< Waamuzi 18 >

1 Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
En ces jours-là il n’y avait pas de roi en Israël; et, en ces jours, la tribu des Danites se cherchait un héritage pour y demeurer, car, jusqu’à ce jour-là, [leur lot] ne leur était point échu en héritage parmi les tribus d’Israël.
2 Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
Et les fils de Dan envoyèrent de Tsorha et d’Eshtaol cinq hommes de leur famille, pris d’entre eux tous, des hommes vaillants, pour explorer le pays et le reconnaître; et ils leur dirent: Allez, reconnaissez le pays. Et ils vinrent à la montagne d’Éphraïm, jusqu’à la maison de Michée, et ils y passèrent la nuit.
3 Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
Comme ils étaient près de la maison de Michée, ils reconnurent la voix du jeune homme, du Lévite; et ils entrèrent là, et lui dirent: Qui t’a amené ici, et que fais-tu par ici, et qu’as-tu ici?
4 Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
Et il leur dit: Michée a fait pour moi telle et telle chose, et il me donne un salaire, et je suis son sacrificateur.
5 Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
Et ils lui dirent: Nous te prions, interroge Dieu, afin que nous sachions si notre chemin par lequel nous allons prospérera.
6 Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
Et le sacrificateur leur dit: Allez en paix, le chemin où vous marchez est devant l’Éternel.
7 Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
Et les cinq hommes s’en allèrent, et vinrent à Laïs; et ils virent le peuple qui était au milieu d’elle, habitant en sécurité, à la manière des Sidoniens, tranquille et confiant; et il n’y avait dans le pays personne qui, possédant la domination, les moleste en aucune chose; et ils étaient éloignés des Sidoniens, et n’avaient commerce avec personne.
8 Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
– Et ils vinrent vers leurs frères, à Tsorha et à Eshtaol; et leurs frères leur dirent: Que [rapportez]-vous?
9 Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
Et ils dirent: Levons-nous, et montons contre eux; car nous avons vu le pays, et voici, il est très bon: et vous vous tenez tranquilles? Ne soyez pas paresseux pour aller, et entrer, et posséder le pays.
10 Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
Quand vous y entrerez, vous entrerez vers un peuple confiant, et le pays est spacieux en tout sens; car Dieu l’a livré en votre main: c’est un lieu où rien ne manque de tout ce qui est sur la terre.
11 Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
Et de là, de Tsorha et d’Eshtaol, partirent 600 hommes de la famille des Danites, ceints de [leurs] armes de guerre.
12 Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
Et ils montèrent, et campèrent à Kiriath-Jéarim, en Juda; c’est pourquoi on a appelé ce lieu-là Mahané-Dan, jusqu’à ce jour: voici, il est derrière Kiriath-Jéarim.
13 Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
Et de là ils passèrent vers la montagne d’Éphraïm, et arrivèrent jusqu’à la maison de Michée.
14 Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
Et les cinq hommes qui étaient allés pour explorer le pays de Laïs, prirent la parole et dirent à leurs frères: Savez-vous qu’il y a dans ces maisons un éphod, et des théraphim, et une image taillée, et une image de fonte? Et maintenant vous savez ce que vous avez à faire.
15 Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
Et ils se détournèrent vers ce lieu-là, et entrèrent dans la maison du jeune homme, du Lévite, la maison de Michée, et ils le saluèrent.
16 Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
Et les 600 hommes des fils de Dan, ceints de leurs armes de guerre, se tinrent à l’entrée de la porte.
17 Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
Et les cinq hommes qui étaient allés pour explorer le pays, montèrent, entrèrent là, [et] prirent l’image taillée, et l’éphod, et les théraphim, et l’image de fonte. Et le sacrificateur se tenait à l’entrée de la porte, ainsi que les 600 hommes qui étaient ceints de leurs armes de guerre.
18 Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
Et ceux-là entrèrent dans la maison de Michée, et prirent l’image taillée, et l’éphod, et les théraphim, et l’image de fonte; et le sacrificateur leur dit: Que faites-vous?
19 Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
Et ils lui dirent: Tais-toi, mets ta main sur ta bouche, et viens avec nous, et sois pour nous un père et un sacrificateur. Vaut-il mieux pour toi d’être sacrificateur de la maison d’un homme seul, ou d’être sacrificateur d’une tribu et d’une famille en Israël?
20 Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
Et le cœur du sacrificateur s’en réjouit, et il prit l’éphod, et les théraphim, et l’image taillée, et il s’en alla au milieu du peuple.
21 Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
Et ils se tournèrent, et s’en allèrent, et mirent devant eux les petits enfants, et les troupeaux, et les choses précieuses.
22 Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
Quand ils furent loin de la maison de Michée, les hommes qui étaient dans les maisons voisines de celle de Michée furent assemblés à grands cris, et ils atteignirent les fils de Dan.
23 Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
Et ils crièrent aux fils de Dan; et eux tournèrent leurs visages, et dirent à Michée: Qu’as-tu, que tu aies rassemblé [ces gens]?
24 Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
Et il dit: Vous avez pris mes dieux que j’ai faits, et le sacrificateur, et vous vous en êtes allés; et que me reste-t-il? Et comment me dites-vous: Qu’as-tu?
25 Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
Et les fils de Dan lui dirent: Ne fais pas entendre ta voix au milieu de nous, de peur que des hommes exaspérés ne se jettent sur vous, et que tu n’y perdes ta vie et la vie de ta maison.
26 Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
Et les fils de Dan s’en allèrent leur chemin; et Michée vit qu’ils étaient trop forts pour lui, et se tourna, et revint à sa maison.
27 Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
Et eux, prirent ce que Michée avait fait, et le sacrificateur qu’il avait, et vinrent à Laïs, vers un peuple tranquille et confiant, et ils les frappèrent par le tranchant de l’épée, et brûlèrent au feu leur ville.
28 Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
Et il n’y avait personne qui la délivre; car elle était loin de Sidon, et ils n’avaient commerce avec personne: elle était dans la vallée qui est vers Beth-Rehob. Et ils bâtirent la ville, et y habitèrent.
29 Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
Et ils appelèrent le nom de la ville: Dan, d’après le nom de Dan, leur père, qui était né à Israël; mais, au commencement, le nom de la ville était Laïs.
30 Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
Et les fils de Dan dressèrent pour eux l’image taillée; et Jonathan, fils de Guershom, fils de Moïse, lui et ses fils, furent sacrificateurs pour la tribu des Danites, jusqu’au jour de la captivité du pays.
31 Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.
Et ils dressèrent pour eux l’image taillée de Michée, qu’il avait faite, pendant tout le temps que la maison de Dieu fut à Silo.

< Waamuzi 18 >