< Waamuzi 14 >
1 Samsoni akateremkia Timna, akamwona mwanamke wa Kifilisti.
I siðe Samson u Tamnat, i vidje ondje jednu djevojku izmeðu kæeri Filistejskih.
2 Alipopanda kutoka huko, akawaambia baba yake na mama yake, “Nimemwona mwanamke wa Kifilisti huko Timna; basi mnipe ili awe mke wangu.”
I vrativši se kaza ocu svojemu i materi svojoj govoreæi: vidjeh djevojku u Tamnatu izmeðu kæeri Filistejskih; oženite me njom.
3 Baba yake na mama yake wakamjibu, “Je, hakuna mwanamke miongoni mwa jamaa yako au miongoni mwa ndugu zako, hata ulazimike kwenda kujitwalia mwanamke kutoka kwa hawa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Nipatieni huyo kwa maana ndiye alinipendeza.”
A otac i mati rekoše mu: zar nema djevojke meðu kæerima tvoje braæe u svem narodu mom, da ideš da se oženiš izmeðu Filisteja neobrezanijeh? A Samson odgovori ocu svojemu: njom me oženi, jer mi je ona omiljela.
4 (Baba yake na mama yake hawakujua kuwa jambo hili limetoka kwa Bwana, kwani alikuwa akitafuta sababu ya kukabiliana na Wafilisti; kwa kuwa wakati huo walikuwa wakiwatawala Waisraeli.)
A otac i mati njegova ne znadijahu da je to od Gospoda, i da traži zadjevicu s Filistejima; jer u ono vrijeme Filisteji vladahu sinovima Izrailjevijem.
5 Samsoni akateremkia Timna pamoja na baba yake na mama yake. Walipofika kwenye mashamba ya mizabibu huko Timna, ghafula mwana simba akamjia akimngurumia.
I tako side Samson s ocem svojim i s materom svojom u Tamnat, i kad doðoše do vinograda Tamnatskih, gle, mlad lav rièuæi sukobi ga.
6 Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu, naye akampasua yule simba kwa mikono yake bila silaha yoyote kama vile mtu ampasuavyo mwana-mbuzi, wala hakumwambia baba yake wala mama yake aliyoyafanya.
I duh Gospodnji side na nj, te rastrže lava kao jare nemajuæi ništa u ruci: i ne kaza ocu ni materi šta je uèinio.
7 Basi akateremka na kuongea na yule mwanamke, naye akampendeza Samsoni.
I tako došavši govori s djevojkom, i ona omilje Samsonu.
8 Baada ya muda aliporudi ili akamwoe, akatazama kando ili kuutazama mzoga wa yule simba, na tazama, kulikuwa na kundi la nyuki ndani ya ule mzoga wa simba na kulikuwa na asali;
A poslije nekoliko dana iduæi opet da je odvede, svrne da vidi mrtvoga lava; a gle, u mrtvom lavu roj pèela i med.
9 akachukua asali mkononi mwake akaendelea huku akila. Alipowafikia baba yake na mama yake, akawapa ile asali nao wakala. Lakini hakuwaambia kuwa alitwaa asali kutoka kwenye mzoga wa simba.
I izvadi ga u ruku, i poðe putem jeduæi; i kad doðe k ocu i materi, dade im te jedoše; ali im ne reèe da je iz mrtvoga lava izvadio med.
10 Basi baba yake akateremka kumwona huyo mwanamke. Samsoni akafanya karamu huko, kama ilivyokuwa desturi ya vijana.
I tako doðe otac njegov k onoj djevojci, i Samson uèini ondje veselje, jer tako èinjahu momci.
11 Watu walipomwona, wakaleta vijana wenzake thelathini ili kuwa pamoja naye.
I kad ga vidješe Filisteji, izabraše trideset druga da budu s njim.
12 Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.
I reèe im Samson: ja æu vam zagonenuti zagonetku, pa ako mi je odgonenete za sedam dana dok je veselje i pogodite, daæu vam trideset košulja i tridesetore sveèane haljine.
13 Lakini msipoweza kufumbua, ndipo ninyi mtanipa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.” Wakamwambia, “Tuambie hicho kitendawili, hebu na tukisikie.”
Ako li ne odgonenete, vi æete dati meni trideset košulja i tridesetore sveèane haljine. A oni mu rekoše: zagoneni zagonetku svoju, da èujemo.
14 Akawaambia, “Ndani ya mlaji, kulitoka kitu cha kuliwa, ndani ya mwenye nguvu, kulitoka kitu kitamu.” Kwa muda wa siku tatu hawakuweza kutoa jibu.
Tada im reèe: od onoga koji jede izide jelo, i od ljutoga izide slatko. I ne mogoše odgonenuti zagonetke tri dana.
15 Siku ya saba, wakamwambia mkewe Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atueleze hicho kitendawili, la sivyo tutakuchoma moto wewe na wa nyumba ya baba yako. Je, mmetualika ili mpate kutunyangʼanya kile tulicho nacho?”
I sedmi dan rekoše ženi Samsonovoj: nagovori muža svojega da nam kaže zagonetku, ili æemo spaliti ognjem tebe i dom oca tvojega. Jeste li nas zato pozvali da nam uzmete imanje? je li tako?
16 Basi mke wa Samsoni akalia mbele yake na kumwambia, “Unanichukia! Hunipendi kabisa. Umewategea watu wangu kitendawili, lakini mimi hujaniambia jibu.” Samsoni akamwambia, “Wala sijamweleza baba yangu wala mama yangu, kwa nini nikufumbulie?”
I stade plakati žena Samsonova pred njim govoreæi: ti mrziš na me, i ti me ne ljubiš; zagonenuo si zagonetku sinovima naroda mojega, a neæeš meni da je kažeš. A on joj reèe: gle, ni ocu svojemu ni materi svojoj nijesam je kazao, a tebi da je kažem?
17 Mkewe akalia kwa muda wa zile siku zote saba za karamu. Hivyo siku ile ya saba Samsoni akamweleza, kwa kuwa aliendelea kumsisitiza sana. Naye akawaeleza watu wake kile kitendawili.
I ona plaka pred njim za sedam dana dokle trajaše veselje. A sedmi dan kaza joj, jer bješe navalila na nj; a ona kaza zagonetku sinovima naroda svojega.
18 Siku ya saba kabla ya jua kutua, watu wa mji wakamwambia Samsoni, “Ni nini kitamu kama asali? Ni nini chenye nguvu kama simba?” Samsoni akawaambia, “Kama hamkulima na mtamba wangu, hamngeweza kufumbua kitendawili changu.”
Tada mu rekoše ljudi grada onoga sedmi dan dok sunce ne zaðe: šta je slaðe od meda, i šta je ljuæe od lava? A on im reèe: da nijeste orali na mojoj junici, ne biste pogodili moje zagonetke.
19 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Samsoni kwa nguvu. Akateremka mpaka Ashkeloni, akawaua watu waume thelathini miongoni mwa watu wa mji, akatwaa mali zao na nguo zao, akawapa watu wale waliofumbua kile kitendawili. Akiwa na hasira, akakwea kurudi nyumbani kwa baba yake.
I doðe na nj duh Gospodnji, te siðe u Askalon, i pobi ondje trideset ljudi, i uze odijelo s njih i dade sveèane haljine onima koji odgonenuše zagonetku; i rasrdi se vrlo i otide kuæi oca svojega.
20 Lakini huyo mke wa Samsoni akakabidhiwa kwa rafiki yake Samsoni ambaye alikuwa rafiki yake msaidizi siku ya arusi.
A žena Samsonova udade se za druga njegova, s kojim se bijaše udružio.