad tous les enfants d'Israël se mirent en mouvement comme un seul homme, et l'Assemblée se réunit devant l'Éternel à Mitspa.
2 Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
Et dans l'Assemblée du peuple de Dieu parurent les chefs de tout le peuple, toutes les Tribus d'Israël, quatre cent mille hommes de pied, tirant l'épée.
3 (Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
Et les enfants de Benjamin apprirent que les enfants d'Israël étaient montés à Mitspa. Et les enfants d'Israël dirent: Exposez la manière en laquelle ce forfait a été commis.
4 Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
Alors le Lévite, mari de la femme qu'on avait tuée, prit la parole et dit: J'entrai à Gibea en Benjamin, moi et ma concubine, pour y passer la nuit.
5 Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
Et les citoyens de Gibea firent une émeute contre moi, et à cause de moi pendant la nuit ils cernèrent la maison. Ils pensaient à me tuer, et ils ont si indignement abusé de ma concubine qu'elle en est morte.
6 Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
Alors j'ai pris ma concubine et je l'ai coupée en pièces dont j'ai fait des envois dans toutes les terres de l'héritage d'Israël, parce qu'on a commis un forfait et une action infâme en Israël.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
Voilà que vous êtes tous ici, enfants d'Israël; ici même délibérez et décidez.
8 Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
Alors tout le peuple se leva comme un seul homme et dit: Tous tant que nous sommes, nous ne voulons ni retourner à nos tentes ni rentrer dans nos maisons.
9 Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
Et maintenant voici comment nous traiterons Gibea: le sort désignera ceux de nous qui marcheront contre elle.
10 Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
Et nous lèverons dix hommes sur cent dans toutes les Tribus d'Israël et cent sur mille et mille sur dix mille, pour procurer des vivres à la troupe afin que s'étant mise en marche, elle traite Gibea de Benjamin en raison exacte de l'action infâme commise en Israël.
11 Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
Tous les hommes d'Israël se rassemblèrent donc près de la ville unis comme un seul homme.
12 Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
Et les Tribus d'Israël députèrent à toutes les familles de Benjamin, pour dire: Qu'est-ce que ce crime qui s'est commis chez vous?
13 Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
Et maintenant livrez-nous les hommes dépravés de Gibea afin que nous les fassions mourir et que nous exterminions le crime du sein d'Israël. Mais les Benjaminites ne voulurent pas écouter la voix de leurs frères, les enfants d'Israël.
14 Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
Et les enfants de Benjamin vinrent de leurs villes se réunir à Gibea pour marcher au combat contre les enfants d'Israël.
15 Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
Et l'on fit ce jour-là passer à la revue vingt-six mille Benjaminites tirant l'épée sortis des villes, non compris les habitants de Gibea qui passèrent à la revue au nombre de sept cents hommes d'élite.
16 Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
Sur toute cette milice il y avait sept cents hommes d'élite inhabiles de la main droite; tous ils lançaient une pierre avec la fronde et ne manquaient pas le but d'un cheveu.
17 Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
Et les Israélites qui passèrent à la revue, étaient, sans Benjamin, quatre cent mille hommes tirant l'épée, tous gens de guerre.
18 Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
Et s'étant mis en marche ils montèrent à Béthel et consultèrent Dieu. Et les enfants d'Israël demandèrent: Lequel de nous marchera le premier au combat contre les enfants de Benjamin? Et l'Éternel dit: Juda marchera le premier.
19 Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
Là-dessus les enfants d'Israël se mirent en campagne le matin, et ils vinrent camper devant Gibea.
20 Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
Et les hommes d'Israël sortirent pour livrer bataille aux Benjaminites, et ils se rangèrent en bataille contre eux devant Gibea.
21 Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
Alors les Benjaminites firent une sortie de Gibea, et en ce jour tuèrent aux Israélites vingt-deux mille hommes qui jonchèrent le sol.
22 Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
Mais l'armée, les hommes d'Israël, prirent courage et reformèrent leur ligne dans le lieu même où le premier jour ils l'avaient formée.
23 Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
Et les enfants d'Israël montèrent [à Béthel] et pleurèrent devant l'Éternel jusqu'au soir, et ils consultèrent l'Éternel en disant: Dois-je engager de nouveau le combat avec les enfants de Benjamin, mon frère? Et l'Éternel dit: Attaque-les!
24 Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
Les enfants d'Israël s'avancèrent donc contre les enfants de Benjamin, le deuxième jour.
25 Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
Mais Benjamin sortit de Gibea à leur rencontre, le deuxième jour, et fit encore mordre la poussière à dix-huit mille hommes des enfants d'Israël, tous tirant l'épée.
