< Waamuzi 2 >
1 Malaika wa Bwana akakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.
L’ange de Yahweh monta de Galgala à Bokim, et dit: « Je vous ai fait monter hors d’Égypte et je vous ai amenés dans le pays que j’ai juré à vos pères de vous donner. J’ai dit: Jamais je ne romprai mon alliance avec vous;
2 Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu yao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?
et vous, vous ne ferez, point alliance avec les habitants de ce pays, vous renverserez leurs autels. Mais vous n’avez pas obéi à ma voix. Pourquoi avez-vous fait cela?
3 Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”
Et moi aussi, j’ai dit: Je ne les chasserai point devant vous; ils seront à vos côtés, et leurs dieux vous seront un piège. »
4 Malaika wa Bwana alipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.
Comme l’ange de Yahweh disait ces paroles à tous les enfants d’Israël, le peuple éleva la voix et pleura.
5 Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtolea Bwana sadaka.
Ils donnèrent à ce lieu le nom de Bokim, et ils y offrirent des sacrifices à Yahweh.
6 Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.
Josué renvoya le peuple, et les enfants d’Israël s’en allèrent chacun dans son héritage pour prendre possession du pays.
7 Watu wakamtumikia Bwana siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, waliokuwa wameona mambo makuu ambayo Bwana alikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.
Le peuple servit Yahweh pendant toute la vie de Josué, et pendant toute la vie des anciens qui survécurent à Josué et qui avaient vu toute la grande œuvre que Yahweh avait accomplie en faveur d’Israël.
8 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.
Josué, fils de Nun, serviteur de Yahweh, mourut âgé de cent dix ans.
9 Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresi katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.
On l’ensevelit dans le territoire qu’il avait eu en partage, à Thamnath-Hérès, dans la montagne d’Ephraïm, au nord du mont Gaas.
10 Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjua Bwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.
Toute cette génération fut aussi recueillie auprès de ses pères, et il s’éleva après elle une autre génération qui ne connaissait pas Yahweh, ni l’œuvre qu’il avait faite en faveur d’Israël.
11 Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Bwana na kuwatumikia Mabaali.
Les enfants d’Israël firent ce qui est mal aux yeux de Yahweh, et ils servirent les Baals.
12 Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. Wakamkasirisha Bwana,
Ils abandonnèrent Yahweh, le Dieu de leurs pères, qui les avait fait sortir du pays d’Égypte, et ils allèrent après d’autres dieux, d’entre les dieux des peuples qui les entouraient; ils se prosternèrent devant eux et ils irritèrent Yahweh.
13 kwa sababu walimwacha na kutumikia Baali na Maashtorethi.
Abandonnant Yahweh, ils servirent Baal et les Astartés.
14 Hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.
La colère de Yahweh s’enflamma contre Israël; il les livra aux mains des pillards qui les pillèrent, et il les vendit entre les mains de leurs ennemis d’alentour, et ils ne purent plus tenir devant leurs ennemis.
15 Popote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.
Partout où ils allaient, la main de Yahweh était contre eux pour leur malheur, comme Yahweh l’avait dit, comme Yahweh le leur avait juré, et ils en vinrent à une grande détresse.
16 Ndipo Bwana akawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.
Yahweh suscitait des juges qui les délivraient de la main de ceux qui les pillaient.
17 Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri za Bwana.
Mais ils n’écoutèrent pas leurs juges, car ils se prostituèrent à d’autres dieux et se prosternèrent devant eux. Ils se détournèrent promptement de la voie qu’avaient suivie leurs pères en obéissant aux commandements de Yahweh; ils ne firent pas de même.
18 Kila mara Bwana alipowainulia mwamuzi, Bwana alikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwa Bwana aliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.
Lorsque Yahweh leur suscitait des juges, Yahweh était avec le juge et il les délivrait de la main de leurs ennemis, tant que le juge vivait; car Yahweh se repentait à cause de leurs gémissements devant ceux qui les opprimaient et les tourmentaient.
19 Lakini kila mara mwamuzi alipofariki, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.
Mais, à la mort du juge, ils se corrompaient de nouveau plus que leurs pères, en allant après d’autres dieux pour les servir et se prosterner devant eux; ils n’abandonnaient pas leurs errements et leur opiniâtreté.
20 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,
Alors la colère de Yahweh s’enflamma contre Israël, et il dit: « Puisque cette nation a transgressé mon alliance que j’avais prescrite à ses pères, et puisqu’ils n’ont pas obéi à ma voix,
21 mimi nami sitafukuza taifa lolote ambalo Yoshua aliliacha alipofariki.
moi, je ne chasserai plus devant eux une seule des nations que Josué a laissées quand il est mort,
22 Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia ya Bwana na kuenenda katika hiyo kama njia baba zao walivyofanya.”
afin de mettre par elles Israël à l’épreuve, pour voir s’ils seront attentifs, ou non, à suivre la voie de Yahweh, comme leurs pères y ont été attentifs. »
23 Bwana alikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.
Et Yahweh laissa en repos, sans se hâter de les chasser, ces nations qu’il n’avait pas livrées entre les mains de Josué.