< Waamuzi 20 >

1 Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
And so all the sons of Israel went out like one man, from Dan to Beersheba, with the land of Gilead, and they gathered together, before the Lord, at Mizpah.
2 Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
And all the chiefs of the people, and every tribe of Israel, convened as an assembly of the people of God, four hundred thousand foot soldiers for battle.
3 (Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
(But it was not hidden from the sons of Benjamin that the sons of Israel had ascended to Mizpah.) And the Levite, the husband of the woman who was killed, being questioned as to how so great a crime had been perpetrated,
4 Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
responded: “I went to Gibeah of Benjamin, with my wife, and I diverted to that place.
5 Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
And behold, the men of that city, at night, surrounded the house in which I was staying, intending to kill me. And they abused my wife with such an incredible fury of lust that in the end she died.
6 Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
And taking her up, I cut her into pieces, and I sent the parts into all the borders of your possession. For never before was such a nefarious crime, and so great a sin, committed in Israel.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
You are all present here, O sons of Israel. Discern what you ought to do.”
8 Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
And all the people, standing, responded as if with the word of one man: “We shall not return to our own tents, nor shall anyone enter into his own house.
9 Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
But this we shall do in common against Gibeah:
10 Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
We shall select ten men out of one hundred from all the tribes of Israel, and one hundred out of one thousand, and one thousand out of ten thousand, so that they may transport supplies for the army, and so that we will be able to fight against Gibeah of Benjamin, and to repay it for its crime as it deserves.”
11 Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
And all of Israel convened against the city, like one man, with one mind and one counsel.
12 Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
And they sent messengers to the entire tribe of Benjamin, who said: “Why has so great a wickedness been found among you?
13 Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
Deliver the men of Gibeah, who have perpetrated this deplorable act, so that they may die, and so that the evil may be taken away from Israel.” And they were not willing to listen to the command of their brothers, the sons of Israel.
14 Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
Instead, out of all the cities that were their lot, they convened at Gibeah, so that they might bring them assistance, and so that they might contend against the entire people of Israel.
15 Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
And there were found from Benjamin twenty-five thousand who drew the sword, aside from the inhabitants of Gibeah,
16 Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
who were seven hundred very strong men, fighting with the left hand as well as with the right hand, and casting stones from a sling so accurately that they were able to strike even a hair, and the path of the stone would by no means miss to either side.
17 Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
Then too, among the men of Israel apart from the sons of Benjamin, there were found four hundred thousand who drew the sword and who were prepared for battle.
18 Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
And they rose up and went to the house of God, that is, to Shiloh. And they consulted God, and they said, “Who shall be, in our army, the first to contend against the sons of Benjamin?” And the Lord responded to them, “Let Judah be your leader.”
19 Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
And immediately the sons of Israel, rising up in the morning, made camp near Gibeah.
20 Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
And setting out from there to fight against Benjamin, they began to assault the city.
21 Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
And the sons of Benjamin, departing from Gibeah, slew twenty-two thousand men from the sons of Israel, on that day.
22 Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
Again the sons of Israel, trusting in both strength and number, set their troops in order, in the same place where they had contended before.
23 Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
But first they also went up and wept before the Lord, even until night. And they consulted him and said, “Should I continue to go forth, so as to contend against the sons of Benjamin, my brothers, or not?” And he responded to them, “Ascend against them, and undertake the struggle.”
24 Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
And when the sons of Israel had continued to do battle against the sons of Benjamin on the next day,
25 Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
the sons of Benjamin burst forth from the gates of Gibeah. And meeting them, they made such a frenzied slaughter against them that they struck down eighteen thousand men who drew the sword.
26 Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
As a result, all the sons of Israel went to the house of God, and sitting down, they wept before the Lord. And they fasted that day until evening, and they offered to him holocausts and victims of peace offerings.
27 Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
And they inquired about their state. At that time, the ark of the covenant of the Lord was in that place.
28 na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
And Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron, was the first ruler of the house. And so, they consulted the Lord, and they said, “Should we continue to go forth in battle against the sons of Benjamin, our brothers, or should we cease?” And the Lord said to them: “Ascend. For tomorrow, I will deliver them into your hands.”
29 Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
And the sons of Israel stationed ambushes around the city of Gibeah.
30 Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
And they brought out their army against Benjamin a third time, just as they had done on the first and second times.
31 Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
But the sons of Benjamin again burst forth boldly from the city. And since their enemies were fleeing, they pursued them a long way, so that they might wound or kill some of them, just as they had done on the first and second days. And they turned their backs along two paths, one bringing them toward Bethel, and the other toward Gibeah. And they struck down about thirty men.
32 Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
For they thought that they were falling back as they had done before. But instead, skillfully feigning flight, they undertook a plan to draw them away from the city, and by seeming to flee, to lead them along the above stated paths.
33 Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
And so all the sons of Israel, rising up from their positions, set their troops in order, in the place which is called Baaltamar. Likewise, the ambushes that encircled the city began, little by little, to reveal themselves,
34 Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
and to advance upon the western part of the city. Moreover, another ten thousand men from all of Israel were provoking a conflict with the inhabitants of the city. And the war grew heavy against the sons of Benjamin. And they did not realize that, on all sides of them, death was imminent.
35 Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
And the Lord struck them down in the sight of the sons of Israel, and they put to death, on that day, twenty-five thousand of them, along with one hundred men, all warriors and those who drew the sword.
36 Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
But the sons of Benjamin, when they had seen themselves to be the weaker, began to flee. And the sons of Israel discerning this, gave them room to flee, so that they might arrive at the ambushes that were prepared, which they had positioned near the city.
37 Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
And after they had risen up suddenly from hiding, and those of Benjamin had turned their backs to those who cut them down, they entered the city, and they struck it with the edge of the sword.
38 Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
Now the sons of Israel had given a sign to those whom they had stationed in ambushes, so that, after they had seized the city, they would light a fire, and by the smoke ascending on high, they would show that the city was captured.
39 ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
And then, the sons of Israel discerned this sign during the battle (for the sons of Benjamin had thought that they fled, and they pursued them forcefully, cutting down thirty men from their army).
40 Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
And they saw something like a pillar of smoke ascending from the city. Likewise, Benjamin, looking back, discerned that the city was captured, for the flames were being carried on high.
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
And those who before had pretended to flee, turning their faces, withstood them more strongly. And when the sons of Benjamin had seen this, they turned their backs in flight,
42 Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
and they began to go toward the way of the desert, with the adversary pursuing them to that place also. Moreover, those who had set fire to the city also met them.
43 Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
And so it happened that they were cut down on both sides by the enemies, nor was there any respite for the dying. They were killed and struck down on the eastern side of the city of Gibeah.
44 Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
Now those who were put to death in the same place were eighteen thousand men, all very robust fighters.
45 Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
And when those who remained of Benjamin had seen this, they fled into the wilderness. And they were traveling toward the rock which is called Rimmon. In that flight also, among those who were scattering in different directions, they slew five thousand men. And though they scattered all the more, they continued to pursue them, and then they put to death another two thousand.
46 Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
And so it happened that all of those who were slain from Benjamin, in various places, were twenty-five thousand fighters, very willing to go to war.
47 Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
And so there remained from the entire number of Benjamin six hundred men who were able to escape and to flee into the wilderness. And they settled at the rock of Rimmon, for four months.
48 Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.
But the sons of Israel, returning, had struck with the sword all that remained in the city, from men even to cattle. And all the cities and villages of Benjamin were consumed with devouring flames.

< Waamuzi 20 >