< Waamuzi 19 >

1 Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme. Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda.
Or, il y avait dans les montagnes d'Ephraïm un lévite qui prit une femme concubine de Bethléem en Juda;
2 Lakini suria wake akafanya ukahaba dhidi yake, naye akamwacha akarudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne,
Puis, sa femme le quitta pour s'en retourner à la maison de son père, à Bethléem en Juda; elle y était depuis quatre mois entiers,
3 mume wake akaenda kumsihi ili arudi. Alikwenda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha.
Quand son mari, s'étant levé, s'en alla vers elle pour parler à son cœur et la ramener avec lui; il emmenait son serviteur et deux ânes. Elle l'introduisit dans la maison de son père; le père de la jeune femme le vit, et il fut joyeux de la rencontre.
4 Baba mkwe wake, yaani, baba yake yule msichana, akamzuia ili akae, hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila, wakinywa na kulala huko.
Le beau-père du lévite, le père de la jeune femme retint son gendre, qui resta avec lui trois jours; ils mangèrent, ils burent et ils logèrent chez lui.
5 Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kula kitu chochote, ndipo uweze kwenda.”
Le quatrième jour parut; et, s'étant levé de grand matin, ils se préparèrent à partir. Et le père de la femme dit au jeune époux: Fortifie ton cœur par une bouchée de pain; après cela, vous partirez.
6 Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha nafsi yako.”
Tous les deux s'assirent donc, ils mangèrent et burent ensemble, et le père de la jeune femme dit à l'époux: Allons, passe ici la nuit, et ton cœur s'en trouvera bien.
7 Basi yule mtu alipotaka kuondoka baba wa yule msichana akamsihi, basi akabaki usiku ule.
Mais l'homme se leva pour partir; puis, son père le contraignant, il s'assit, et il passa la nuit dans la maison.
8 Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja mpaka mchana!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.
Le cinquième jour, il se leva de grand matin pour s'en aller, et le père de la jeune femme lui dit: Fortifie ton cœur, reste ici jusqu'au déclin du jour. Et ils mangèrent ensemble.
9 Basi wakati yule mtu alipoinuka aende zake, pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba wa yule msichana akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka mapema asubuhi na uende nyumbani kwako.”
Quand l'homme se leva pour partir avec sa femme et son serviteur, son beau-père, le père de la jeune femme lui dit: Voilà que, le jour décline vers le soir, passe la nuit avec nous, et ton cœur s'en trouvera bien; demain, vous vous lèverez de grand matin, et tu retourneras en ta demeure.
10 Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kwenda mpaka Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikiwa, pamoja na suria wake.
Mais l'homme ne consentit point à passer là encore une nuit; il se leva et partit, et il alla jusqu'en face de Jébus, la même que Jérusalem; il avait avec lui ses deux ânes chargés, et sa femme.
11 Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”
Ils poussèrent donc jusqu'à Jébus. Or, le jour était bien avancé, et le serviteur dit à son maître: Viens, et nous entrerons dans cette ville de Jébus, et nous y passerons la nuit.
12 Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea mpaka tufike Gibea.”
Le maître lui dit: N'entre pas dans une ville étrangère, où il n'y a point de fils d'Israël; allons jusqu'à Gabaa.
13 Akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji mmojawapo.”
Puis, il ajouta: Allons, approchons-nous de l'une de ces deux villes; nous logerons à Gabaa ou à Rhama.
14 Hivyo wakaendelea na safari, jua likachwea walipokaribia Gibea ambao ni mji wa Benyamini.
Et, passant outre, ils marchèrent; le soleil se coucha comme ils traversaient le territoire de Gabaa, qui est de la tribu de Benjamin.
15 Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.
Ils entrèrent en cette ville pour y passer la nuit; et étant entrés, ils s'assirent sur la place de la ville. Or, il n'y eut pas un homme qui les conduisit dans sa maison afin de les loger.
16 Jioni ile mtu mmoja mzee toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi za shamba.
Cependant, un homme âgé revenait, sur le tard, de ses travaux des champs, et cet homme était des montagnes d'Ephraïm; il habitait Gabaa, et les hommes de cette ville étaient des fils de Benjamin.
