< Waamuzi 15 >

1 Baada ya kitambo kidogo, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mwana-mbuzi, kwenda kumzuru mkewe. Akasema, “Nataka kuingia chumbani kwa mke wangu.” Lakini baba yake huyo mwanamke hakumruhusu kuingia.
And it comes to pass after [some] days, in the days of wheat-harvest, that Samson looks after his wife, with a kid of the goats, and says, “I go in to my wife, to the inner chamber”; and her father has not permitted him to go in,
2 Huyo baba mkwe wake akamwambia, “Nilikuwa na hakika kwamba ulimkataa, hivyo mimi nikampa rafiki yako. Je, mdogo wake wa kike si mzuri zaidi kuliko yeye? Mchukue huyo badala yake.”
and her father says, “I certainly said that you surely hated her, and I give her to your companion; is her younger sister not better than she? Please let her be to you instead of her.”
3 Samsoni akawaambia, “Wakati huu, nitakapowadhuru Wafilisti, sitakuwa na lawama.”
And Samson says of them, “I am more innocent this time than the Philistines, though I am doing evil with them.”
4 Hivyo Samsoni akatoka akawakamata mbweha 300 na kuwafunga wawili wawili kwa mikia yao kila mmoja kwa mwingine. Kisha akafungia mwenge wa moto, kwenye mikia ya kila jozi moja ya mbweha aliyokuwa ameifunga,
And Samson goes and catches three hundred foxes, and takes torches, and turns tail to tail, and puts a torch between the two tails, in the midst,
5 akawasha ile mienge na kuwaachia wale mbweha katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka zilizosimamishwa katika matita. Akateketeza matita ya nafaka zilizosimama, pamoja na mashamba ya mizabibu na viunga vya mizeituni.
and kindles fire in the torches, and sends [them] out into the standing grain of the Philistines, and burns [it] from heap even to standing grain, even to vineyard [and] olive-yard.
6 Ndipo Wafilisti wakauliza, “Ni nani aliyetenda jambo hili?” Wakaambiwa, “Ni Samsoni, yule mkwewe Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake.” Hivyo Wafilisti wakapanda wakamteketeza kwa moto yeye huyo mwanamke pamoja na baba yake.
And the Philistines say, “Who has done this?” And they say, “Samson, son-in-law of the Timnite, because he has taken away his wife, and gives her to his companion”; and the Philistines go up, and burn her and her father with fire.
7 Samsoni akawaambia, “Kwa kuwa mmetenda hivyo, hakika sitatulia mpaka niwe nimelipiza kisasi juu yenu.”
And Samson says to them, “Though you do thus, nevertheless I am avenged on you, and afterward I cease!”
8 Akawashambulia kwa ukali kwa mapigo makuu na kuwaua watu wengi sana. Kisha akateremka na kukaa katika ufa kwenye mwamba wa Etamu.
And he strikes them hip and thigh [with] a great striking, and goes down and dwells in the cleft of the rock of Etam.
9 Wafilisti wakapanda na kupiga kambi huko Yuda na kuenea huko Lehi.
And the Philistines go up, and encamp in Judah, and are spread out in Lehi,
10 Watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kupigana nasi?” Wakawajibu, “Tumekuja ili kumkamata Samsoni na kumtenda kama alivyotutendea.”
and the men of Judah say, “Why have you come up against us?” And they say, “We have come up to bind Samson, to do to him as he has done to us.”
11 Ndipo watu 3,000 toka Yuda walipoteremka na kwenda kwenye ufa wa mwamba huko Etamu, na kumwambia Samsoni, “Je, hujatambua kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hiki ulichotutendea?” Akawajibu, “Mimi nimewatendea tu kile walichonitendea.”
And three thousand men of Judah go down to the cleft of the rock of Etam, and say to Samson, “Have you now known that the Philistines are rulers over us? And what [is] this you have done to us?” And he says to them, “As they did to me, so I did to them.”
12 Wakamwambia, “Tumekuja kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kuwa hamtaniua ninyi wenyewe.”
And they say to him, “We have come down to bind you—to give you into the hand of the Philistines.” And Samson says to them, “Swear to me, lest you fall on me yourselves.”
13 Wakamjibu, “Sisi hatutakuua, bali tutakufunga tu na kukutia mikononi mwao.” Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya. Wakamchukua toka huko kwenye ufa katika mwamba.
And they speak to him, saying, “No, but we certainly bind you, and have given you into their hand, and we certainly do not put you to death”; and they bind him with two thick bands, new ones, and bring him up from the rock.
14 Alipokaribia Lehi, Wafilisti wakamjia wakipiga kelele. Roho wa Bwana akamjia juu yake kwa nguvu. Kamba zilizomfunga mikono yake zikawa kama kitani iliyochomwa kwa moto, na vifungo vyake vikaanguka chini toka mikononi mwake.
He has come to Lehi—and the Philistines have shouted at meeting him—and the Spirit of YHWH prospers over him, and the thick bands which [are] on his arms are as flax which they burn with fire, and his bands are melted from off his hands,
15 Ndipo akaona mfupa mpya wa taya la punda, akanyoosha mkono, akauchukua na kuua nao Wafilisti wapatao 1,000.
and he finds a fresh jawbone of a donkey, and puts forth his hand and takes it, and strikes down one thousand men with it.
16 Ndipo Samsoni akasema, “Kwa taya la punda malundo juu ya malundo. Kwa taya la punda nimeua watu 1,000.”
And Samson says, “With the jawbone of a donkey, heap on heaps—I have struck down one thousand men with the jawbone of a donkey!”
17 Alipomaliza kusema, akautupa ule mfupa wa taya; na mahali pale pakaitwa Ramath-Lehi.
And it comes to pass, when he finishes speaking, that he casts away the jawbone out of his hand, and calls that place Ramath-Lehi;
18 Kwa kuwa alikuwa amesikia kiu sana, akamlilia Bwana akisema, “Umempa mtumishi wako ushindi huu mkuu. Je, sasa nife kwa kiu na kuangukia mikononi mwa hawa watu wasiotahiriwa?”
and he thirsts exceedingly, and calls to YHWH, and says, “You have given this great salvation by the hand of Your servant; and now, I die with thirst, and have fallen into the hand of the uncircumcised.”
19 Bwana akafunua shimo huko Lehi, pakatoka maji. Samsoni alipoyanywa, nguvu zikamrudia na kuhuika. Hivyo chemchemi ile ikaitwa En-Hakore, nayo iko mpaka leo huko Lehi.
And God cleaves the hollow place which [is] in Lehi, and waters come out of it, and he drinks, and his spirit comes back, and he revives; therefore [one] has called its name “The fountain of him who is calling,” which [is] in Lehi to this day.
20 Samsoni akawa mwamuzi wa Waisraeli katika siku za Wafilisti kwa muda wa miaka ishirini.
And he judges Israel in the days of the Philistines [for] twenty years.

< Waamuzi 15 >