< Waamuzi 15 >

1 Baada ya kitambo kidogo, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mwana-mbuzi, kwenda kumzuru mkewe. Akasema, “Nataka kuingia chumbani kwa mke wangu.” Lakini baba yake huyo mwanamke hakumruhusu kuingia.
Quelque temps après, à l'époque de la moisson des blés, Samson alla voir sa femme, en apportant un chevreau. Il dit: " Je veux entrer auprès de ma femme dans sa chambre. " Mais son père ne lui accorda pas l'entrée;
2 Huyo baba mkwe wake akamwambia, “Nilikuwa na hakika kwamba ulimkataa, hivyo mimi nikampa rafiki yako. Je, mdogo wake wa kike si mzuri zaidi kuliko yeye? Mchukue huyo badala yake.”
et son père dit: " J'ai pensé que tu avais pour elle de la haine, et je l'ai donnée à ton ami. Est-ce que sa jeune sœur n'est pas plus belle qu'elle? Qu'elle soit ta femme à sa place. "
3 Samsoni akawaambia, “Wakati huu, nitakapowadhuru Wafilisti, sitakuwa na lawama.”
Samson leur dit: " Cette fois je serai innocent envers les Philistins, si je leur fais du mal. "
4 Hivyo Samsoni akatoka akawakamata mbweha 300 na kuwafunga wawili wawili kwa mikia yao kila mmoja kwa mwingine. Kisha akafungia mwenge wa moto, kwenye mikia ya kila jozi moja ya mbweha aliyokuwa ameifunga,
Et Samson s'en alla. Il attrapa trois cents renards et, ayant pris des torches, il tourna les renards queue contre queue, et mit une torche entre les deux queues, au milieu.
5 akawasha ile mienge na kuwaachia wale mbweha katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka zilizosimamishwa katika matita. Akateketeza matita ya nafaka zilizosimama, pamoja na mashamba ya mizabibu na viunga vya mizeituni.
Il alluma ensuite les torches et lâcha les renards dans les moissons des Philistins; il embrasa depuis les tas de gerbes jusqu'aux blés sur pied et aux plantations d'oliviers.
6 Ndipo Wafilisti wakauliza, “Ni nani aliyetenda jambo hili?” Wakaambiwa, “Ni Samsoni, yule mkwewe Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake.” Hivyo Wafilisti wakapanda wakamteketeza kwa moto yeye huyo mwanamke pamoja na baba yake.
Les Philistins dirent: " Qui a fait cela? " On répondit: " C'est Samson, le gendre du Thamnéen, parce que celui-ci lui a pris sa femme et l'a donnée à son ami. " Et les Philistins étant montés, ils la brûlèrent, elle et son père.
7 Samsoni akawaambia, “Kwa kuwa mmetenda hivyo, hakika sitatulia mpaka niwe nimelipiza kisasi juu yenu.”
Samson leur dit: " C'est ainsi que vous agissez! Eh bien, je ne cesserai qu'après m'être vengé de vous. "
8 Akawashambulia kwa ukali kwa mapigo makuu na kuwaua watu wengi sana. Kisha akateremka na kukaa katika ufa kwenye mwamba wa Etamu.
Et il les battit rudement, cuisse et hanche; il descendit ensuite et demeura dans la caverne du rocher d'Etam.
9 Wafilisti wakapanda na kupiga kambi huko Yuda na kuenea huko Lehi.
Alors les Philistins montèrent et campèrent en Juda, se répandant en Léchi.
10 Watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kupigana nasi?” Wakawajibu, “Tumekuja ili kumkamata Samsoni na kumtenda kama alivyotutendea.”
Les hommes de Juda dirent: " Pourquoi êtes-vous tournés contre nous? " Ils répondirent: " Nous sommes montés pour lier Samson, afin de le traiter comme il nous a traités. "
11 Ndipo watu 3,000 toka Yuda walipoteremka na kwenda kwenye ufa wa mwamba huko Etamu, na kumwambia Samsoni, “Je, hujatambua kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hiki ulichotutendea?” Akawajibu, “Mimi nimewatendea tu kile walichonitendea.”