17 Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnakwenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”
Il leva les yeux, et il vit le voyageur sur la place de la ville; alors, l'homme âgé lui dit: Où vas-tu, et d'où es-tu parti?
18 Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu, ambako ndiko ninakoishi. Nilikwenda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninakwenda katika nyumba ya Bwana. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake.
Et le lévite lui répondit: Nous allons de Bethléem en Juda, aux montagnes d'Ephraïm. Je suis de ce lieu; j'étais allé à Bethléem en Juda, et je retourne à ma maison, et il n'y a pas ici un homme qui me conduise en sa demeure.
19 Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu na mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako, yaani mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliyefuatana naye. Hatuhitaji kitu chochote.”
Cependant, nous avons pour nos ânes de la litière et du fourrage; nous avons du pain et du vin pour moi, ta servante et le jeune homme; aucune chose ne manque donc à tes serviteurs.
20 Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, msilale katika uwanja huu wa mji.”
Alors, l'homme âgé reprit: La paix soit avec toi; d'ailleurs, tu trouveras chez moi tout ce dont tu as besoin; tu ne passeras pas la nuit sur cette place.
21 Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.
Et il l'introduisit dans sa maison, où il prépara un endroit pour loger ses ânes; puis, ils se lavèrent les pieds, et ils mangèrent et ils burent.
22 Walipokuwa wakijiburudisha, watu waovu wa mji huo, wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema na yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mtu aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”
Ils étaient donc à se réjouir le cœur. Or, voilà que les hommes de la ville, fils de parents pervers, entourèrent la maison, frappèrent à la porte, et dirent à l'homme, au maître de la maison, au vieillard: Amène-nous l'homme qui est entré en ta demeure, afin que nous le connaissions.
23 Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mtu ni mgeni wangu msifanye jambo hili la aibu.
Et le maître de la maison sortit auprès d'eux, et il dit: Mes frères, ne maltraitez pas cet homme, après qu'il est entré dans ma maison; ne commettez pas une action si insensée.
24 Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira na suria wa huyu mtu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mtu huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”
J'ai une fille vierge, et lui a une femme; je vais vous les amener: déshonorez-les, traitez-les comme bon vous semblera; mais, avec cet homme, ne faites pas l'action insensée que vous dites.
25 Lakini wale watu hawakumsikia. Hivyo yule mtu akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku ule kucha mpaka asubuhi. Kulipoanza kupambazuka wakamwachia aende.
Mais les hommes ne consentirent point à l'écouter; enfin, le lévite prit sa femme, et il la leur conduisit au dehors; ils la connurent et l'outragèrent toute la nuit jusqu'au matin, et ils la renvoyèrent lorsqu'ils virent poindre le jour.
26 Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.
Et la femme s'en fut à l'aurore; elle tomba devant la porte de la maison où était son mari, elle y resta jusqu'au jour.
27 Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameanguka pale penye ingilio la nyumba na mikono yake ikiwa penye kizingiti cha chini.
Le lévite se leva dès le matin; il ouvrit la porte de la maison, il sortit pour reprendre sa route, et voilà que la femme, sa concubine, était étendue devant la porte de la maison, les mains sur le seuil.
28 Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua akampandisha juu ya punda wake, wakaondoka kwenda nyumbani.
Et il lui dit: Lève-toi, et partons. Elle ne répondit point, car elle était morte. Et il la plaça sur un âne, et il l'emmena où il demeurait.
29 Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, sehemu kumi na mbili, na kuvipeleka hivyo vipande katika sehemu zote za Israeli.
Là, saisissant son glaive, il prit sa femme, et il la divisa en douze parts, qu'il envoya par tout Israël.
30 Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Israeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”
Et tout homme qui les vit s'écria: Jamais, depuis le jour où les fils d'Israël sortirent d'Egypte jusqu'à celui-ci, pareille chose ne s'est vue. Tenez conseil au sujet de cette femme, et parlez.

< Waamuzi 19 >