< Waamuzi 20 >

1 Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
Tous les Israélites se mirent en mouvement, depuis Dan jusqu’à Bersabée et le pays de Galaad, et se rendirent ensemble, comme un seul homme, devant l’Eternel, à Miçpa.
2 Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
Toutes les sommités du peuple, de toutes les tribus d’Israël, assistèrent à cette assemblée du peuple de Dieu, composée de quatre cent mille hommes de pied, sachant tirer l’épée.
3 (Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
Les Benjamites furent informés que les enfants d’Israël étaient montés à Miçpa. Les enfants d’Israël dirent: "Expliquez-nous comment est arrivée cette chose odieuse!"
4 Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
Alors le lévite, celui dont la femme avait été assassinée, prit la parole et dit: "J’Étais venu à Ghibea-en-Benjamin, avec ma concubine, pour y passer la nuit.
5 Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
Et les habitants de Ghibea se sont levés contre moi, et ont cerné de nuit la maison où j’étais; ils avaient le projet de me tuer, et ils ont abusé de ma concubine au point qu’elle en est morte.
6 Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
Alors j’ai pris son corps, l’ai coupé en morceaux et l’ai envoyé dans toute la campagne du territoire d’Israël; car ils avaient commis un acte honteux et criminel en Israël.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
Vous voici, tous, enfants d’Israël; avisez ici même et prenez un parti!"
8 Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
Tout le peuple se leva comme un seul homme en disant: "Aucun d’entre nous ne rentrera dans sa tente, ni ne se retirera dans sa maison!
9 Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
Et maintenant, voici comment nous agirons contre Ghibea: nous procéderons par un tirage au sort,
10 Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
et prendrons ainsi, dans toutes les tribus d’Israël, dix hommes sur cent, cent sur mille, mille sur dix mille, qui seront chargés des subsistances du peuple, tandis que celui-ci marchera sur Ghibea-en-Benjamin, pour châtier l’infamie qu’il a commise en Israël."
11 Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
Et tous les hommes d’Israël marchèrent ensemble contre la ville, unis comme un seul homme.
12 Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
Les tribus d’Israël envoyèrent d’abord des hommes dans toutes les familles de Benjamin, pour leur dire: "Qu’est-ce que ce méfait qui s’est commis chez vous?
13 Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
Maintenant livrez-nous ces hommes indignes qui sont à Ghibea, pour que nous les mettions à mort et fassions disparaître le mal du sein d’Israël." Mais les enfants de Benjamin ne voulurent pas céder à la voix des Israélites leurs frères,
14 Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
et ils se rendirent en masse des autres villes à Ghibea, pour engager la lutte avec les enfants d’Israël.
15 Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
Les Benjamites de ces villes, s’étant comptés, formaient alors un total de vingt-six mille hommes tirant l’épée, outre les habitants de Ghibea, qui fournirent au dénombrement sept cents hommes d’élite:
16 Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
élite de toute cette armée, ces sept cents hommes étaient gauchers, et, avec la pierre de leurs frondes, visaient un cheveu sans le manquer.
17 Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
De leur côté, les Israélites, moins Benjamin, s’étant dénombrés, comptaient quatre cent mille hommes sachant manier l’épée, tous hommes de guerre.
18 Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
Ceux-ci montèrent à Béthel pour consulter le Seigneur en ces termes: "Lequel de nous doit marcher le premier au combat contre les Benjamites?" L’Eternel répondit: "Juda sera le premier."
19 Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
Les Israélites se mirent en marche le lendemain matin, et dressèrent leur camp devant Ghibea.
20 Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
Puis ils s’avancèrent pour livrer bataille aux Benjamites, et engagèrent la lutte avec eux sous les murs de Ghibea.
21 Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
Mais les Benjamites se jetèrent hors de Ghibea et firent ce jour-là mordre la poussière à vingt-deux mille hommes d’Israël.
22 Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
L’Armée israélite, sans perdre courage, se rangea de nouveau en bataille au même lieu que le premier jour.
23 Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
Et les Israélites montèrent pleurer devant le Seigneur jusqu’au soir et le consultèrent en disant: "Dois-je engager une seconde bataille avec Benjamin mon frère?" A quoi le Seigneur répondit: "Marchez contre lui."
24 Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
Les enfants d’Israël s’avancèrent donc une seconde fois contre ceux de Benjamin.
25 Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
Et ceux-ci, ayant fait de Ghibea une nouvelle sortie contre eux, ce second jour, couchèrent encore dans la poussière dix-huit mille hommes d’Israël, tous habiles à manier l’épée.
