< Waamuzi 17 >
1 Palikuwa na mtu aliyeitwa Mika ambaye aliishi katika vilima vya Efraimu.
Il y avait un homme de la montagne d'Éphraïm, dont le nom était Mica.
2 Akamwambia mama yake, “Zile shekeli 1,100 za fedha zilizochukuliwa kwako, ambazo nilisikia ukizinenea maneno ya laana, hizi hapa; mimi ndiye niliyezichukua, lakini sasa ninakurudishia.” Ndipo mama yake akamwambia, “Bwana na akubariki, mwanangu.”
Il dit à sa mère: Les onze cents pièces d'argent qui te furent prises, et pour lesquelles tu fis des imprécations, même à mes oreilles, voici, cet argent est entre mes mains; c'est moi qui l'avais pris. Alors sa mère dit: Que mon fils soit béni par l'Éternel!
3 Alipozirudisha zile shekeli 1,100 za fedha kwa mama yake, mama yake akamwambia, “Mimi nimeiweka fedha hii wakfu kwa Bwana kwa ajili ya mwanangu kutengenezea kinyago cha kuchonga na sanamu ya kusubu. Mimi nitakurudishia wewe.”
Et il rendit à sa mère les onze cents pièces d'argent. Sa mère dit: Je consacre de ma main cet argent à l'Éternel pour mon fils, afin d'en faire une image taillée et une image de fonte; et maintenant, je te le rends.
4 Hivyo akamrudishia mama yake ile fedha, naye mama yake akachukua shekeli mia mbili za hiyo fedha na kumpa mfua fedha, ambaye aliifanyiza kinyago na sanamu. Navyo vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika.
Il rendit l'argent à sa mère; et elle en prit deux cents pièces, et les donna au fondeur, qui en fit une image taillée et une image de fonte; et elles furent dans la maison de Mica.
5 Basi Mika alikuwa na mahali pa kuabudia miungu, akatengeneza naivera, pamoja na vinyago, na kumweka mmoja wa wanawe kuwa kuhani wake.
Ainsi ce Mica eut une maison de dieux; il fit un éphod et des théraphim, et consacra l'un de ses fils, qui lui servit de sacrificateur.
6 Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme, kila mmoja akafanya kama alivyoona vyema machoni pake mwenyewe.
En ce temps-là il n'y avait point de roi en Israël, chacun faisait ce qui lui semblait bon.
7 Basi palikuwa na kijana mmoja wa Bethlehemu ya Yuda. Yeye alikuwa Mlawi aliyeishi miongoni mwa kabila la Yuda.
Or, il y avait un jeune homme de Bethléhem de Juda, de la famille de Juda, qui était Lévite, et il séjournait là.
8 Huyu kijana akatoka katika mji huo wa Bethlehemu ya Yuda na kutafuta mahali pengine ambapo angeweza kuishi. Alipokuwa akisafiri, akafika nyumbani kwa Mika katika vilima vya Efraimu.
Cet homme partit de la ville de Bethléhem de Juda, pour aller demeurer où il trouverait son avantage. Et il vint, en poursuivant son chemin, à la montagne d'Éphraïm, jusqu'à la maison de Mica.
9 Mika akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu ya Yuda, ninatafuta mahali pa kuishi.”
Et Mica lui dit: D'où viens-tu? Le Lévite lui répondit: Je suis de Bethléhem de Juda, et je cherche une demeure où je trouverai mon avantage.
10 Ndipo Mika akamwambia, “Ishi pamoja nami, uwe baba yangu na kuhani wangu, nami nitakupa shekeli kumi za fedha, nguo na chakula.”
Et Mica lui dit: Demeure avec moi, et sers-moi de père et de sacrificateur; et je te donnerai dix pièces d'argent par an, un habillement complet et ta nourriture. Et le Lévite y alla.
11 Hivyo yule Mlawi akakubali kuishi pamoja naye, naye huyo kijana akawa kwake kama mmoja wa wanawe.
Ainsi le Lévite se décida à demeurer avec cet homme, et ce jeune homme fut pour lui comme l'un de ses fils.
12 Hivyo Mika akamweka wakfu huyo kijana Mlawi, naye huyo akawa kuhani wake na kuishi nyumbani mwake.
Et Mica consacra le Lévite, et le jeune homme lui servit de sacrificateur, et demeura dans sa maison.
13 Ndipo Mika akasema, “Sasa najua Bwana atanitendea mema, kwa kuwa Mlawi huyu amekuwa kuhani wangu.”
Alors Mica dit: Maintenant je sais que l'Éternel me fera du bien, parce que j'ai ce Lévite pour sacrificateur.