< Waamuzi 14 >

1 Samsoni akateremkia Timna, akamwona mwanamke wa Kifilisti.
Et Samson descendit à Thimna; et il vit à Thimna une femme d’entre les filles des Philistins.
2 Alipopanda kutoka huko, akawaambia baba yake na mama yake, “Nimemwona mwanamke wa Kifilisti huko Timna; basi mnipe ili awe mke wangu.”
Et il remonta et le raconta à son père et à sa mère, et dit: J’ai vu à Thimna une femme d’entre les filles des Philistins; et maintenant, prenez-la-moi pour femme.
3 Baba yake na mama yake wakamjibu, “Je, hakuna mwanamke miongoni mwa jamaa yako au miongoni mwa ndugu zako, hata ulazimike kwenda kujitwalia mwanamke kutoka kwa hawa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Nipatieni huyo kwa maana ndiye alinipendeza.”
Et son père et sa mère lui dirent: N’y a-t-il pas de femme parmi les filles de tes frères, et dans tout mon peuple, que tu ailles prendre une femme d’entre les Philistins, les incirconcis? Et Samson dit à son père: Prends celle-là pour moi, car elle plaît à mes yeux.
4 (Baba yake na mama yake hawakujua kuwa jambo hili limetoka kwa Bwana, kwani alikuwa akitafuta sababu ya kukabiliana na Wafilisti; kwa kuwa wakati huo walikuwa wakiwatawala Waisraeli.)
Et son père et sa mère ne savaient pas que cela venait de l’Éternel; car [Samson] cherchait une occasion de la part des Philistins. Or en ce temps-là les Philistins dominaient sur Israël.
5 Samsoni akateremkia Timna pamoja na baba yake na mama yake. Walipofika kwenye mashamba ya mizabibu huko Timna, ghafula mwana simba akamjia akimngurumia.
Et Samson descendit à Thimna avec son père et sa mère; et ils arrivèrent jusqu’aux vignes de Thimna. Et voici, un jeune lion rugissant [vint] à sa rencontre.
6 Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu, naye akampasua yule simba kwa mikono yake bila silaha yoyote kama vile mtu ampasuavyo mwana-mbuzi, wala hakumwambia baba yake wala mama yake aliyoyafanya.
Et l’Esprit de l’Éternel le saisit: et il le déchira, comme on déchire un chevreau, quoiqu’il n’ait rien en sa main; et il ne déclara point à son père ni à sa mère ce qu’il avait fait.
7 Basi akateremka na kuongea na yule mwanamke, naye akampendeza Samsoni.
Et il descendit, et parla à la femme, et elle plut aux yeux de Samson.
8 Baada ya muda aliporudi ili akamwoe, akatazama kando ili kuutazama mzoga wa yule simba, na tazama, kulikuwa na kundi la nyuki ndani ya ule mzoga wa simba na kulikuwa na asali;
Et il retourna quelque temps après pour la prendre, et se détourna pour voir le cadavre du lion; et voici, il y avait dans le corps du lion un essaim d’abeilles, et du miel;
9 akachukua asali mkononi mwake akaendelea huku akila. Alipowafikia baba yake na mama yake, akawapa ile asali nao wakala. Lakini hakuwaambia kuwa alitwaa asali kutoka kwenye mzoga wa simba.
et il en prit dans ses mains, et s’en alla, mangeant en chemin; et il alla vers son père et vers sa mère, et leur en donna, et ils en mangèrent; mais il ne leur raconta pas qu’il avait tiré le miel du corps du lion.
10 Basi baba yake akateremka kumwona huyo mwanamke. Samsoni akafanya karamu huko, kama ilivyokuwa desturi ya vijana.
Et son père descendit vers la femme, et Samson fit là un festin; car c’est ainsi que les jeunes gens avaient l’habitude de faire.
11 Watu walipomwona, wakaleta vijana wenzake thelathini ili kuwa pamoja naye.
Et il arriva que, quand ils le virent, ils prirent 30 compagnons, et ils furent avec lui.
12 Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.
