< Waamuzi 12 >
1 Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
И собрашася мужие Ефремли и приидоша в Сефину, и реша Иеффаю: почто ходил еси ополчитися на сыны Аммони, и нас не позвал еси ити с тобою? Дом твой с тобою сожжем огнем.
2 Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
И рече к ним Иеффай: имех прю аз и людие мои, и сынове Аммони оскорбиша мене зело: и воззвах вас, и не избависте мене от руки их:
3 Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
и видех, яко не бяше спасающаго, и положих душу мою в руку мою, и приидох к сыном Аммоним, и предаде я Господь в руку мою: и вскую приидосте ко мне днесь, ополчити ли ся на мя?
4 Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
И собра Иеффай вся мужы Галаадски и ополчися на Ефрема: и избиша мужие Галаадстии Ефрема, понеже глаголаху: уцелевшии от Ефрема, вы Галаад среде Ефрема и среде Манассии.
5 Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
И засяде Галаад проходы у Иордана Ефремовы. И бысть егда реша уцелевшии от Ефрема: прейдем: и рекоша им мужие Галаадстии: еда ли от Ефрема вы? И реша: несмы.
6 walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
И реша им: рцыте, клас. И не управиша рещи тако: и имаху их, и закалаху у преходов Иорданих: и падоша в то время от Ефрема четыредесять и две тысящы.
7 Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
И суди Иеффай Израилеви лет шесть: и умре Иеффай Галаадитин, и погребен бысть во граде своем в Галааде.
8 Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
И суди по нем Израилеви Есевон от Вифлеема:
9 Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
и быша ему тридесять сыны и тридесять дщери, яже отдаде вон (мужем), и тридесять жен приведе сыном своим отвне: и суди Израилеви седмь лет:
10 Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
и умре Есевон, и погребен бысть в Вифлееме.
11 Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
И суди по нем Израилеви Елон Завулонянин десять лет:
12 Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
и умре Елон Завулонянин, и погребен бысть во Елиме в земли Завулони.
13 Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
И суди по нем Израилеви Авдон сын Еллихов Фарафонитин:
14 Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
и быша ему четыредесять сынове и тридесять внуцы, ездящии на седмидесяти ослех: и суди Израилеви осмь лет:
15 Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.
и умре Авдон сын Еллихов Фарафонитин, и погребен бысть в Фарафоне, в земли Ефремли, в горе Амаликове.