< Waamuzi 11 >
1 Basi Yefta Mgileadi alikuwa mtu shujaa. Baba yake alikuwa Gileadi, naye mama yake alikuwa kahaba.
At that time, there was a Gileadite, Jephthah, a very strong man and a fighter, the son of a kept woman, and he was born of Gilead.
2 Mke wa Gileadi akamzalia wana wengine, nao watoto hao walipokua, wakamfukuza Yefta na kumwambia, “Wewe huwezi kupata urithi katika jamii yetu, kwa sababu wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.”
Now Gilead had a wife, from whom he received sons. And they, after growing up, cast out Jephthah, saying, “You cannot inherit in the house of our father, because you were born of another mother.”
3 Basi Yefta akawakimbia ndugu zake akaenda kuishi katika nchi ya Tobu, mahali ambako watu waasi walijiunga naye na kumfuata.
And so, fleeing and avoiding them, he lived in the land of Tob. And men who were indigent and robbers joined with him, and they followed him as their leader.
4 Baada ya muda Waamoni wakafanya vita na Israeli,
In those days, the sons of Ammon fought against Israel.
5 viongozi wa Gileadi wakaenda kumchukua Yefta katika nchi ya Tobu.
And being steadfastly attacked, the elders of Gilead traveled so that they might obtain for their assistance Jephthah, from the land of Tob.
6 Wakamwambia Yefta, “Uwe jemadari wetu, ili tuweze kupigana na Waamoni.”
And they said to him, “Come and be our leader, and fight against the sons of Ammon.”
7 Yefta akawaambia, “Je, hamkunichukia mimi na kunifukuza katika nyumba ya baba yangu? Kwa nini mnanijia sasa, wakati mna matatizo.”
But he answered them: “Are you not the ones who hated me, and who cast me out of my father’s house? And yet now you come to me, compelled by necessity?”
8 Viongozi wa Gileadi wakamwambia Yefta, “Lakini sasa tumegeuka kukuelekea wewe, ili uende pamoja nasi kupigana na Waamoni, nawe utakuwa kiongozi wetu juu ya watu wote wa Gileadi.”
And the leaders of Gilead said to Jephthah, “But it is due to this necessity that we have approached you now, so that you may set out with us, and fight against the sons of Ammon, and be commander over all who live in Gilead.”
9 Yefta akawaambia, “Ikiwa mtanirudisha kwetu kupigana na Waamoni, naye Bwana akanisaidia kuwashinda, Je, ni kweli nitakuwa kiongozi wenu?”
Jephthah also said to them: “If you have come to me so that I may fight for you against the sons of Ammon, and if the Lord will deliver them into my hands, will I truly be your leader?”
10 Viongozi wa Gileadi wakamjibu Yefta, “Bwana ndiye shahidi yetu. Kwa hakika tutafanya kama usemavyo.”
They answered him, “The Lord who hears these things is himself the Mediator and the Witness that we shall do what we have promised.”
11 Basi Yefta akaenda na viongozi wa Gileadi, nao watu wakamfanya kiongozi na jemadari wao. Naye akarudia maneno yake yote mbele za Bwana huko Mispa.
And so Jephthah went with the leaders of Gilead, and all the people made him their leader. And Jephthah spoke all his words, in the sight of the Lord, at Mizpah.
12 Ndipo Yefta akatuma wajumbe kwa mfalme wa Waamoni akisema, “Una nini juu yetu, hata umekuja kushambulia nchi yetu?”
And he sent messengers to the king of the sons of Ammon, who said on his behalf, “What is there between you and me, that you would approach against me, so that you might lay waste to my land?”
13 Mfalme wa Waamoni akawajibu wajumbe wale wa Yefta, “Wakati Waisraeli walipopanda kutoka Misri, waliichukua nchi yangu kuanzia Arnoni mpaka Yaboki, hadi kufikia Yordani. Sasa rudisha kwa amani.”
And he responded to them, “It is because Israel took my land, when he ascended from Egypt, from the parts of Arnon, as far as the Jabbok and the Jordan. Now therefore, restore these to me with peace.”
14 Yefta akarudisha wajumbe kwa mfalme wa Waamoni,
And Jephthah again commissioned them, and he ordered them to say to the king of Ammon:
15 kusema: “Hili ndilo asemalo Yefta, Israeli hawakuchukua nchi ya Moabu wala ya Waamoni.
