< Waamuzi 17 >

1 Palikuwa na mtu aliyeitwa Mika ambaye aliishi katika vilima vya Efraimu.
And there is a man of the hill-country of Ephraim, and his name [is] Micah,
2 Akamwambia mama yake, “Zile shekeli 1,100 za fedha zilizochukuliwa kwako, ambazo nilisikia ukizinenea maneno ya laana, hizi hapa; mimi ndiye niliyezichukua, lakini sasa ninakurudishia.” Ndipo mama yake akamwambia, “Bwana na akubariki, mwanangu.”
and he says to his mother, “The eleven hundred pieces of silver which have been taken of yours, and [of which] you have sworn, and also spoken in my ears; behold, the silver [is] with me, I have taken it”; and his mother says, “Blessed [is] my son of YHWH.”
3 Alipozirudisha zile shekeli 1,100 za fedha kwa mama yake, mama yake akamwambia, “Mimi nimeiweka fedha hii wakfu kwa Bwana kwa ajili ya mwanangu kutengenezea kinyago cha kuchonga na sanamu ya kusubu. Mimi nitakurudishia wewe.”
And he gives back the eleven hundred pieces of silver to his mother, and his mother says, “I had certainly sanctified the silver to YHWH, from my hand, for my son, to make a carved image, and a molten image; and now, I give it back to you.”
4 Hivyo akamrudishia mama yake ile fedha, naye mama yake akachukua shekeli mia mbili za hiyo fedha na kumpa mfua fedha, ambaye aliifanyiza kinyago na sanamu. Navyo vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika.
And he gives back the money to his mother, and his mother takes two hundred pieces of silver, and gives them to a refiner, and he makes them a carved image, and a molten image, and it is in the house of Micah.
5 Basi Mika alikuwa na mahali pa kuabudia miungu, akatengeneza naivera, pamoja na vinyago, na kumweka mmoja wa wanawe kuwa kuhani wake.
As for the man Micah, he has a house of gods, and he makes an ephod, and teraphim, and consecrates the hand of one of his sons, and he is for a priest to him;
6 Katika siku hizo Israeli hawakuwa na mfalme, kila mmoja akafanya kama alivyoona vyema machoni pake mwenyewe.
in those days there is no king in Israel, each does that which is right in his own eyes.
7 Basi palikuwa na kijana mmoja wa Bethlehemu ya Yuda. Yeye alikuwa Mlawi aliyeishi miongoni mwa kabila la Yuda.
And there is a young man of Beth-Lehem-Judah, of the family of Judah, and he [is] a Levite, and he [is] a sojourner there.
8 Huyu kijana akatoka katika mji huo wa Bethlehemu ya Yuda na kutafuta mahali pengine ambapo angeweza kuishi. Alipokuwa akisafiri, akafika nyumbani kwa Mika katika vilima vya Efraimu.
And the man goes out of the city, out of Beth-Lehem-Judah, to sojourn where he finds, and comes to the hill-country of Ephraim, to the house of Micah, to work his way.
9 Mika akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Mimi ni Mlawi kutoka Bethlehemu ya Yuda, ninatafuta mahali pa kuishi.”
And Micah says to him, “Where do you come from?” And he says to him, “I [am] a Levite of Beth-Lehem-Judah, and I am going to sojourn where I find.”
10 Ndipo Mika akamwambia, “Ishi pamoja nami, uwe baba yangu na kuhani wangu, nami nitakupa shekeli kumi za fedha, nguo na chakula.”
And Micah says to him, “Dwell with me, and be for a father and for a priest to me, and I give ten pieces of silver to you for the days, and a suit of garments, and your sustenance”; and the Levite goes [in].
11 Hivyo yule Mlawi akakubali kuishi pamoja naye, naye huyo kijana akawa kwake kama mmoja wa wanawe.
And the Levite is willing to dwell with the man, and the young man is to him as one of his sons.
12 Hivyo Mika akamweka wakfu huyo kijana Mlawi, naye huyo akawa kuhani wake na kuishi nyumbani mwake.
And Micah consecrates the hand of the Levite, and the young man is for a priest to him, and he is in the house of Micah,
13 Ndipo Mika akasema, “Sasa najua Bwana atanitendea mema, kwa kuwa Mlawi huyu amekuwa kuhani wangu.”
and Micah says, “Now I have known that YHWH does good to me, for the Levite has been for a priest to me.”

< Waamuzi 17 >