< Waamuzi 12 >

1 Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
Les hommes d’Ephraïm, s’étant rassemblés, passèrent vers Saphon et dirent à Jephté: « Pourquoi es-tu allé combattre les fils d’Ammon, sans nous avoir appelés à marcher avec toi? Nous allons brûler sur toi ta maison. »
2 Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
Jephté leur répondit: « J’étais, moi et mon peuple, en grande contestation avec les fils d’Ammon; alors je vous ai appelés, mais vous ne m’avez pas délivré de leurs mains.
3 Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
Voyant que tu ne venais pas à mon secours, j’ai risqué ma vie et j’ai marché contre les fils d’Ammon; et Yahweh les a livrés entre mes mains. Pourquoi donc êtes-vous montés aujourd’hui vers moi, pour me faire la guerre? »
4 Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
Jephté rassembla tous les hommes de Galaad, et livra bataille à Ephraïm. Les hommes de Galaad battirent ceux d’Ephraïm, car ceux-ci avaient dit: « Vous n’êtes, ô Galaadites, que des fugitifs d’Ephraïm, au milieu d’Ephraïm et de Manassé! »
5 Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
Galaad s’empara des gués du Jourdain du côté d’Ephraïm, et quand l’un des fuyards d’Ephraïm disait: « Laissez-moi passer, » les hommes de Galaad lui demandaient: « Es-tu Ephraïmite? » Il répondait: « Non ».
6 walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
Ils lui disaient alors: « Eh bien, dis: Schibboleth. » Et il disait: « Sibboleth, » ne réussissant pas à bien prononcer. Ils le saisissaient alors et l’égorgeaient près des gués du Jourdain. Il périt en ce temps-là quarante-deux mille hommes d’Ephraïm.
7 Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
Jephté jugea Israël pendant six ans; puis Jephté le Galaadite mourut et fut enterré dans l’une des villes de Galaad.
8 Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
Après lui, Abesan, de Bethléem, fut juge en Israël.
9 Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
Il eut trente fils; il maria trente filles hors de sa maison, et il fit venir du dehors trente filles pour ses fils. Il fut juge en Israël pendant sept ans;
10 Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
ensuite Abesan mourant et fut enterré à Bethléem.
11 Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
Après lui, Ahialon, de Zabulon, fut juge en Israël; il fut juge en Israël pendant dix ans;
12 Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
puis Ahialon, de Zabulon, mourut et fut enterré à Ajalon, dans le pays de Zabulon.
13 Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
Après lui, Abdon, fils d’Illel, de Pharathon fut juge en Israël.
14 Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
Il eut quarante fils et trente petits-fils, qui montaient sur soixante-dix ânons. Il fut juge en Israël pendant huit ans;
15 Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.
puis Abdon, fils d’Illel, de Pharathon, mourut et fut enterré à Pharathon, dans le pays d’Ephraïm, sur la montagne des Amalécites.

< Waamuzi 12 >