“Jephthah says this: Israel did not take the land of Moab, nor the land of the sons of Ammon.
16 Lakini walipopanda kutoka Misri, Israeli walipitia katika jangwa hadi Bahari ya Shamu na wakafika Kadeshi.
But when they ascended together from Egypt, he walked through the desert as far as the Red Sea, and he went into Kadesh.
17 Ndipo Israeli wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu, wakisema, ‘Tupe ruhusa kupita katika nchi yako,’ Lakini mfalme wa Edomu hakutusikia. Wakapeleka pia wajumbe kwa mfalme wa Moabu, naye akakataa. Kwa hiyo Israeli wakakaa huko Kadeshi.
And he sent messengers to the king of Edom, saying, ‘Permit me to pass through your land.’ But he was not willing to agree to his petition. Likewise, he sent to the king of Moab, who also refused to offer him passage. And so he delayed in Kadesh,
18 “Baadaye wakasafiri kupitia jangwa, wakiambaa na nchi za Edomu na Moabu, wakapitia upande wa mashariki wa nchi ya Moabu na kupiga kambi upande mwingine wa Arnoni. Hawakuingia katika nchi ya Moabu, kwa kuwa Arnoni ilikuwa mpaka wake.
and he circled around the side of the land of Edom and the land of Moab. And he arrived opposite the eastern region of the land of Moab. And he made camp across the Arnon. But he was not willing to enter the borders of Moab. (Of course, Arnon is the border of the land of Moab.)
19 “Kisha Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, na kumwambia, ‘Tupe ruhusa kupita katika nchi yako ili kufikia mahali petu.’
And so Israel sent messengers to Sihon, the king of the Amorites, who was living at Heshbon. And they said to him, “Permit me to cross through your land as far as the river.”
20 Hata hivyo, Sihoni hakuwaamini Waisraeli kupita katika nchi yake. Akaandaa jeshi lake lote na kupiga kambi huko Yahasa, nao wakapigana na Israeli.
But he, too, despising the words of Israel, would not permit him to cross through his borders. Instead, gathering an innumerable multitude, he went out against him at Jahaz, and he resisted strongly.
21 “Ndipo Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawashinda. Israeli wakaitwaa nchi yote ya Waamori, waliokuwa wakiishi katika nchi hiyo,
But the Lord delivered him, with his entire army, into the hands of Israel. And he struck him down, and he possessed all the land of the Amorite, the inhabitant of that region,
22 wakiiteka nchi yote kuanzia Arnoni mpaka Yaboki, na kutoka jangwani mpaka Yordani.
with all its parts, from the Arnon as far as the Jabbok, and from the wilderness even to the Jordan.
23 “Basi kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, amewafukuza Waamori watoke mbele ya watu wake Israeli, wewe unayo haki gani ya kuitamalaki?
Therefore, it was the Lord, the God of Israel, who overthrew the Amorites, by means of his people Israel fighting against them. And now you wish to possess his land?
24 Je, haikupasi kuchukua kile ambacho mungu wako Kemoshi amekupa? Vivyo hivyo, chochote kile Bwana Mungu wetu alichotupa sisi, tutakimiliki.
Are not the things that your god Chemosh possesses owed to you by right? And so, what the Lord our God has obtained by victory falls to us as a possession.
25 Je, wewe ni bora kuliko Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu? Je, yeye alishagombana na Israeli au kupigana nao wakati wowote?
Or are you, perhaps, better than Balak, the son of Zippor, the king of Moab? Or are you able to explain what his argument was against Israel, and why he fought against him?
26 Kwa maana kwa miaka 300 Israeli wameishi Heshboni na vijiji vyake, Aroeri na vijiji vyake, na katika miji yote iliyo kando ya Arnoni. Kwa nini wewe haukuyachukua wakati huo?
And though he has lived in Heshbon, and its villages, and in Aroer, and its villages, and in all the cities near the Jordan for three hundred years, why have you, for such long a time, put forward nothing about this claim?
27 Mimi sijakukosea jambo lolote, bali wewe ndiye unayenikosea kwa kufanya vita nami. Basi Bwana, aliye Mwamuzi, leo na aamue ugomvi kati ya Waisraeli na Waamoni.”
Therefore, I am not sinning against you, but you are doing evil against me, by declaring an unjust war against me. May the Lord be the Judge and the Arbiter this day, between Israel and the sons of Ammon.”
