< Waamuzi 19 >

1 Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme. Basi Mlawi mmoja aliyeishi sehemu za mbali katika nchi ya vilima ya Efraimu, akamchukua suria mmoja kutoka Bethlehemu ya Yuda.
and to be in/on/with day [the] they(masc.) and king nothing in/on/with Israel and to be man Levi to sojourn in/on/with flank mountain: hill country Ephraim and to take: take to/for him woman: wife concubine from Bethlehem Bethlehem Judah
2 Lakini suria wake akafanya ukahaba dhidi yake, naye akamwacha akarudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Baada ya kukaa huko kwa muda wa miezi minne,
and to fornicate upon him concubine his and to go: went from with him to(wards) house: home father her to(wards) Bethlehem Bethlehem Judah and to be there day four month
3 mume wake akaenda kumsihi ili arudi. Alikwenda na mtumishi wake na punda wawili. Yule mwanamke akamkaribisha nyumbani mwa baba yake, baba yake alipomwona akamkaribisha kwa furaha.
and to arise: rise man: husband her and to go: went after her to/for to speak: speak upon heart her (to/for to return: rescue her *Q(K)*) and youth his with him and pair donkey and to come (in): bring him house: home father her and to see: see him father [the] maiden and to rejoice to/for to encounter: meet him
4 Baba mkwe wake, yaani, baba yake yule msichana, akamzuia ili akae, hivyo akakaa na huyo baba mkwe wake kwa siku tatu, wakila, wakinywa na kulala huko.
and to strengthen: hold in/on/with him relative his father [the] maiden and to dwell with him three day and to eat and to drink and to lodge there
5 Siku ya nne wakaamka mapema naye akajiandaa kuondoka, lakini baba wa yule msichana akamwambia mkwewe, “Ujiburudishe kwa kula kitu chochote, ndipo uweze kwenda.”
and to be in/on/with day [the] fourth and to rise in/on/with morning and to arise: rise to/for to go: went and to say father [the] maiden to(wards) son-in-law his to support heart your morsel food: bread and after to go: went
6 Basi wakaketi wote wawili ili kula na kunywa pamoja. Baadaye baba wa msichana akamwambia, “Tafadhali ubakie usiku huu upate kujifurahisha nafsi yako.”
and to dwell and to eat two their together and to drink and to say father [the] maiden to(wards) [the] man be willing please and to lodge and be good heart your
7 Basi yule mtu alipotaka kuondoka baba wa yule msichana akamsihi, basi akabaki usiku ule.
and to arise: rise [the] man to/for to go: went and to press in/on/with him relative his and to return: again and to lodge there
8 Asubuhi ya siku ya tano, alipoamka ili aondoke, baba wa yule msichana akamwambia, “Jiburudishe nafsi yako. Ngoja mpaka mchana!” Kwa hiyo wote wawili wakala chakula pamoja.
and to rise in/on/with morning in/on/with day [the] fifth to/for to go: went and to say father [the] maiden to support please heart your and to delay till to stretch [the] day and to eat two their
9 Basi wakati yule mtu alipoinuka aende zake, pamoja na suria wake na mtumishi wake, baba mkwe wake, yaani, baba wa yule msichana akamwambia, “Tazama sasa jioni inakaribia. Ulale hapa usiku unakaribia. Ukae, ukajifurahishe nafsi yako. Kesho unaweza kuamka mapema asubuhi na uende nyumbani kwako.”
and to arise: rise [the] man to/for to go: went he/she/it and concubine his and youth his and to say to/for him relative his father [the] maiden behold please to slacken [the] day to/for to grow dark to lodge please behold to camp [the] day to lodge here and be good heart your and to rise tomorrow to/for way: journey your and to go: went to/for tent: home your
10 Lakini akakataa kulala tena, akaondoka na kwenda mpaka Yebusi (ndio Yerusalemu), akiwa na punda wake wawili waliotandikiwa, pamoja na suria wake.
and not be willing [the] man to/for to lodge and to arise: rise and to go: went and to come (in): come till before Jebus he/she/it Jerusalem and with him pair donkey to saddle/tie and concubine his with him
11 Alipokaribia Yebusi na usiku ukiwa umekaribia, mtumishi akamwambia bwana wake, “Haya sasa natuingie katika mji huu wa Wayebusi tulale humo.”