26 Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
Alors tous les enfants d'Israël et tout le peuple montèrent et vinrent à Béthel, et pleurant ils s'assirent là devant l'Éternel, et ils jeûnèrent ce jour-là jusqu'au soir et offrirent à l'Éternel des holocaustes et des sacrifices pacifiques.
27 Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
Et les enfants d'Israël consultèrent l'Éternel (or à cette époque l'Arche de l'Alliance de Dieu était là;
28 na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
et Phinées, fils d'Eléazar, fils d'Aaron, était en charge devant Lui à cette époque) en disant: Dois-je derechef marcher au combat contre les enfants de Benjamin, mon frère, ou bien me désisterai-je? Et l'Éternel dit: Marchez, car demain je les livrerai entre vos mains.
29 Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
Alors Israël dressa une embuscade contre Gibea de tous les côtés.
30 Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
Et les enfants d'Israël marchèrent contre ceux de Benjamin le troisième jour, et ils prirent position devant Gibea cette fois comme les autres fois.
31 Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
Ensuite les enfants de Benjamin firent une sortie contre cette armée, et ils se laissèrent entraîner loin de la ville, et cette fois comme les autres fois ils se mirent à frapper et à tuer dans les rangs du peuple, sur les routes dont l'une mène à Béthel et l'autre à Gibea par la campagne, environ trente hommes d'Israël.
32 Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
Et les enfants de Benjamin disaient: Ils sont battus par nous, comme au début. Mais les enfants d'Israël disaient: Fuyons, afin de les attirer loin de la ville sur ces routes.
33 Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
Et tous les hommes d'Israël quittant leur position formèrent leur ligne à Baal-Thamar, et les Israélites embusqués s'élancèrent hors de leur retraite, de la steppe de Gibea.
34 Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
Et de devant Gibea s'avancèrent dix mille hommes d'élite de tout Israël, et l'action devint sérieuse. Or [les Benjaminites] ne se doutaient pas du désastre qu'ils allaient essuyer.
35 Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
Et l'Éternel battit Benjamin devant Israël; et les enfants d'Israël, dans cette journée, tuèrent à Benjamin vingt-cinq mille et cent hommes tous tirant l'épée.
36 Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
Les enfants de Benjamin voyaient déjà en déroute les enfants d'Israël qui cédaient le terrain aux Benjaminites, comptant sur l'embuscade qu'ils avaient dressée contre Gibea.
37 Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
Mais ces gens embusqués par un prompt mouvement assaillirent Gibea et l'occupèrent et frappèrent toute la ville avec le tranchant de l'épée.
38 Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
Or les hommes d'Israël étaient convenus avec les gens embusqués de ceci: « Faites en sorte qu'il s'élève de la ville un gros nuage de fumée. »
39 ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
C'est alors que dans la bataille les Israélites firent leur conversion, Benjamin commençant à tuer environ trente hommes à Israël et disant: Nul doute! ils sont battus par nous comme dans la première bataille.
40 Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
Cependant de la ville commençait à s'élever le nuage, une colonne de fumée; et les Benjaminites regardèrent derrière eux, et voilà que toute la ville en feu s'élevait vers le ciel.
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
Et les Israélites ayant fait leur conversion, les hommes de Benjamin furent éperdus, car ils se voyaient sous le coup du désastre.
42 Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
Et tournant le dos aux Israélites ils prirent le chemin du désert; mais les combattants s'acharnèrent sur leurs traces, et massacrant ceux des villes dans les villes,
43 Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
cernant et poursuivant Benjamin, l'écrasant quand il s'arrêtait, et cela jusque vis-à-vis de Gibea du côté du soleil levant.
44 Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
Et ainsi périrent dix-huit mille hommes de Benjamin, tous braves guerriers.
45 Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
Et ayant tourné le dos, ils s'enfuirent dans le désert au rocher de Rimmon; mais les Israélites firent sur les routes une glanure de cinq mille hommes, et les poursuivirent jusqu'à Gédéon, et ils en tuèrent deux mille.
46 Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
Et la totalité des Benjaminites tués dans cette journée fut de vingt-cinq mille hommes tirant l'épée et tous braves guerriers.
47 Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
Et il y eut six cents hommes qui ayant tourné le dos s'enfuirent dans le désert au rocher de Rimmon et ils y demeurèrent quatre mois.
48 Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.
Et les Israélites revinrent aux Benjaminites [restants], et ils les frappèrent avec le tranchant de l'épée depuis les hommes des villes jusqu'au bétail et à tout ce qui se trouva, ils incendièrent aussi toutes les villes qu'ils rencontrèrent.

< Waamuzi 20 >