28 Hata hivyo, Mfalme wa Waamoni, hakuyajali maneno ya ujumbe wa Yefta.
But the king of the sons of Ammon was not willing to agree to the words of Jephthah that he commissioned by the messengers.
29 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Yefta. Akapita katikati ya Gileadi na Manase, pia akapita katika Mispa ya Gileadi, na kutokea huko akasonga mbele kushambulia Waamoni.
Therefore, the Spirit of the Lord rested upon Jephthah, and circling around Gilead, and Manasseh, and also Mizpah of Gilead, and crossing from there to the sons of Ammon,
30 Naye Yefta akaweka nadhiri mbele za Bwana akisema, “Ikiwa utawatia Waamoni mikononi mwangu,
he made a vow to the Lord, saying, “If you will deliver the sons of Ammon into my hands,
31 chochote kile kitakachotoka katika mlango wa nyumba yangu cha kwanza ili kunilaki nirudipo kwa amani katika kuwashinda Waamoni, kitakuwa ni cha Bwana na nitakitoa kuwa sadaka ya kuteketezwa.”
whoever will be the first to depart from the doors of my house to meet me, when I return in peace from the sons of Ammon, the same will I offer as a holocaust to the Lord.”
32 Ndipo Yefta akavuka kupigana na hao Waamoni, naye Bwana akawatia mkononi mwake.
And Jephthah crossed to the sons of Ammon, so that he might fight against them. And the Lord delivered them into his hands.
33 Akawapiga kwa ushindi mkubwa kuanzia Aroeri mpaka karibu na Minithi na kuendelea mpaka Abel-Keramimu, miji yote iliyopigwa ni ishirini. Basi Israeli wakawashinda Waamoni.
And he struck them down from Aroer, as far as the entrance to Minnith, twenty cities, and as far as Abel, which is covered with vineyards, in an exceedingly great slaughter. And the sons of Ammon were humbled by the sons of Israel.
34 Yefta aliporudi nyumbani Mispa, tazama, binti yake akatoka ili kumlaki kwa matari na kucheza. Alikuwa ndiye mtoto pekee, hakuwa na mwana wala binti mwingine.
But when Jephthah returned to Mizpah, to his own house, his only daughter met him with timbrels and dances. For he had no other children.
35 Alipomwona akararua mavazi yake akalia, “Ee! Binti yangu! Umenifanya niwe na huzuni na kunyongʼonyea sana, kwa kuwa nimeweka nadhiri kwa Bwana, ambayo siwezi kuivunja.”
And upon seeing her, he tore his garments, and he said: “Alas, my daughter! You have cheated me, and you yourself have been cheated. For I opened my mouth to the Lord, and I can do nothing else.”
36 Akajibu, “Baba yangu, umetoa neno lako kwa Bwana. Nitendee mimi kama vile ulivyoahidi, kwa kuwa Bwana amekupa ushindi dhidi ya adui zako Waamoni.”
And she answered him, “My father, if you have opened your mouth to the Lord, do to me whatever you have promised, since victory has been granted to you, as well as vengeance against your enemies.”
37 Naye akamwambia baba yake, “Naomba nifanyiwe jambo hili. Nipewe miezi miwili ili kuzunguka vilimani nikaulilie ubikira wangu, mimi na wenzangu.”
And she said to her father: “Grant to me this one thing, which I request. Permit me, that I may wander the hillsides for two months, and that I may mourn my virginity with my companions.”
38 Baba yake akamwambia, “Waweza kwenda.” Naye akamwacha aende kwa miezi miwili. Hivyo akaondoka pamoja na wasichana wenzake, naye akaulilia ubikira wake huko vilimani kwa sababu asingeolewa kamwe.
And he answered her, “Go.” And he released her for two months. And when she had departed with her friends and companions, she wept over her virginity in the hillsides.
39 Baada ya hiyo miezi miwili, alirejea kwa baba yake, naye baba yake akamtendea kama alivyokuwa ametoa nadhiri yake. Naye alikuwa bikira. Nayo ikawa desturi katika Israeli,
And when the two months expired, she returned to her father, and he did to her just as he had vowed, though she knew no man. From this, the custom grew up in Israel, and the practice has been preserved,
40 kwamba kila mwaka binti wa Israeli huenda kwa siku nne ili kumkumbuka huyo binti wa Yefta, Mgileadi.
such that, after each year passes, the daughters of Israel convene as one, and they lament the daughter of Jephthah, the Gileadite, for four days.