they(masc.) with Jebus and [the] day to go down much and to say [the] youth to(wards) lord his to go: come! [emph?] please and to turn aside: turn aside to(wards) city [the] Jebusite [the] this and to lodge in/on/with her
12 Lakini bwana wake akamjibu, “Hapana. Hatutaingia kwenye mji wa kigeni, ambao watu wake si Waisraeli. Tutaendelea mpaka tufike Gibea.”
and to say to(wards) him lord his not to turn aside: turn aside to(wards) city foreign which not from son: descendant/people Israel they(fem.) and to pass till Gibeah
13 Akasema, “Haya, tujitahidi tufike Gibea au Rama, nasi tutalala katika mji mmojawapo.”
and to say to/for youth his (to go: follow [emph?] *Q(K)*) and to present: come in/on/with one [the] place and to lodge in/on/with Gibeah or in/on/with Ramah
14 Hivyo wakaendelea na safari, jua likachwea walipokaribia Gibea ambao ni mji wa Benyamini.
and to pass and to go: went and to come (in): come to/for them [the] sun beside [the] Gibeah which to/for Benjamin
15 Wakageuka ili kuingia na kulala Gibea. Wakaingia humo, wakaketi kwenye uwanja wa mji, wala hakuna mtu yeyote aliyewakaribisha kwake ili wapate kulala.
and to turn aside: turn aside there to/for to come (in): come to/for to lodge in/on/with Gibeah and to come (in): come and to dwell in/on/with street/plaza [the] city and nothing man: anyone to gather [obj] them [the] house: home [to] to/for to lodge
16 Jioni ile mtu mmoja mzee toka nchi ya vilima ya Efraimu, aliyekuwa anaishi huko Gibea (watu wa sehemu ile walikuwa Wabenyamini), akarudi kutoka kwenye kazi za shamba.
and behold man old to come (in): come from deed: work his from [the] land: country in/on/with evening and [the] man from mountain: hill country Ephraim and he/she/it to sojourn in/on/with Gibeah and human [the] place Benjaminite Benjaminite
17 Alipotazama na kuwaona hao wasafiri katika uwanja wa mji, yule mzee akawauliza, “Ninyi mnakwenda wapi? Nanyi mmetoka wapi?”
and to lift: look eye his and to see: see [obj] [the] man [the] to journey in/on/with street/plaza [the] city and to say [the] man [the] old where? to go: went and from where? to come (in): come
18 Akamwambia, “Tumepita kutoka Bethlehemu ya Yuda, tunaelekea katika nchi ya vilima ya Efraimu, ambako ndiko ninakoishi. Nilikwenda Bethlehemu ya Yuda na sasa ninakwenda katika nyumba ya Bwana. Hakuna mtu yeyote aliyenikaribisha katika nyumba yake.
and to say to(wards) him to pass we from Bethlehem Bethlehem Judah till flank mountain: hill country Ephraim from there I and to go: went till Bethlehem Bethlehem Judah and [obj] house: temple LORD I to go: went and nothing man: anyone to gather [obj] me [the] house: home [to]
19 Tunazo nyasi na chakula cha punda wetu na mkate na divai kwa ajili yetu sisi watumishi wako, yaani mimi, mtumishi wako mwanamke, pamoja na huyu kijana tuliyefuatana naye. Hatuhitaji kitu chochote.”
and also straw also fodder there to/for donkey our and also food: bread and wine there to/for me and to/for maidservant your and to/for youth with servant/slave your nothing need all word: thing
20 Yule mzee akawaambia, “Amani iwe kwenu! Karibuni nyumbani mwangu. Nitawapa mahitaji yenu yote, msilale katika uwanja huu wa mji.”
and to say [the] man [the] old peace to/for you except all need your upon me except in/on/with street/plaza not to lodge
21 Hivyo akamwingiza nyumbani mwake na kuwalisha punda wake. Baada ya kunawa miguu yao, wakala na kunywa.
and to come (in): bring him to/for house: home his (and to feed *Q(k)*) to/for donkey and to wash: wash foot their and to eat and to drink
22 Walipokuwa wakijiburudisha, watu waovu wa mji huo, wakaizingira ile nyumba. Wakagonga mlango na kusema na yule mzee mwenye nyumba, “Mtoe nje yule mtu aliyeingia kwako, tupate kumlawiti.”
