< Waamuzi 18 >

1 Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
W tych dniach nie było króla w Izraelu, toteż w tych dniach pokolenie Dana szukało sobie dziedzictwa do zamieszkania. Aż do tego dnia bowiem nie przypadło im dziedzictwo pośród pokoleń Izraela.
2 Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
Synowie Dana wyprawili więc ze swoich granic pięciu mężczyzn ze swego pokolenia, walecznych mężczyzn z Sorea i Esztaol, aby wyszpiegowali ziemię i zbadali ją. Powiedzieli do nich: Idźcie, zbadajcie ziemię. Ci przybyli [na] górę Efraim, aż do domu Micheasza, i tam przenocowali.
3 Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
Gdy byli blisko domu Micheasza, poznali głos młodzieńca Lewity. Wstąpili więc tam i zapytali go: Kto cię tu przyprowadził? I co tu robisz? I jaką masz tu sprawę?
4 Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
A on im odpowiedział: Tak a tak postąpił ze mną Micheasz, najął mnie i jestem jego kapłanem.
5 Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
I powiedzieli do niego: Prosimy, poradź się Boga, abyśmy się dowiedzieli, czy poszczęści się nam nasza droga, którą idziemy.
6 Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
I kapłan im odpowiedział: Idźcie w pokoju. PAN bowiem czuwa nad waszą drogą, którą idziecie.
7 Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
Poszło więc tych pięciu mężczyzn i przybyli do Lajisz. I zobaczyli, że lud, który w nim był, mieszkał beztrosko, według zwyczaju Sydończyków, spokojnie i bezpiecznie, i że nie było władcy, który by ich trapił w tej ziemi. Ponadto byli daleko od Sydończyków i nie mieli z nikim [żadnych] interesów.
8 Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
Gdy więc wrócili do swych braci do Sorea i Esztaol, ich bracia zapytali ich: Co [powiecie]?
9 Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
Odpowiedzieli: Wstańcie i wyruszajmy przeciwko nim. Widzieliśmy bowiem ziemię, a jest ona bardzo dobra. A wy stoicie? Nie ociągajcie się z wyruszeniem i wejściem do tej ziemi, aby ją posiąść.
10 Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
Gdy wejdziecie, przyjdziecie do ludu bezpiecznego, do ziemi przestronnej. Bóg bowiem dał ją w wasze ręce; to miejsce, gdzie nie brakuje niczego z tego wszystkiego, co jest na ziemi.
11 Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
I wyruszyło stamtąd z pokolenia Dana, z Sorea i Esztaol, sześciuset mężczyzn uzbrojonych do walki.
12 Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
Będąc w drodze, rozbili obóz przy Kiriat-Jearim w Judzie. Dlatego to miejsce nazywa się Machane-Dan aż do dziś. [A znajduje się] za Kiriat-Jearim.
13 Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
A kiedy wyruszyli stamtąd na górę Efraim, przybyli aż do domu Micheasza;
14 Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
I odezwało się tych pięciu mężczyzn, którzy szli, aby wyszpiegować ziemię Lajisz, i powiedzieli do swych braci: Czy wiecie, że w tych domach znajduje się efod i terafim, a także posąg ryty oraz posąg odlany? Rozważcie więc teraz, co macie czynić.
15 Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
Skierowali się więc tam i przyszli do domu młodzieńca Lewity, do domu Micheasza, i pozdrowili go.
16 Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
Lecz sześciuset mężczyzn uzbrojonych do walki, którzy byli z synów Dana, stało u wejścia do bramy.
17 Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
I tych pięciu mężczyzn, którzy poszli, aby wyszpiegować ziemię, zabrało ryty posąg, efod, terafim i odlany posąg. A kapłan stał u wejścia do bramy wraz z sześciuset mężczyznami uzbrojonymi do walki.
18 Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
A gdy ci, którzy weszli do domu Micheasza, wzięli ryty posąg, efod, terafim i odlany posąg, kapłan powiedział do nich: Co robicie?
19 Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
Oni odpowiedzieli mu: Milcz! Połóż rękę na usta i chodź z nami, i bądź dla nas ojcem i kapłanem. Czyż lepiej ci być kapłanem w domu jednego człowieka, czy być kapłanem całego pokolenia i rodu w Izraelu?
20 Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
I uradowało się serce kapłana. Wziął więc efod, terafim i ryty posąg i przyłączył się do tego ludu.
21 Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
A oni zawrócili i poszli, a przed sobą puścili dzieci i bydło oraz [to, co] kosztowniejsze.
22 Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
A gdy byli już daleko od domu Micheasza, wtedy mężczyźni, którzy [mieszkali] w domach blisko domu Micheasza, zebrali się i zaczęli ścigać synów Dana.
23 Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
I wołali za synami Dana. Ci zaś odwrócili się i powiedzieli do Micheasza: Co ci jest, że zebrałeś tych ludzi?
24 Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
I odpowiedział: Zabraliście moich bogów, które uczyniłem, oraz kapłana i poszliście sobie. Co mi więc pozostaje? Jak jeszcze możecie mówić: Co ci jest?
25 Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
Na to synowie Dana odpowiedzieli: Niech nie słyszymy za sobą twego głosu, by się nie rzucili na was rozgniewani ludzie, a straciłbyś swe życie i życie swego domu.
26 Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
Poszli więc synowie Dana swoją drogą, a Micheasz, widząc, że byli silniejsi od niego, zawrócił i poszedł do swego domu.
27 Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
Oni zaś zabrali to, co wykonał Micheasz, oraz kapłana, którego miał, i przybyli do Lajisz, do ludu spokojnego i bezpiecznego. I pobili go ostrzem miecza, a miasto spalili ogniem.
28 Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
A nie było nikogo, kto by ich ratował, gdyż byli daleko od Sydonu i nie mieli z nikim [żadnych] interesów. A [miasto] to [leżało] w dolinie, która jest w Bet-Rechob. Oni odbudowali miasto i zamieszkali w nim.
29 Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
I nazwali to miasto Dan od imienia swego ojca Dana, który urodził się Izraelowi. A przedtem miasto to nosiło nazwę Lajisz.
30 Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
I synowie Dana ustawili sobie ryty posąg. A Jonatan, syn Gerszona, syna Manassesa, on i jego synowie byli kapłanami dla pokolenia Dana aż do czasu uprowadzenia do niewoli [mieszkańców] tej ziemi.
31 Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.
Postawili sobie ten ryty posąg, który uczynił Micheasz, po wszystkie dni, póki dom Boży był w Szilo.

< Waamuzi 18 >