< Waamuzi 18 >

1 Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
En ce temps-là il n'y avait point de roi en Israël; et la tribu de Dan cherchait en ce temps-là un domaine pour elle, afin d'y habiter; car jusqu'alors il ne lui était point échu d'héritage parmi les tribus d'Israël.
2 Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
Les enfants de Dan envoyèrent donc cinq hommes de leur famille, pris d'entre eux tous, gens vaillants, de Tsora et d'Eshthaol, pour explorer le pays et le reconnaître; et ils leur dirent: Allez, explorez le pays. Ils vinrent dans la montagne d'Éphraïm jusqu'à la maison de Mica, et ils y passèrent la nuit.
3 Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
Et comme ils étaient auprès de la maison de Mica, ils reconnurent la voix du jeune Lévite; et, s'étant approchés de cette maison, ils lui dirent: Qui t'a amené ici? que fais-tu dans ce lieu? et qu'as-tu ici?
4 Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
Et il répondit: Mica fait pour moi telle et telle chose, il me donne un salaire, et je lui sers de sacrificateur.
5 Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
Ils dirent encore: Nous te prions, consulte Dieu, afin que nous sachions si le voyage que nous entreprenons sera heureux.
6 Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
Et le sacrificateur leur dit: Allez en paix; l'Éternel a devant ses yeux le voyage que vous entreprenez.
7 Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
Ces cinq hommes partirent donc, et ils arrivèrent à Laïs. Ils virent que le peuple qui y était, habitait en sécurité, à la manière des Sidoniens, tranquille et confiant, sans que personne dans le pays eût autorité sur eux et leur fît injure en rien; ils étaient éloignés des Sidoniens, et ils n'avaient à faire avec personne.
8 Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
Ils revinrent ensuite auprès de leurs frères à Tsora et à Eshthaol, et leurs frères leur dirent: Que rapportez-vous?
9 Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
Et ils répondirent: Allons, montons contre eux; car nous avons vu le pays, et voici, il est très bon. Quoi! vous êtes sans rien dire? Ne soyez point paresseux à partir, pour aller posséder ce pays.
10 Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
Quand vous y entrerez, vous arriverez vers un peuple qui est en pleine sécurité. Le pays est de grande étendue, et Dieu l'a livré entre vos mains. C'est un lieu où rien ne manque de tout ce qui est sur la terre.
11 Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
Il partit donc de là, de Tsora et d'Eshthaol, de la famille de Dan, six cents hommes munis de leurs armes.
12 Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
Ils montèrent et campèrent à Kirjath-Jéarim, en Juda; et on a appelé ce lieu-là Machané-Dan (camp de Dan), jusqu'à ce jour; il est derrière Kirjath-Jéarim.
13 Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
Puis de là ils passèrent dans la montagne d'Éphraïm, et arrivèrent jusqu'à la maison de Mica.
14 Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
Alors les cinq hommes qui étaient allés pour explorer le pays de Laïs, prenant la parole, dirent à leurs frères: Savez-vous que dans ces maisons il y a un éphod et des théraphim, une image taillée et une image de fonte? Voyez donc maintenant ce que vous avez à faire.
15 Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
Alors ils s'approchèrent de là, et entrèrent dans la maison du jeune Lévite, dans la maison de Mica, et le saluèrent.
16 Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
Or, les six cents hommes d'entre les fils de Dan, qui étaient sous les armes, s'arrêtèrent à l'entrée de la porte.
17 Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
Mais les cinq hommes qui étaient allés pour explorer le pays, montèrent, entrèrent dans la maison, et prirent l'image taillée, l'éphod, les théraphim et l'image de fonte, pendant que le sacrificateur était à l'entrée de la porte, avec les six cents hommes armés.
18 Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
Étant donc entrés dans la maison de Mica, ils prirent l'image taillée, l'éphod, les théraphim et l'image de fonte. Et le sacrificateur leur dit: Que faites-vous?
19 Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
Mais ils lui dirent: Tais-toi, et mets ta main sur ta bouche, et viens avec nous; tu nous serviras de père et de sacrificateur. Lequel vaut mieux pour toi, d'être sacrificateur de la maison d'un seul homme, ou d'être sacrificateur d'une tribu et d'une famille en Israël?
20 Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
Alors le sacrificateur eut de la joie en son cœur; il prit l'éphod, les théraphim et l'image taillée, et se mit au milieu du peuple.
21 Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
Ils se remirent donc en chemin, et marchèrent, en plaçant devant eux les petits enfants, le bétail et les bagages.
22 Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
Ils étaient déjà loin de la maison de Mica, lorsque ceux qui étaient dans les maisons voisines de celle de Mica, se rassemblèrent à grand cri, et poursuivirent les enfants de Dan.
23 Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
Et ils crièrent après eux. Mais eux, tournant visage, dirent à Mica:
24 Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
Qu'as-tu, que tu cries ainsi? Il répondit: Vous avez enlevé mes dieux, que j'avais faits, ainsi que le sacrificateur, et vous êtes partis. Que me reste-t-il? Et comment me dites-vous: Qu'as-tu?
25 Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
Mais les enfants de Dan lui dirent: Ne nous fais point entendre ta voix, de peur que des hommes irrités ne se jettent sur vous, et que vous n'y laissiez la vie, toi et ta famille.
26 Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
Les descendants de Dan continuèrent donc leur chemin. Et Mica, voyant qu'ils étaient plus forts que lui, tourna visage et revint en sa maison.
27 Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
Ainsi, ayant pris les choses que Mica avait faites et le sacrificateur qu'il avait, ils tombèrent sur Laïs, sur un peuple tranquille et qui se croyait en sûreté; et ils le firent passer au fil de l'épée; puis, ayant mis le feu à la ville, ils la brûlèrent.
28 Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
Et il n'y eut personne qui la délivrât; car elle était loin de Sidon; ses habitants n'avaient aucun commerce avec personne, et elle était située dans la vallée qui s'étend vers Beth-Réhob. Ils rebâtirent la ville, et y habitèrent.
29 Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
Et ils nommèrent cette ville-là, Dan, d'après le nom de Dan, leur père, qui était né à Israël; mais le nom de la ville était auparavant Laïs.
30 Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
Puis les enfants de Dan dressèrent pour eux l'image taillée; et Jonathan, fils de Guershon, fils de Manassé, lui et ses enfants, furent sacrificateurs pour la tribu de Dan jusqu'au jour où ils furent conduits hors du pays.
31 Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.
Ils établirent pour eux l'image taillée que Mica avait faite, pendant tout le temps que la maison de Dieu fut à Silo.

< Waamuzi 18 >