they(masc.) be good [obj] heart their and behold human [the] city human son: young animal Belial to turn: surround [obj] [the] house: home to beat upon [the] door and to say to(wards) [the] man master: men [the] house: home [the] old to/for to say to come out: send [obj] [the] man which to come (in): come to(wards) house: home your and to know him
23 Yule mwenye nyumba akatoka nje na kuwaambia, “Hapana, ndugu zangu msiwe waovu namna hii, ninawasihi. Kwa kuwa huyu mtu ni mgeni wangu msifanye jambo hili la aibu.
and to come out: come to(wards) them [the] man master [the] house: home and to say to(wards) them not brother: compatriot my not be evil please after which to come (in): come [the] man [the] this to(wards) house: home my not to make: do [obj] [the] folly [the] this
24 Tazameni, hapa yupo binti yangu ambaye ni bikira na suria wa huyu mtu. Nitawatoleeni hawa sasa, mkawatwae kwa nguvu na kuwafanyia lolote mtakalo. Lakini kwa mtu huyu msimfanyie jambo ovu hivyo.”
behold daughter my [the] virgin and concubine his to come out: send please [obj] them and to afflict [obj] them and to make: do to/for them [the] pleasant in/on/with eye: appearance your and to/for man [the] this not to make: do word: thing [the] folly [the] this
25 Lakini wale watu hawakumsikia. Hivyo yule mtu akamtoa yule suria wake nje kwa wale watu, nao wakambaka na kumnajisi usiku ule kucha mpaka asubuhi. Kulipoanza kupambazuka wakamwachia aende.
and not be willing [the] human to/for to hear: hear to/for him and to strengthen: hold [the] man in/on/with concubine his and to come out: come to(wards) them [the] outside and to know [obj] her and to abuse in/on/with her all [the] night till [the] morning and to send: let go her (like/as to ascend: dawn *Q(K)*) [the] dawn
26 Alfajiri yule mwanamke akarudi kwenye ile nyumba bwana wake alikokuwa, akaanguka chini mlangoni, akalala pale hata kulipopambazuka.
and to come (in): come [the] woman to/for to turn [the] morning and to fall: kill entrance house: home [the] man which lord her there till [the] light
27 Bwana wake alipoamka asubuhi na kufungua mlango wa nyumba na kutoka nje ili kuendelea na safari yake, tazama, yule suria wake alikuwa ameanguka pale penye ingilio la nyumba na mikono yake ikiwa penye kizingiti cha chini.
and to arise: rise lord her in/on/with morning and to open door [the] house: home and to come out: come to/for to go: went to/for way: journey his and behold [the] woman concubine his to fall: kill entrance [the] house: home and hand her upon [the] threshold
28 Akamwambia yule suria, “Inuka, twende.” Lakini hakujibu. Yule bwana akamwinua akampandisha juu ya punda wake, wakaondoka kwenda nyumbani.
and to say to(wards) her to arise: rise and to go: went and nothing to answer and to take: bring her upon [the] donkey and to arise: rise [the] man and to go: went to/for place his
29 Alipofika nyumbani, akachukua kisu na kumkatakata yule suria kiungo kwa kiungo, sehemu kumi na mbili, na kuvipeleka hivyo vipande katika sehemu zote za Israeli.
and to come (in): come to(wards) house: home his and to take: take [obj] [the] knife and to strengthen: hold in/on/with concubine his and to cut her to/for bone her to/for two ten piece and to send: depart her in/on/with all border: area Israel
30 Kila mtu aliyeona akasema, “Jambo la namna hii halijaonekana wala kutendeka, tangu Israeli walipopanda kutoka Misri. Fikirini juu ya jambo hili! Tafakarini juu ya jambo hili! Tuambieni tufanye nini!”
and to be all [the] to see: see and to say not to be and not to see: see like/as this to/for from day to ascend: rise son: descendant/people Israel from land: country/planet Egypt till [the] day: today [the] this to set: consider to/for you upon her to plan and to speak: speak

< Waamuzi 19 >