< Waamuzi 14 >
1 Samsoni akateremkia Timna, akamwona mwanamke wa Kifilisti.
Ensuite Samson descendit à Thamnatha; et voyant là une femme d’entre les filles des Philistins,
2 Alipopanda kutoka huko, akawaambia baba yake na mama yake, “Nimemwona mwanamke wa Kifilisti huko Timna; basi mnipe ili awe mke wangu.”
Il monta, et il l’annonça à son père et à sa mère, disant: J’ai vu à Thamnatha une femme d’entre les filles des Philistins, que je vous prie d’accepter pour mon épouse.
3 Baba yake na mama yake wakamjibu, “Je, hakuna mwanamke miongoni mwa jamaa yako au miongoni mwa ndugu zako, hata ulazimike kwenda kujitwalia mwanamke kutoka kwa hawa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Nipatieni huyo kwa maana ndiye alinipendeza.”
Son père et sa mère lui répondirent: Est-ce qu’il n’y a point de femme parmi les filles de tes frères, et dans tout mon peuple, puisque tu veux prendre une femme d’entre les Philistins qui sont incirconcis? Et Samson dit à son père: Acceptez-la pour moi, parce qu’elle a plu à mes yeux.
4 (Baba yake na mama yake hawakujua kuwa jambo hili limetoka kwa Bwana, kwani alikuwa akitafuta sababu ya kukabiliana na Wafilisti; kwa kuwa wakati huo walikuwa wakiwatawala Waisraeli.)
Mais ses parents ne savaient pas que la chose se faisait par le Seigneur, et qu’il cherchait une occasion contre les Philistins; car en ce temps-là les Philistins dominaient sur Israël.
5 Samsoni akateremkia Timna pamoja na baba yake na mama yake. Walipofika kwenye mashamba ya mizabibu huko Timna, ghafula mwana simba akamjia akimngurumia.
C’est pourquoi Samson descendit avec son père et sa mère à Thamnatha. Et, lorsqu’ils furent arrivés aux vignes de la ville, parut le petit d’un lion furieux et rugissant, et il vint à la rencontre de Samson.
6 Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu, naye akampasua yule simba kwa mikono yake bila silaha yoyote kama vile mtu ampasuavyo mwana-mbuzi, wala hakumwambia baba yake wala mama yake aliyoyafanya.
Mais l’Esprit du Seigneur s’empara de Samson, qui déchira le lion comme il aurait mis un chevreau en pièces, n’ayant absolument rien dans la main; et il ne voulut pas le déclarer à son père et à sa mère.
7 Basi akateremka na kuongea na yule mwanamke, naye akampendeza Samsoni.
Et il descendit, et il parla à la femme qui avait plu à ses yeux.
8 Baada ya muda aliporudi ili akamwoe, akatazama kando ili kuutazama mzoga wa yule simba, na tazama, kulikuwa na kundi la nyuki ndani ya ule mzoga wa simba na kulikuwa na asali;
Et, après quelques jours, revenant pour l’épouser, il se détourna pour voir le corps du lion, et voilà qu’un essaim d’abeilles était dans la gueule du lion, et un rayon de miel.
9 akachukua asali mkononi mwake akaendelea huku akila. Alipowafikia baba yake na mama yake, akawapa ile asali nao wakala. Lakini hakuwaambia kuwa alitwaa asali kutoka kwenye mzoga wa simba.
Ayant pris ce rayon dans ses mains, il le mangeait en chemin; et étant arrivé chez son père et sa mère, il leur en donna une partie, qu’eux-mêmes aussi mangèrent; mais cependant il ne voulut pas leur déclarer qu’il avait pris le miel dans la gueule du lion.
10 Basi baba yake akateremka kumwona huyo mwanamke. Samsoni akafanya karamu huko, kama ilivyokuwa desturi ya vijana.
Son père descendit donc chez cette femme, et il fit pour son fils Samson un festin; car c’est ainsi que les jeunes gens avaient coutume de faire.
11 Watu walipomwona, wakaleta vijana wenzake thelathini ili kuwa pamoja naye.
Or, lorsque les habitants de ce lieu l’eurent vu, ils lui donnèrent trente jeunes hommes pour être avec lui.
