< Waamuzi 16 >
1 Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake.
He also went into Gaza. And there he saw a harlot woman, and he entered to her.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”
And when the Philistines had heard of this, and it had become well known among them, that Samson had entered the city, they surrounded him, placing guards at the gate of the city. And there they were keeping watch all night in silence, so that, in the morning, they might kill him as he was going out.
3 Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.
But Samson slept until the middle of the night, and rising up from there, he took both doors from the gate, with their posts and bars. And laying them upon his shoulders, he carried them to the top of the hill that looks toward Hebron.
4 Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila.
After these things, he loved a woman who was living in the valley of Sorek. And she was called Delilah.
5 Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”
And the leaders of the Philistines went to her, and they said: “Deceive him, and learn from him wherein lies his great strength, and how we may be able to overcome him and to impose restraints on him. And if you will do this, each one of us will give you one thousand one hundred silver coins.”
6 Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”
Therefore, Delilah said to Samson, “Tell me, I beg you, wherein lies your very great strength, and with what might you be bound, so that you could not break free?”
7 Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
And Samson answered her, “If I will be bound with seven cords, made of sinews not yet dry, but still damp, I will be weak like other men.”
8 Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni.
And the princes of the Philistines brought to her seven cords, such as he had described. And she bound him with these.
9 Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.
And so, those hiding in ambush with her, in the bedroom, were expecting the end of the matter. And she cried out to him, “The Philistines are upon you, Samson!” And he broke the cords, as one would break a thread of flax, twisted for cutting and singed by fire. And so it was not known wherein lay his strength.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”
And Delilah said to him: “Behold, you have mocked me, and you have spoken a falsehood. But at least now, tell me with what you may be bound.”
11 Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”
And he answered her, “If I will be bound with new cords, which have never been used, I will be weak and like other men.”
12 Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.
Again, Delilah tied him with these, and she cried out, “The Philistines are upon you, Samson!” For an ambush had been prepared in the bedroom. But he broke the bindings like the filaments of a web.
13 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo,
And Delilah spoke to him again: “How long will you deceive me and tell me falsehoods? Reveal with what you ought to be bound.” And Samson responded to her, “If you weave the seven locks of my head with a loom, and if you tie these around a spike and fix it to the ground, I will be weak.”
14 na kuvikaza kwa msumari. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.
And when Delilah had done this, she said to him, “The Philistines are upon you, Samson.” And arising from sleep, he withdrew the spike with the hairs and the weaving.
15 Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.”
And Delilah said to him: “How can you say that you love me, when your soul is not with me? You have lied to me on three occasions, and you are not willing to reveal wherein lies your very great strength.”
16 Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.
And when she had been very troublesome to him, and over many days had continually stayed nearby, giving him no time to rest, his soul was faint, and he was weary, even unto death.
17 Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”
Then disclosing the truth of the matter, he said to her: “Iron has never been drawn across my head, for I am a Nazirite, that is, I have been consecrated to God from my mother’s womb. If my head will be shaven, my strength will depart from me, and I will be faint and will be like other men.”
18 Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao.
Then, seeing that he had confessed to her his whole soul, she sent to the leaders of the Philistines and ordered: “Come up just once more. For now he has opened his heart to me.” And they went up, taking with them the money that they had promised.
19 Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.
But she made him sleep upon her knees, and recline his head upon her bosom. And she called a barber, and he shaved his seven locks of hair. And she began to push him away, and to repel him from herself. For immediately his strength departed from him.
20 Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!” Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.
And she said, “The Philistines are upon you, Samson!” And awaking from sleep, he said in his mind, “I will break away and shake myself free, just as I did before.” For he did not know that the Lord had withdrawn from him.
21 Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani.
And when the Philistines had seized him, they immediately plucked out his eyes. And they led him, bound in chains, to Gaza. And enclosing him in a prison, they made him work a millstone.
22 Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.
And now his hair began to grow back.
23 Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”
And the leaders of the Philistines convened as one, so that they might offer great sacrifices to Dagon, their god. And they feasted, saying, “Our god has delivered our enemy, Samson, into our hands.”
24 Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema: “Sasa mungu wetu amemtia adui yetu mikononi mwetu, yule aliyeharibu nchi yetu na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”
Then, too, the people, seeing this, praised their god, and they said the same, “Our god has delivered our adversary into our hands: the one who destroyed our land and who killed very many.”
25 Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao. Wakamweka kati ya nguzo mbili.
And rejoicing in their celebration, having now taken food, they instructed that Samson be called, and that he be mocked before them. And having been brought from prison, he was mocked before them. And they caused him to stand between two pillars.
26 Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.”
And he said to the boy who was guiding his steps, “Permit me to touch the pillars, which support the entire house, and to lean against them, so that I may rest a little.”
27 Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza.
Now the house was full of men and women. And all the leaders of the Philistines were there, as well as about three thousand persons, of both sexes, on the roof and in the upper level of the house, who were watching Samson being mocked.
28 Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.”
Then, calling upon the Lord, he said, “O Lord God remember me, and restore to me now my former strength, O my God, so that I may avenge myself against my enemies, and so that I may receive one vengeance for the deprivation of my two eyes.”
29 Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto.
And taking hold of both the pillars, on which the house rested, and holding one with his right hand and the other with his left,
30 Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.
he said, “May my life die with the Philistines.” And when he had shaken the pillars strongly, the house fell upon all the leaders, and the rest of the multitude who were there. And he killed many more in his death than he had killed before in his life.
31 Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
Then his brothers and all his relatives, going down, took his body, and they buried it between Zorah and Eshtaol, in the burying place of his father, Manoah. And he judged Israel for twenty years.