26 Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
Alors tous les Israélites et toute la population montèrent à Béthel et restèrent là, devant l’Eternel, se lamentant et jeûnant toute la journée jusqu’au soir, et ils offrirent des holocaustes et des rémunératoires à l’Eternel;
27 Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
et les Israélites consultèrent l’Eternel (car l’arche d’alliance du Seigneur était là à cette époque,
28 na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
et Phinéas, fils d’Eléazar fils d’Aaron, fonctionnait devant lui en ce même temps), et ils dirent: "Dois-je encore aller en guerre contre mon frère Benjamin, ou cesser les hostilités?" Et l’Eternel répondit: "Marchez! car demain je le mettrai en votre puissance."
29 Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
Alors les Israélites dressèrent des embuscades tout autour de Ghibea,
30 Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
marchèrent une troisième fois contre les Benjamites, et s’avancèrent en bon ordre contre Ghibea, comme précédemment.
31 Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
Les Benjamites firent une sortie contre eux, ce qui les éloigna de la ville, et ils commencèrent à leur infliger des pertes comme précédemment, faisant périr sur les routes de la campagne, dont l’une conduit è Béthel, l’autre à Ghibea, environ trente hommes d’Israël.
32 Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
Les enfants de Benjamin se dirent: "Les voilà battus par nous comme auparavant!" Mais les enfants d’Israël s’étaient dit: "Nous allons fuir, pour les attirer hors de la ville sur les routes."
33 Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
Le gros de l’armée d’Israël quitta donc sa position et alla se ranger à Baal-Tamar, tandis que les Israélites embusqués débouchaient de leur poste, de la prairie de Ghibea.
34 Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
Dix mille hommes, des meilleurs guerriers d’Israël, arrivèrent ainsi à l’opposite de Ghibea, et l’attaque fut terrible; mais les Benjamites ne se doutaient pas du désastre qui les atteignait.
35 Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
Le Seigneur fit succomber Benjamin sous les armes d’Israël, et les Israélites, ce jour-là, tuèrent à Benjamin vingt-cinq mille cent hommes, tous experts à l’épée.
36 Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
Les Benjamites avaient donc jugé leurs ennemis battus; mais ceux-ci leur avaient cédé le terrain, parce qu’ils comptaient sur l’embuscade qu’ils avaient postée près de Ghibea.
37 Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
De fait, les hommes embusqués fondirent prestement sur Ghibea, se répandirent par la ville et passèrent tout au fil de l’épée.
38 Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
Les hommes d’Israël étaient convenus d’un signal avec ceux de l’embuscade: celle-ci devait faire monter de la ville une masse épaisse de fumée.
39 ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
Donc, le combat engagé, les Israélites tournèrent le dos, et Benjamin commença à leur tuer du monde, environ trente hommes, persuadé qu’il les battrait comme au combat précédent.
40 Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
En ce moment, la fumée commença à s’élever de la ville en colonne épaisse; et Benjamin, en se retournant, vit toute la ville se dissiper en fumée dans les airs.
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
Et les hommes d’Israël firent volte-face, et ceux de Benjamin furent éperdus, voyant leur désastre imminent.
42 Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
Et ils s’enfuirent devant ceux d’Israël dans la direction du désert, mais l’attaque les y suivit, tandis que ceux des villes les exterminaient à l’intérieur.
43 Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
On cerna Benjamin, on le poursuivit à outrance, on l’écrasa à chaque halte, jusqu’à l’opposite de Ghibea à l’orient.
44 Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
Il périt ainsi de Benjamin dix-huit mille hommes, tous braves guerriers.
45 Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
Les autres s’enfuirent au désert, vers la Roche de Rimmon; on les écharpa sur les routes, au nombre de cinq mille hommes, et continuant la poursuite jusqu’a Ghideôm, on en tua encore deux mille.
46 Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
Le total des pertes de Benjamin, en cette occurrence, fut donc de vingt-cinq mille hommes, tous braves guerriers.
47 Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
Six cents hommes purent s’enfuir au désert, vers la Roche de Rimmon, où ils demeurèrent quatre mois.
48 Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.
De leur côté, les Israélites, se retournant contre la tribu de Benjamin, y passèrent au fil de l’épée la population entière des villes jusqu’au bétail, tout ce qu’ils rencontrèrent; et toutes les villes qui s’y trouvaient, ils les livrèrent aux flammes.

< Waamuzi 20 >