< Waamuzi 14 >

1 Samsoni akateremkia Timna, akamwona mwanamke wa Kifilisti.
Samson descendit à Thamna, et il vit à Thamna une femme d'entre les filles des Philistins.
2 Alipopanda kutoka huko, akawaambia baba yake na mama yake, “Nimemwona mwanamke wa Kifilisti huko Timna; basi mnipe ili awe mke wangu.”
Lorsqu'il fut remonté, il le déclara à son père et à sa mère, en disant: " J'ai vu à Thamna une femme d'entre les filles des Philistins; prenez-la maintenant pour être ma femme. "
3 Baba yake na mama yake wakamjibu, “Je, hakuna mwanamke miongoni mwa jamaa yako au miongoni mwa ndugu zako, hata ulazimike kwenda kujitwalia mwanamke kutoka kwa hawa Wafilisti wasiotahiriwa?” Lakini Samsoni akamwambia baba yake, “Nipatieni huyo kwa maana ndiye alinipendeza.”
Son père et sa mère lui dirent: " N'y a-t-il point de femme parmi les filles de tes frères et dans tout notre peuple, que tu ailles prendre une femme chez les Philistins, qui sont incirconcis? " Et Samson dit à son père: " Prends celle-là pour moi, car elle me plaît. "
4 (Baba yake na mama yake hawakujua kuwa jambo hili limetoka kwa Bwana, kwani alikuwa akitafuta sababu ya kukabiliana na Wafilisti; kwa kuwa wakati huo walikuwa wakiwatawala Waisraeli.)
Son père et sa mère ne savaient pas que cela venait de Yahweh; car il cherchait une occasion de querelle venant des Philistins. — En ce temps-là les Philistins dominaient sur Israël.
5 Samsoni akateremkia Timna pamoja na baba yake na mama yake. Walipofika kwenye mashamba ya mizabibu huko Timna, ghafula mwana simba akamjia akimngurumia.
Samson descendit avec son père et sa mère à Thamna. Lorsqu'ils arrivèrent aux vignes de Thamna, voici qu'un jeune lion rugissant vint à sa rencontre.
6 Roho wa Bwana akaja juu yake kwa nguvu, naye akampasua yule simba kwa mikono yake bila silaha yoyote kama vile mtu ampasuavyo mwana-mbuzi, wala hakumwambia baba yake wala mama yake aliyoyafanya.
L'Esprit de Yahweh saisit Samson; et, sans avoir rien à la main, Samson déchira le lion comme on déchire un chevreau. Et il ne raconta pas à son père et à sa mère ce qu'il avait fait.
7 Basi akateremka na kuongea na yule mwanamke, naye akampendeza Samsoni.
Il descendit et parla à la femme, et elle lui plut.
8 Baada ya muda aliporudi ili akamwoe, akatazama kando ili kuutazama mzoga wa yule simba, na tazama, kulikuwa na kundi la nyuki ndani ya ule mzoga wa simba na kulikuwa na asali;
Quelque temps après, s'étant rendu de nouveau à Thamna pour la prendre, il fit un détour pour voir le cadavre du lion, et voici qu'il y avait un essaim d'abeilles et du miel dans le corps du lion.
9 akachukua asali mkononi mwake akaendelea huku akila. Alipowafikia baba yake na mama yake, akawapa ile asali nao wakala. Lakini hakuwaambia kuwa alitwaa asali kutoka kwenye mzoga wa simba.
Il en prit dans ses mains et en mangea chemin faisant; et lorsqu'il fut arrivé près de son père et de sa mère, il leur en donna et ils en mangèrent; mais il ne leur dit pas qu'il avait pris le miel dans le corps du lion.
10 Basi baba yake akateremka kumwona huyo mwanamke. Samsoni akafanya karamu huko, kama ilivyokuwa desturi ya vijana.
Le père de Samson descendit chez la femme; et là, Samson donna un festin, car c'était la coutume des jeunes gens.
11 Watu walipomwona, wakaleta vijana wenzake thelathini ili kuwa pamoja naye.
Dès qu'on le vit, on invita trente compagnons pour être avec lui.
12 Samsoni akawaambia, “Niwape kitendawili, mkiweza kunipa jibu katika muda wa siku hizi saba za karamu, nitawapa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.
