< Waamuzi 15 >

1 Baada ya kitambo kidogo, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mwana-mbuzi, kwenda kumzuru mkewe. Akasema, “Nataka kuingia chumbani kwa mke wangu.” Lakini baba yake huyo mwanamke hakumruhusu kuingia.
And it cometh to pass, after [some] days, in the days of wheat-harvest, that Samson looketh after his wife, with a kid of the goats, and saith, 'I go in unto my wife, to the inner chamber;' and her father hath not permitted him to go in,
2 Huyo baba mkwe wake akamwambia, “Nilikuwa na hakika kwamba ulimkataa, hivyo mimi nikampa rafiki yako. Je, mdogo wake wa kike si mzuri zaidi kuliko yeye? Mchukue huyo badala yake.”
and her father saith, I certainly said, that thou didst certainly hate her, and I give her to thy companion; is not her sister — the young one — better than she? Let her be, I pray thee, to thee, instead of her.'
3 Samsoni akawaambia, “Wakati huu, nitakapowadhuru Wafilisti, sitakuwa na lawama.”
And Samson saith of them, 'I am more innocent this time than the Philistines, though I am doing with them evil.'
4 Hivyo Samsoni akatoka akawakamata mbweha 300 na kuwafunga wawili wawili kwa mikia yao kila mmoja kwa mwingine. Kisha akafungia mwenge wa moto, kwenye mikia ya kila jozi moja ya mbweha aliyokuwa ameifunga,
And Samson goeth and catcheth three hundred foxes, and taketh torches, and turneth tail unto tail, and putteth a torch between the two tails, in the midst,
5 akawasha ile mienge na kuwaachia wale mbweha katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka zilizosimamishwa katika matita. Akateketeza matita ya nafaka zilizosimama, pamoja na mashamba ya mizabibu na viunga vya mizeituni.
and kindleth fire in the torches, and sendeth [them] out into the standing corn of the Philistines, and burneth [it] from heap even unto standing corn, even unto vineyard — olive-yard.
6 Ndipo Wafilisti wakauliza, “Ni nani aliyetenda jambo hili?” Wakaambiwa, “Ni Samsoni, yule mkwewe Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake.” Hivyo Wafilisti wakapanda wakamteketeza kwa moto yeye huyo mwanamke pamoja na baba yake.
And the Philistines say, 'Who hath done this?' And they say, 'Samson, son-in-law of the Timnite, because he hath taken away his wife, and giveth her to his companion;' and the Philistines go up, and burn her and her father with fire.
7 Samsoni akawaambia, “Kwa kuwa mmetenda hivyo, hakika sitatulia mpaka niwe nimelipiza kisasi juu yenu.”
And Samson saith to them, 'Though ye do thus, nevertheless I am avenged on you, and afterwards I cease!'
8 Akawashambulia kwa ukali kwa mapigo makuu na kuwaua watu wengi sana. Kisha akateremka na kukaa katika ufa kwenye mwamba wa Etamu.
And he smiteth them hip and thigh — a great smiting, and goeth down and dwelleth in the cleft of the rock Etam.
9 Wafilisti wakapanda na kupiga kambi huko Yuda na kuenea huko Lehi.
And the Philistines go up, and encamp in Judah, and are spread out in Lehi,
10 Watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kupigana nasi?” Wakawajibu, “Tumekuja ili kumkamata Samsoni na kumtenda kama alivyotutendea.”
and the men of Judah say, 'Why have ye come up against us?' and they say, 'To bind Samson we have come up, to do to him as he hath done to us.'
11 Ndipo watu 3,000 toka Yuda walipoteremka na kwenda kwenye ufa wa mwamba huko Etamu, na kumwambia Samsoni, “Je, hujatambua kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hiki ulichotutendea?” Akawajibu, “Mimi nimewatendea tu kile walichonitendea.”
And three thousand men of Judah go down unto the cleft of the rock Etam, and say to Samson, 'Hast thou now known that the Philistines are rulers over us? and what [is] this thou hast done to us?' And he saith to them, 'As they did to me, so I did to them.'
12 Wakamwambia, “Tumekuja kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kuwa hamtaniua ninyi wenyewe.”
And they say to him, 'To bind thee we have come down — to give thee into the hand of the Philistines.' And Samson saith to them, 'Swear to me, lest ye fall upon me yourselves.'
13 Wakamjibu, “Sisi hatutakuua, bali tutakufunga tu na kukutia mikononi mwao.” Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya. Wakamchukua toka huko kwenye ufa katika mwamba.
And they speak to him, saying, No, but we certainly bind thee, and have given thee into their hand, and we certainly do not put thee to death;' and they bind him with two thick bands, new ones, and bring him up from the rock.
14 Alipokaribia Lehi, Wafilisti wakamjia wakipiga kelele. Roho wa Bwana akamjia juu yake kwa nguvu. Kamba zilizomfunga mikono yake zikawa kama kitani iliyochomwa kwa moto, na vifungo vyake vikaanguka chini toka mikononi mwake.
He hath come unto Lehi — and the Philistines have shouted at meeting him — and the Spirit of Jehovah prospereth over him, and the thick bands which [are] on his arms are as flax which they burn with fire, and his bands are wasted from off his hands,
15 Ndipo akaona mfupa mpya wa taya la punda, akanyoosha mkono, akauchukua na kuua nao Wafilisti wapatao 1,000.
and he findeth a fresh jaw-bone of an ass, and putteth forth his hand and taketh it, and smiteth with it — a thousand men.
16 Ndipo Samsoni akasema, “Kwa taya la punda malundo juu ya malundo. Kwa taya la punda nimeua watu 1,000.”
And Samson saith, 'With a jaw-bone of the ass — an ass upon asses — with a jaw-bone of the ass I have smitten a thousand men.'
17 Alipomaliza kusema, akautupa ule mfupa wa taya; na mahali pale pakaitwa Ramath-Lehi.
And it cometh to pass when he finisheth speaking, that he casteth away the jaw-bone out of his hand, and calleth that place Ramath-Lehi;
18 Kwa kuwa alikuwa amesikia kiu sana, akamlilia Bwana akisema, “Umempa mtumishi wako ushindi huu mkuu. Je, sasa nife kwa kiu na kuangukia mikononi mwa hawa watu wasiotahiriwa?”
and he thirsteth exceedingly, and calleth unto Jehovah, and saith, 'Thou — Thou hast given by the hand of Thy servant this great salvation; and now, I die with thirst, and have fallen into the hand of the uncircumcised.'
19 Bwana akafunua shimo huko Lehi, pakatoka maji. Samsoni alipoyanywa, nguvu zikamrudia na kuhuika. Hivyo chemchemi ile ikaitwa En-Hakore, nayo iko mpaka leo huko Lehi.
And God cleaveth the hollow place which [is] in Lehi, and waters come out of it, and he drinketh, and his spirit cometh back, and he reviveth; therefore hath [one] called its name 'The fountain of him who is calling,' which [is] in Lehi unto this day.
20 Samsoni akawa mwamuzi wa Waisraeli katika siku za Wafilisti kwa muda wa miaka ishirini.
And he judgeth Israel in the days of the Philistines twenty years.

< Waamuzi 15 >