12 Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.
Samson leur dit: Je vous proposerai une énigme; si vous me l’expliquez pendant les sept jours du festin, je vous donnerai trente vêtements de dessous et autant de tuniques;
13 Lakini msipoweza kufumbua, ndipo ninyi mtanipa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.” Wakamwambia, “Tuambie hicho kitendawili, hebu na tukisikie.”
Mais si vous ne pouvez pas l’expliquer, c’est vous qui me donnerez trente vêtements de dessous et des tuniques en même nombre. Ils lui répondirent: Propose l’énigme afin que nous l’entendions.
14 Akawaambia, “Ndani ya mlaji, kulitoka kitu cha kuliwa, ndani ya mwenye nguvu, kulitoka kitu kitamu.” Kwa muda wa siku tatu hawakuweza kutoa jibu.
Alors Samson leur dit: De celui qui mangeait est sortie une nourriture, et du fort est sorti de la douceur; et ils ne purent point pendant trois jours expliquer l’énigme.
15 Siku ya saba, wakamwambia mkewe Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atueleze hicho kitendawili, la sivyo tutakuchoma moto wewe na wa nyumba ya baba yako. Je, mmetualika ili mpate kutunyangʼanya kile tulicho nacho?”
Mais, lorsqu’approchait le septième jour, ils dirent à la femme de Samson: Gagne ton mari par tes caresses, et persuade-lui de te donner la signification de l’énigme; que si tu ne veux pas le faire, nous te brûlerons, toi et la maison de ton père; est-ce que tu ne nous as appelés aux noces que pour nous dépouiller?
16 Basi mke wa Samsoni akalia mbele yake na kumwambia, “Unanichukia! Hunipendi kabisa. Umewategea watu wangu kitendawili, lakini mimi hujaniambia jibu.” Samsoni akamwambia, “Wala sijamweleza baba yangu wala mama yangu, kwa nini nikufumbulie?”
Elle répandait des larmes auprès de Samson, et se plaignait, disant: Tu me hais et tu ne m’aimes point; c’est pour cela que tu ne veux pas m’expliquer l’énigme que tu as proposée aux fils de mon peuple. Mais Samson répondit: Je ne l’ai point voulu dire à mon père et à ma mère; et je pourrai te l’expliquer?
17 Mkewe akalia kwa muda wa zile siku zote saba za karamu. Hivyo siku ile ya saba Samsoni akamweleza, kwa kuwa aliendelea kumsisitiza sana. Naye akawaeleza watu wake kile kitendawili.
Ainsi, pendant les sept jours du festin elle pleurait devant lui; et enfin le septième jour, comme elle lui était importune, il lui expliqua. Elle aussitôt la fit connaître à ses concitoyens.
18 Siku ya saba kabla ya jua kutua, watu wa mji wakamwambia Samsoni, “Ni nini kitamu kama asali? Ni nini chenye nguvu kama simba?” Samsoni akawaambia, “Kama hamkulima na mtamba wangu, hamngeweza kufumbua kitendawili changu.”
Et eux dirent à Samson le septième jour avant le coucher du soleil: Quoi de plus doux que du miel, et de plus fort que le lion? Et Samson leur répondit: Si vous n’aviez pas labouré avec ma génisse, vous n’auriez pas découvert mon énigme.
19 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Samsoni kwa nguvu. Akateremka mpaka Ashkeloni, akawaua watu waume thelathini miongoni mwa watu wa mji, akatwaa mali zao na nguo zao, akawapa watu wale waliofumbua kile kitendawili. Akiwa na hasira, akakwea kurudi nyumbani kwa baba yake.
C’est pourquoi l’esprit du Seigneur s’empara de Samson, et il descendit à Ascalon: et là il tua trente hommes dont il donna les vêtements qu’il leur avait pris à ceux qui avaient expliqué l’énigme. Et étant très irrité il monta à la maison de son père.
20 Lakini huyo mke wa Samsoni akakabidhiwa kwa rafiki yake Samsoni ambaye alikuwa rafiki yake msaidizi siku ya arusi.
Or, sa femme prit pour mari un de ses amis, un de ceux qui l’avaient accompagné à ses noces.