< Waamuzi 16 >

1 Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
Samson alla à Gaza; il y vit une courtisane, et il entra chez elle.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
On l'annonça aux gens de Gaza, en disant: " Samson est venu ici. " Et ils l'environnèrent et se tinrent en embuscade toute la nuit à la porte de la ville. Ils se tinrent tranquilles toute la nuit, en disant: " Attendons jusqu'à ce que luise le matin, et nous le tuerons. "
3 Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
Samson demeura couché jusqu'à minuit; à minuit, il se leva et, saisissant les battants de la porte de la ville et les deux poteaux, il les arracha avec la barre, les mit sur ses épaules et les porta sur le sommet de la montagne qui regarde Hébron.
4 Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
Après cela, il aima une femme dans la vallée de Sorec; elle se nommait Dalila.
5 Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
Les princes des philistins montèrent vers elle et lui dirent: " Flatte-le et vois où gît sa grande force, et comment nous pourrons nous rendre maîtres de lui, afin de le lier et de le dompter, et nous te donnerons chacun mille et cent sicles d'argent. "
6 Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
Dalila dit à Samson: " Dis-moi, je te prie, ou gît ta grande force, et avec quoi il faudrait te lier pour te dompter? "
7 Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
Samson lui dit: " Si l'on me liait avec sept cordes fraîches, qui ne seraient pas encore sèches, je deviendrais faible et je serais comme un autre homme. "
8 Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
Les princes des Philistins apportèrent à Dalila sept cordes fraîches, qui n'étaient pas encore sèches; et elle le lia avec ces cordes.
9 Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
— Or elle avait des gens en embuscade dans la chambre. — Elle lui dit: " Les Philistins sont sur toi, Samson! " Et il rompit les cordes, comme se rompt un cordon d'étoupe quand il sent le feu; et l'on ne connut pas le secret de sa force.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
Dalila dit à Samson: " Voici, tu t'es joué de moi et tu m'as dit des mensonges. Maintenant, je te prie, indique-moi avec quoi il faut te lier. "
11 Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
Il lui dit: " Si on me liait avec des cordes neuves, n'ayant servi à aucun usage, je deviendrais faible et je serais comme un autre homme. "
12 Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
Dalila prit des cordes neuves, avec lesquelles elle le lia. Et elle lui dit: " Les Philistins sont sur toi, Samson! " — Or des gens se tenaient en embuscade dans la chambre. — Et il rompit comme un fil les cordes qu'il avait aux bras.
13 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
Dalila dit à Samson: " Jusqu'à présent tu t'es joué de moi, et tu m'as dit des mensonges. Indique-moi avec quoi il faut te lier. " Il lui dit: " Tu n'as qu'à tisser les sept tresses de ma tête avec le tissu. "
14 na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
Et elle les fixa avec la cheville. Puis elle lui dit: " Les Philistins sont sur toi, Samson! " Et, se réveillant de son sommeil, il arracha la cheville du métier et le tissu.
15 Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
Elle lui dit: " Comment peux-tu dire: je t'aime! puisque ton cœur n'est pas avec moi? Voilà trois fois que tu t'es joué de moi, et que tu ne m'as pas indiqué où gît ta grande force. "
16 Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
Elle le tourmentait ainsi chaque jour et le fatiguait de ses instances; à la fin, son âme s'impatienta jusqu'à en mourir;
17 Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
il lui ouvrit tout son cœur et lui dit: " Le rasoir n'a jamais passé sur ma tête, car je suis nazaréen de Dieu dès le sein de ma mère. Si j'étais rasé, ma force m'abandonnerait, je deviendrais faible et je serais comme tous les autres hommes. "
18 Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
Dalila vit qu'il lui avait ouvert tout son cœur; elle envoya appeler les princes des Philistins et leur fit dire: " Montez cette fois, car il m'a ouvert tout son cœur. " Et les princes des Philistins montèrent vers elle. apportant l'argent dans leurs mains.
19 Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
Elle l'endormit sur ses genoux et, ayant appelé l'homme, elle fit raser les sept tresses de la tête de Samson et commença à le dompter, et sa force se retira de lui.
20 Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
Elle dit alors: " Les Philistins sont sur toi, Samson! " Il se réveilla de son sommeil et dit: " Je me tirerai d'affaire comme les autres fois, et je me dégagerai; " car il ne savait pas que Yahweh s'était retiré de lui.
21 Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
Les Philistins le saisirent et lui crevèrent les yeux et, l'ayant fait descendre à Gaza, ils le lièrent d'une double chaîne d'airain. Il tournait la meule dans la prison.
22 Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
Cependant les cheveux de sa tête commençaient à repousser depuis qu'il avait été rasé.
23 Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
Les princes des Philistins s'assemblèrent pour offrir un grand sacrifice à Dagon, leur dieu, et pour se réjouir. Ils disaient: " Notre dieu a livré entre nos mains Samson, notre ennemi. "
24 Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
Le peuple le vit, et ils louèrent leur dieu, car ils disaient: " Notre dieu a livré entre nos mains notre ennemi, celui qui ravageait notre pays, et qui nous tuait tant de gens. "
25 Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
Quand leurs cœurs furent devenus joyeux, ils dirent: " Qu'on fasse venir Samson, et qu'il nous divertisse! " Ils tirèrent Samson de la prison, et il dansa devant eux. On l'avait placé entre les colonnes.
26 Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
Samson dit au jeune homme qui le tenait par la main: " Laisse-moi toucher les colonnes sur lesquelles se tient la maison et m'y appuyer.
27 Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
Or la maison était remplie d'hommes et de femmes; tous les princes des Philistins étaient là, et il y avait sur le toit environ trois mille personnes, hommes et femmes, qui regardaient Samson danser.
28 Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
Alors Samson invoqua Yahweh et dit: " Seigneur Yahweh, souvenez-vous de moi, je vous prie, et donnez-moi de la force cette fois seulement, ô Dieu. afin que d'un seul coup je me venge des Philistins pour mes deux yeux. "
29 Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
Et Samson, embrassant les deux colonnes du milieu sur lesquelles se tenait la maison, s'appuya sur elles, sur l'une de la main droite, sur l'autre de la main gauche.
30 Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
Et Samson dit: " Que je meure avec les Philistins! ". Et il se pencha avec force, et la maison s'écroula sur les princes et sur tout le peuple qui s'y trouvait. Ceux qu'il fit périr en mourant furent plus nombreux que ceux qu'il avait tués pendant sa vie.
31 Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
Ses frères et toute la maison de son père descendirent à Gaza et l'emportèrent. Lorsqu'ils furent remontés, ils l'enterrèrent entre Saraa et Esthaol, dans le sépulcre de Manué, son père. Il avait jugé Israël pendant vingt ans.

< Waamuzi 16 >