Et Samson leur dit: Je vous proposerai, s’il vous plaît, une énigme; si vous me l’ expliquez dans les sept jours du festin et si vous la trouvez, je vous donnerai 30 chemises, et 30 vêtements de rechange.
13 Lakini msipoweza kufumbua, ndipo ninyi mtanipa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.” Wakamwambia, “Tuambie hicho kitendawili, hebu na tukisikie.”
Mais si vous ne pouvez pas me l’expliquer, c’est vous qui me donnerez 30 chemises, et 30 vêtements de rechange. Et ils lui dirent: Propose ton énigme, et nous l’entendrons.
14 Akawaambia, “Ndani ya mlaji, kulitoka kitu cha kuliwa, ndani ya mwenye nguvu, kulitoka kitu kitamu.” Kwa muda wa siku tatu hawakuweza kutoa jibu.
Et il leur dit: De celui qui mange est sorti le manger, et du fort est sortie la douceur. Et pendant trois jours ils ne purent expliquer l’énigme.
15 Siku ya saba, wakamwambia mkewe Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atueleze hicho kitendawili, la sivyo tutakuchoma moto wewe na wa nyumba ya baba yako. Je, mmetualika ili mpate kutunyangʼanya kile tulicho nacho?”
Et il arriva, le septième jour, qu’ils dirent à la femme de Samson: Persuade ton mari, et il nous expliquera l’énigme, de peur que nous ne te brûlions au feu, toi et la maison de ton père. C’est pour nous dépouiller que vous nous avez appelés, n’est-ce pas?
16 Basi mke wa Samsoni akalia mbele yake na kumwambia, “Unanichukia! Hunipendi kabisa. Umewategea watu wangu kitendawili, lakini mimi hujaniambia jibu.” Samsoni akamwambia, “Wala sijamweleza baba yangu wala mama yangu, kwa nini nikufumbulie?”
Et la femme de Samson pleura auprès de lui, et dit: Tu n’as pour moi que de la haine, et tu ne m’aimes pas; tu as proposé une énigme aux fils de mon peuple, et tu ne me l’as pas expliquée. Et il lui dit: Voici, je ne l’ai pas expliquée à mon père et à ma mère, et je te l’expliquerais à toi?
17 Mkewe akalia kwa muda wa zile siku zote saba za karamu. Hivyo siku ile ya saba Samsoni akamweleza, kwa kuwa aliendelea kumsisitiza sana. Naye akawaeleza watu wake kile kitendawili.
Et elle pleura auprès de lui pendant les sept jours qu’ils eurent le festin; et il arriva, le septième jour, qu’il la lui expliqua, parce qu’elle le tourmentait; et elle expliqua l’énigme aux fils de son peuple.
18 Siku ya saba kabla ya jua kutua, watu wa mji wakamwambia Samsoni, “Ni nini kitamu kama asali? Ni nini chenye nguvu kama simba?” Samsoni akawaambia, “Kama hamkulima na mtamba wangu, hamngeweza kufumbua kitendawili changu.”
Et le septième jour, avant que le soleil se couche, les hommes de la ville lui dirent: Qu’y a-t-il de plus doux que le miel, et qu’y a-t-il de plus fort que le lion? Et il leur dit: Si vous n’aviez pas labouré avec ma génisse, vous n’auriez pas trouvé mon énigme.
19 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Samsoni kwa nguvu. Akateremka mpaka Ashkeloni, akawaua watu waume thelathini miongoni mwa watu wa mji, akatwaa mali zao na nguo zao, akawapa watu wale waliofumbua kile kitendawili. Akiwa na hasira, akakwea kurudi nyumbani kwa baba yake.
Et l’Esprit de l’Éternel le saisit; et il descendit à Askalon, et en tua 30 hommes, et prit leurs dépouilles, et donna les vêtements de rechange à ceux qui avaient expliqué l’énigme. Et sa colère s’embrasa, et il monta à la maison de son père.
20 Lakini huyo mke wa Samsoni akakabidhiwa kwa rafiki yake Samsoni ambaye alikuwa rafiki yake msaidizi siku ya arusi.
Et la femme de Samson fut [donnée] à son compagnon, dont il avait fait son ami.

< Waamuzi 14 >