< Waamuzi 12 >

1 Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
`Lo! forsothe discencioun roos in Effraym; for whi thei, that passiden ayens the north, seiden to Jepte, Whi yedist thou to batel ayens the sones of Amon, and noldist clepe vs, that we schulden go with thee? Therfor we schulen brenne thin hows.
2 Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
To whiche he answeride, Greet strijf was to me and to my puple ayens the sones of Amon, and Y clepide you, that ye schulden `yyue help to me, and ye nolden do.
3 Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
`Which thing Y siy, and puttide my lijf in myn hondis; and Y passide to the sones of Amon, and `the Lord bitook hem in to myn hondis; what haue Y disseruyd, that ye ryse togidere ayens me in to batel?
4 Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
Therfor whanne alle the men of Galaad weren clepid to hym, he fauyt ayens Effraym; and the men of Galaad smytiden Effraym; for he seide, Galaad is `fugitif ether exilid fro Effraym, and dwellith in the myddis of Effraym and of Manasses.
5 Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
And the men of Galaad ocupieden the forthis of Jordan, bi whiche Effraym schulden turne ayen. And whanne a man fleynge of the noumbre of Effraym hadde come to tho forthis, and hadde seid, Y biseche, that thou suffre me passe; men of Galaad seiden to hym, Whether thou art a man of Effraym? And whanne he seide, Y am not,
6 walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
thei axiden hym, Seie thou therfor Sebolech, `whiche is interpretid, `an eer of corn. Which answeride, Thebolech, and myyte not brynge forth an eer of corn bi the same lettre. And anoon thei strangeliden hym takun in thilke passyng of Jordan; and two and fourti thousynde of Effraym felden doun in that tyme.
7 Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
And so Jepte, `a man of Galaad, demyde Israel sixe yeer; and he `was deed, and biried in his citee Galaad.
8 Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
Abethsan of Bethleem, that hadde thretti sones, and so many douytris, demyde Israel aftir Jepte;
9 Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
whiche douytris he sente out, and yaf to hosebondis, and he took wyues to hise sones of the same noumbre, and brouyte in to hys hows; which demyde Israel seuene yeer;
10 Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
and he `was deed, and biried in Bethleem.
11 Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
Whos successour was Hailon of Zabulon; and he demyde Israel ten yeer;
12 Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
and he was deed, and biried in Zabulon.
13 Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
Aftir hym Abdon, the sone of Ellel, of Pharaton, demyde Israel;
14 Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
which Abdon hadde fourti sones, and of hem thretti sones, stiynge on seuenti coltis of femal assis, `that is, mulis, and he demyde Israel eiyte yeer;
15 Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.
and he `was deed, and biried in Pharaton, in the loond of Effraym, in the hil of Amalech.

< Waamuzi 12 >