Trois mille hommes de Juda descendirent à la caverne du rocher d'Etam, et dirent à Samson: " Ne sais-tu pas que les Philistins sont nos maîtres? Qu'est-ce que tu nous as fait là? " Il leur répondit: " Je les ai traités comme ils m'ont traité. "
12 Wakamwambia, “Tumekuja kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kuwa hamtaniua ninyi wenyewe.”
Ils lui dirent: " Nous sommes descendus pour te lier, afin de te livrer entre les mains des Philistins. " Samson leur dit: " Jurez-moi que vous ne voulez pas me tuer. "
13 Wakamjibu, “Sisi hatutakuua, bali tutakufunga tu na kukutia mikononi mwao.” Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya. Wakamchukua toka huko kwenye ufa katika mwamba.
Ils lui répondirent en disant: " Non; nous voulons seulement te lier et te livrer entre leurs mains, mais nous ne te ferons pas mourir. " Et l'ayant lié de deux cordes neuves, ils le firent monter du rocher.
14 Alipokaribia Lehi, Wafilisti wakamjia wakipiga kelele. Roho wa Bwana akamjia juu yake kwa nguvu. Kamba zilizomfunga mikono yake zikawa kama kitani iliyochomwa kwa moto, na vifungo vyake vikaanguka chini toka mikononi mwake.
Lorsqu'il arriva à Léchi, les Philistins poussèrent à sa rencontre des cris de joie. Alors l'Esprit de Yahweh le saisit, et les cordes qu'il avait aux bras devinrent comme des fils de lin brûlés par le feu, et ses liens tombèrent de ses mains.
15 Ndipo akaona mfupa mpya wa taya la punda, akanyoosha mkono, akauchukua na kuua nao Wafilisti wapatao 1,000.
Trouvant une mâchoire d'âne fraîche, il étendit la main, la saisit et en frappa mille hommes.
16 Ndipo Samsoni akasema, “Kwa taya la punda malundo juu ya malundo. Kwa taya la punda nimeua watu 1,000.”
Et Samson dit: " Avec une mâchoire d'âne, je les ai bien asinés (rossés), avec une mâchoire d'âne, j'ai frappé mille hommes. "
17 Alipomaliza kusema, akautupa ule mfupa wa taya; na mahali pale pakaitwa Ramath-Lehi.
Quand il eut achevé de parler, il jeta de sa main la mâchoire, et nomma ce lieu Ramath-Léchi.
18 Kwa kuwa alikuwa amesikia kiu sana, akamlilia Bwana akisema, “Umempa mtumishi wako ushindi huu mkuu. Je, sasa nife kwa kiu na kuangukia mikononi mwa hawa watu wasiotahiriwa?”
Dévoré par la soif, il invoqua Yahweh, et dit: " C'est vous qui avez accordé par la main de votre serviteur cette grande délivrance; et maintenant, faut-il que je meure de soif et que je tombe entre les mains des incirconcis? "
19 Bwana akafunua shimo huko Lehi, pakatoka maji. Samsoni alipoyanywa, nguvu zikamrudia na kuhuika. Hivyo chemchemi ile ikaitwa En-Hakore, nayo iko mpaka leo huko Lehi.
Et Dieu fendit le rocher creux qui est à Léchi, et il en sortit de l'eau. Samson but, son esprit se ranima et il reprit vie. C'est pourquoi on a appelé cette source En-Hakkoré; elle existe à Léchi, jusqu'à ce jour.
20 Samsoni akawa mwamuzi wa Waisraeli katika siku za Wafilisti kwa muda wa miaka ishirini.
Samson jugea Israël, au temps des Philistins, pendant vingt ans.

< Waamuzi 15 >