< Waamuzi 17 >

1 Palikuwa na mtu aliyeitwa Mika ambaye aliishi katika vilima vya Efraimu.
There was a man in the hill country of Ephraim, and his name was Micah.
2 Akamwambia mama yake, “Zile shekeli 1,100 za fedha zilizochukuliwa kwako, ambazo nilisikia ukizinenea maneno ya laana, hizi hapa; mimi ndiye niliyezichukua, lakini sasa ninakurudishia.” Ndipo mama yake akamwambia, “Bwana na akubariki, mwanangu.”
He said to his mother, “The 1,100 pieces of silver that were taken from you, about which you spoke a curse, and which I heard—look here! I have the silver with me. I stole it.” His mother said, “May Yahweh bless you, my son!”
3 Alipozirudisha zile shekeli 1,100 za fedha kwa mama yake, mama yake akamwambia, “Mimi nimeiweka fedha hii wakfu kwa Bwana kwa ajili ya mwanangu kutengenezea kinyago cha kuchonga na sanamu ya kusubu. Mimi nitakurudishia wewe.”
He restored the 1,100 pieces of silver to his mother and his mother said, “I set apart this silver to Yahweh, for my son to make carved and cast metal figures. So now, I restore it to you.”
4 Hivyo akamrudishia mama yake ile fedha, naye mama yake akachukua shekeli mia mbili za hiyo fedha na kumpa mfua fedha, ambaye aliifanyiza kinyago na sanamu. Navyo vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika.
When he restored the money to his mother, his mother took two hundred pieces of silver and gave them to a metal worker who made them into carved and cast metal figures, and they were placed in the house of Micah.
5 Basi Mika alikuwa na mahali pa kuabudia miungu, akatengeneza naivera, pamoja na vinyago, na kumweka mmoja wa wanawe kuwa kuhani wake.
The man Micah had a house of idols and he made an ephod and household gods, and he hired one of his sons to become his priest.
6 Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme, kila mmoja akafanya kama alivyoona vyema machoni pake mwenyewe.
In those days there was no king in Israel, and everyone did what was right in his own eyes.
7 Basi palikuwa na kijana mmoja wa Bethlehemu ya Yuda. Yeye alikuwa Mlawi aliyeishi miongoni mwa kabila la Yuda.
Now there was a young man of Bethlehem in Judah, of the clan of Judah, who was a Levite. He stayed there to fulfill his duties.
8 Huyu kijana akatoka katika mji huo wa Bethlehemu ya Yuda na kutafuta mahali pengine ambapo angeweza kuishi. Alipokuwa akisafiri, akafika nyumbani kwa Mika katika vilima vya Efraimu.
The man left Bethlehem in Judah to go and find a place to live. As he journeyed, he came to Micah's house in the hill country of Ephraim.
9 Mika akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu ya Yuda, ninatafuta mahali pa kuishi.”
Micah said to him, “Where do you come from?” The man said to him, “I am a Levite of Bethlehem in Judah, and I am traveling to find a place where I might live.”
10 Ndipo Mika akamwambia, “Ishi pamoja nami, uwe baba yangu na kuhani wangu, nami nitakupa shekeli kumi za fedha, nguo na chakula.”
Micah said to him, “Stay with me, and be to me a father and a priest. I will give you ten pieces of silver a year, a suit of clothes, and your food.” So the Levite went into his house.
11 Hivyo yule Mlawi akakubali kuishi pamoja naye, naye huyo kijana akawa kwake kama mmoja wa wanawe.
The Levite was content to live with the man, and the young man became to Micah like one of his sons.
12 Hivyo Mika akamweka wakfu huyo kijana Mlawi, naye huyo akawa kuhani wake na kuishi nyumbani mwake.
Micah set apart the Levite for sacred duties, and the young man became his priest, and was in Micah's house.
13 Ndipo Mika akasema, “Sasa najua Bwana atanitendea mema, kwa kuwa Mlawi huyu amekuwa kuhani wangu.”
Then Micah said, “Now I know that Yahweh will do good for me, because this Levite has become my priest.”

< Waamuzi 17 >