Samson leur dit: " Je vais vous proposer une énigme. Si vous me l'expliquez pendant les sept jours du festin et si vous la devinez, je vous donnerai trente tuniques et trente vêtements de rechange;
13 Lakini msipoweza kufumbua, ndipo ninyi mtanipa mavazi thelathini ya kitani na mavazi mengine mivao thelathini.” Wakamwambia, “Tuambie hicho kitendawili, hebu na tukisikie.”
mais si vous me pouvez pas me l'expliquer, c'est vous qui me donnerez trente tuniques et trente vêtements de rechange. " Ils lui dirent: " Propose ton énigme, que nous l'entendions. "
14 Akawaambia, “Ndani ya mlaji, kulitoka kitu cha kuliwa, ndani ya mwenye nguvu, kulitoka kitu kitamu.” Kwa muda wa siku tatu hawakuweza kutoa jibu.
Il leur dit: " De celui qui mange est sorti ce qui se mange, du fort est sorti le doux. " Pendant trois jours, ils ne purent expliquer l'énigme.
15 Siku ya saba, wakamwambia mkewe Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atueleze hicho kitendawili, la sivyo tutakuchoma moto wewe na wa nyumba ya baba yako. Je, mmetualika ili mpate kutunyangʼanya kile tulicho nacho?”
Le septième jour, ils dirent à la femme de Samson: " Persuade à ton mari de nous expliquer l'énigme; sinon, nous te brûlerons, toi et la maison de ton père. C'est pour nous dépouiller que vous nous avez invités, sans doute? "
16 Basi mke wa Samsoni akalia mbele yake na kumwambia, “Unanichukia! Hunipendi kabisa. Umewategea watu wangu kitendawili, lakini mimi hujaniambia jibu.” Samsoni akamwambia, “Wala sijamweleza baba yangu wala mama yangu, kwa nini nikufumbulie?”
La femme de Samson pleurait auprès de lui et disait: " Tu n'as pour moi que de la haine, et tu me m'aimes pas. Tu as proposé une énigme aux fils de mon peuple, et tu ne me l'as pas expliquée! " Il lui répondit: " Je ne l'ai expliquée ni à mon père ni à ma mère, et je te l'expliquerais! "
17 Mkewe akalia kwa muda wa zile siku zote saba za karamu. Hivyo siku ile ya saba Samsoni akamweleza, kwa kuwa aliendelea kumsisitiza sana. Naye akawaeleza watu wake kile kitendawili.
Elle pleura ainsi devant lui pendant les sept jours que dura le festin; le septième jour, comme elle le tourmentait, il lui expliqua l'énigme, et elle l'expliqua aux enfants de son peuple.
18 Siku ya saba kabla ya jua kutua, watu wa mji wakamwambia Samsoni, “Ni nini kitamu kama asali? Ni nini chenye nguvu kama simba?” Samsoni akawaambia, “Kama hamkulima na mtamba wangu, hamngeweza kufumbua kitendawili changu.”
Les gens de la ville dirent à Samson, le septième jour, avant le coucher du soleil: " Quoi de plus doux que le miel, et quoi de plus fort que le lion? " Et il leur dit: " Si vous n'aviez pas labouré avec ma génisse, vous n'auriez pas deviné mon énigme. "
19 Ndipo Roho wa Bwana akamjia Samsoni kwa nguvu. Akateremka mpaka Ashkeloni, akawaua watu waume thelathini miongoni mwa watu wa mji, akatwaa mali zao na nguo zao, akawapa watu wale waliofumbua kile kitendawili. Akiwa na hasira, akakwea kurudi nyumbani kwa baba yake.
L'Esprit de Yahweh le saisit, et il descendit à Ascalon. Il y tua trente hommes et, ayant pris leurs dépouilles, il donna les vêtements de rechange à ceux qui avaient expliqué l'énigme. Puis, enflammé de colère, il monta à la maison de son père.
20 Lakini huyo mke wa Samsoni akakabidhiwa kwa rafiki yake Samsoni ambaye alikuwa rafiki yake msaidizi siku ya arusi.
La femme de Samson fut donnée à l'un de ses compagnons qu'il s'était choisi pour ami.

< Waamuzi 14 >