< Waamuzi 18 >

1 Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
En ces jours-là il n’y avait point de roi en Israël, et la tribu de Dan se cherchait une possession pour y habiter; car jusqu’à ce jour elle n’avait pas reçu de lot parmi les autres tribus.
2 Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
Les enfants de Dan envoyèrent donc cinq hommes de leur race et de leur famille, des plus vaillants de Saraa et d’Esthaol, pour explorer la terre, et l’examiner avec soin; et ils leur dirent: Allez et considérez la terre. Lorsque ceux-ci, s’étant mis en chemin, furent venus à la montagne d’Ephraïm, et qu’ils furent entrés dans la maison de Michas, ils s’y reposèrent;
3 Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
Et reconnaissant la voix du jeune Lévite, et se trouvant dans son logis, ils lui demandèrent: Qui t’a amené ici? qu’y fais-tu? pour quel motif as-tu voulu y venir?
4 Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
Il leur répondit: Michas a fait pour moi telle et telle chose, et il ma loué moyennant un salaire, pour que je lui serve de prêtre.
5 Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
Or, ils le prièrent de consulter le Seigneur, afin qu’ils pussent savoir s’ils feraient un heureux voyage, et si leur entreprise aurait son effet.
6 Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
Il leur répondit: Allez en paix, le Seigneur regarde votre voie, et le chemin par lequel vous allez.
7 Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
S’en allant donc, les cinq hommes vinrent à Laïs, et ils virent que le peuple y habitait sans aucune crainte, selon la coutume des Sidoniens, en sécurité et tranquille, personne absolument ne s’opposant à lui, ayant de grandes richesses, loin de Sidon, et séparé de tous les hommes.
8 Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
Et étant retournés vers leurs frères à Saraa et à Esthaol, ils répondirent à ceux qui leur demandèrent ce qu’ils avaient fait:
9 Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
Levez-vous, montons vers eux, car nous avons vu la terre très riche et très fertile; ne mettez point de négligence, et ne différez point. Allons, et possédons-la, il n’y aura aucun labeur.
10 Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
Nous entrerons chez des gens en sécurité, dans une contrée très étendue, et le Seigneur nous livrera un lieu dans lequel il n’y a manque d’aucune chose de ce qui est produit sur la terre.
11 Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
Ils partirent donc de la famille de Dan, c’est-à-dire de Saraa et d’Esthaol, six cents hommes, munis d’armes de guerre,
12 Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
Et, montant, ils demeurèrent à Cariathiarim de Juda; lequel lieu, depuis ce temps-là, reçut le nom de Camp de Dan, et il est derrière Cariathiarim.
13 Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
De là ils passèrent à la montagne d’Ephraïm. Et lorsqu’ils furent venus à la maison de Michas,
14 Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
Les cinq hommes qui auparavant avaient été envoyés pour considérer la terre de Laïs, dirent à tous leurs autres frères: Vous savez qu’en ces maisons-là il y a un ephod, des théraphims, une image taillée au ciseau, et une idole de fonte; voyez ce qui vous plaît.
15 Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
Lors donc qu’ils se furent un peu détournés, ils entrèrent dans la maison du jeune Lévite qui était dans la maison de Michas; et ils le saluèrent avec des paroles de paix.
16 Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
Cependant, les six cents hommes, tels qu’ils étaient armés, se tenaient devant la porte.
17 Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
Mais ceux qui étaient entrés dans la maison du jeune homme s’efforçaient d’enlever l’image taillée au ciseau, l’éphod, les théraphims et l’idole de fonte; et le prêtre se tenait devant la porte, les six cents hommes très vaillants se tenant non loin de là.
18 Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
Ceux donc qui étaient entrés enlevèrent l’image taillée au ciseau, l’éphod, les idoles, et celle de fonte. Le prêtre leur dit: Que faites-vous?
19 Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
Ils lui répondirent: Tais-toi, et mets ton doigt sur ta bouche; et viens avec nous, afin que nous t’ayons pour père et pour prêtre. Lequel est le meilleur pour toi, que tu sois prêtre dans la maison d’un homme, ou dans une tribu et une famille en Israël?
20 Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
Ce qu’ayant entendu, il acquiesça à leurs paroles, prit l’éphod, les idoles et l’image taillée au ciseau, et partit avec eux.
21 Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
Lorsqu’ils étaient en chemin, et qu’ils avaient fait aller devant eux les enfants, les bestiaux et tout ce qui était précieux,
22 Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
Et que déjà ils étaient loin de la maison de Michas, les hommes qui demeuraient dans la maison de Michas, s’appelant les uns les autres, les suivirent,
23 Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
Et se mirent à crier après eux. Ceux-ci s’étant retournés, dirent à Michas: Que demandes-tu? Pourquoi cries-tu?
24 Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
Il répondit: Vous m’avez enlevé mes dieux que je me suis faits, mon prêtre, et tout ce que j’ai, et vous dites: Qu’as-tu?
25 Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
Et les enfants de Dan lui dirent: Prends garde que tu ne nous parles davantage, que des hommes excités par la colère ne viennent contre toi, et que toi-même tu ne périsses avec toute ta maison.
26 Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
Et ils continuèrent ainsi leur chemin commencé. Mais Michas, voyant qu’ils seraient plus forts que lui, s’en retourna à sa maison.
27 Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
Cependant les six cents hommes emmenèrent le prêtre et ce que nous avons dit plus haut; et ils vinrent à Laïs, chez un peuple tranquille et en sécurité, et ils les frappèrent du tranchant du glaive, et livrèrent la ville aux flammes,
28 Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
Personne absolument ne portant secours aux habitants de Laïs, parce qu’ils habitaient loin de Sidon, et qu’ils n’avaient avec quelque homme que ce soit aucune société et aucun commerce. Or, la ville était située dans la contrée de Rohob; et l’ayant reconstruite, ils y habitèrent,
29 Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
Appelant cette ville du nom de Dan, selon le nom de leur père qu’avait engendré Israël, elle qui auparavant était appelée Laïs.
30 Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
Ils érigèrent pour eux l’image taillée au ciseau, et ils établirent Jonathan, fils de Gersam, fils de Moïse, et ses fils prêtres dans la tribu de Dan, jusqu’au jour de leur captivité.
31 Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.
Et l’idole de Michas demeura parmi eux pendant tout le temps que la maison de Dieu fut à Silo. En ces jours-là il n’y avait point de roi dans Israël.

< Waamuzi 18 >