< Waamuzi 15 >
1 Baada ya kitambo kidogo, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mwana-mbuzi, kwenda kumzuru mkewe. Akasema, “Nataka kuingia chumbani kwa mke wangu.” Lakini baba yake huyo mwanamke hakumruhusu kuingia.
But within a while after, in the time of wheate haruest, Samson visited his wife with a kid, saying, I wil go in to my wife into the chamber: but her father would not suffer him to goe in.
2 Huyo baba mkwe wake akamwambia, “Nilikuwa na hakika kwamba ulimkataa, hivyo mimi nikampa rafiki yako. Je, mdogo wake wa kike si mzuri zaidi kuliko yeye? Mchukue huyo badala yake.”
And her father sayde, I thought that thou hadst hated her: therefore gaue I her to thy companion. Is not her yonger sister fayrer then shee? take her, I pray thee, in stead of the other.
3 Samsoni akawaambia, “Wakati huu, nitakapowadhuru Wafilisti, sitakuwa na lawama.”
Then Samson saide vnto them, Nowe am I more blamelesse then the Philistims: therefore will I doe them displeasure.
4 Hivyo Samsoni akatoka akawakamata mbweha 300 na kuwafunga wawili wawili kwa mikia yao kila mmoja kwa mwingine. Kisha akafungia mwenge wa moto, kwenye mikia ya kila jozi moja ya mbweha aliyokuwa ameifunga,
And Samson went out, and tooke three hundreth foxes, and tooke firebrands, and turned them taile to taile, and put a firebrand in ye middes betweene two tailes.
5 akawasha ile mienge na kuwaachia wale mbweha katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka zilizosimamishwa katika matita. Akateketeza matita ya nafaka zilizosimama, pamoja na mashamba ya mizabibu na viunga vya mizeituni.
And when he had set the brandes on fire, he sent them out into the standing corne of the Philistims, and burnt vp both the rickes and the standing corne with the vineyardes and oliues.
6 Ndipo Wafilisti wakauliza, “Ni nani aliyetenda jambo hili?” Wakaambiwa, “Ni Samsoni, yule mkwewe Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake.” Hivyo Wafilisti wakapanda wakamteketeza kwa moto yeye huyo mwanamke pamoja na baba yake.
Then the Philistims sayde, Who hath done this? And they answered, Samson the sonne in law of the Timnite, because hee had taken his wife, and giuen her to his companion. Then the Philistims came vp and burnt her and her father with fire.
7 Samsoni akawaambia, “Kwa kuwa mmetenda hivyo, hakika sitatulia mpaka niwe nimelipiza kisasi juu yenu.”
And Samson saide vnto them, Though yee haue done this, yet wil I be auenged of you, and then I wil cease.
8 Akawashambulia kwa ukali kwa mapigo makuu na kuwaua watu wengi sana. Kisha akateremka na kukaa katika ufa kwenye mwamba wa Etamu.
So hee smote them hippe and thigh with a mightie plague: then hee went and dwelt in the top of the rocke Etam.
9 Wafilisti wakapanda na kupiga kambi huko Yuda na kuenea huko Lehi.
Then the Philistims came vp, and pitched in Iudah, and were spred abroad in Lehi.
10 Watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kupigana nasi?” Wakawajibu, “Tumekuja ili kumkamata Samsoni na kumtenda kama alivyotutendea.”
And the men of Iudah sayde, Why are yee come vp vnto vs? And they answered, To binde Samson are we come vp, and to do to him as hee hath done to vs.
11 Ndipo watu 3,000 toka Yuda walipoteremka na kwenda kwenye ufa wa mwamba huko Etamu, na kumwambia Samsoni, “Je, hujatambua kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hiki ulichotutendea?” Akawajibu, “Mimi nimewatendea tu kile walichonitendea.”
Then three thousande men of Iudah went to the top of the rocke Etam, and sayde to Samson, Knowest thou not that the Philistims are rulers ouer vs? Wherefore then hast thou done thus vnto vs? And he answered them, As they did vnto me, so haue I done vnto them.
12 Wakamwambia, “Tumekuja kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.” Samsoni akawaambia, “Niapieni kuwa hamtaniua ninyi wenyewe.”
Againe they sayd vnto him, Wee are come to binde thee, and to deliuer thee into the hande of the Philistims. And Samson sayde vnto them, Sweare vnto me, that yee will not fall vpon me your selues.
13 Wakamjibu, “Sisi hatutakuua, bali tutakufunga tu na kukutia mikononi mwao.” Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya. Wakamchukua toka huko kwenye ufa katika mwamba.
And they answered him, saying, No, but we will bynde thee and deliuer thee vnto their hande, but we will not kill thee. And they bound him with two newe cordes, and brought him from the rocke.
14 Alipokaribia Lehi, Wafilisti wakamjia wakipiga kelele. Roho wa Bwana akamjia juu yake kwa nguvu. Kamba zilizomfunga mikono yake zikawa kama kitani iliyochomwa kwa moto, na vifungo vyake vikaanguka chini toka mikononi mwake.
When hee came to Lehi, the Philistims shouted against him, and the Spirite of the Lord came vpon him, and the cordes that were vpon his armes, became as flaxe that was burnt with fire: for the bandes loosed from his handes.
15 Ndipo akaona mfupa mpya wa taya la punda, akanyoosha mkono, akauchukua na kuua nao Wafilisti wapatao 1,000.
And he found a new iawebone of an asse, and put forth his hand, and caught it, and slewe a thousand men therewith.
16 Ndipo Samsoni akasema, “Kwa taya la punda malundo juu ya malundo. Kwa taya la punda nimeua watu 1,000.”
Then Samson sayd, With the iaw of an asse are heapes vpon heapes: with the iawe of an asse haue I slaine a thousand men.
17 Alipomaliza kusema, akautupa ule mfupa wa taya; na mahali pale pakaitwa Ramath-Lehi.
And when he had left speaking, hee cast away the iawebone out of his hande, and called that place, Ramath-Lehi.
18 Kwa kuwa alikuwa amesikia kiu sana, akamlilia Bwana akisema, “Umempa mtumishi wako ushindi huu mkuu. Je, sasa nife kwa kiu na kuangukia mikononi mwa hawa watu wasiotahiriwa?”
And he was sore a thirst, and called on the Lord, and sayde, Thou hast giuen this great deliuerance into the hand of thy seruaunt: and nowe shall I dye for thirst, and fall into the handes of the vncircumcised?
19 Bwana akafunua shimo huko Lehi, pakatoka maji. Samsoni alipoyanywa, nguvu zikamrudia na kuhuika. Hivyo chemchemi ile ikaitwa En-Hakore, nayo iko mpaka leo huko Lehi.
Then God brake the cheeke tooth, that was in the iawe, and water came thereout: and when he had drunke, his Spirit came againe, and he was reuiued: wherefore the name therof is called, Enhakkore, which is in Lehi vnto this day.
20 Samsoni akawa mwamuzi wa Waisraeli katika siku za Wafilisti kwa muda wa miaka ishirini.
And hee iudged Israel in the dayes of the Philistims twentie yeeres.