< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
Torej po Józuetovi smrti se je pripetilo, da so Izraelovi otroci vprašali Gospoda, rekoč: »Kdo bo za nas najprej šel gor zoper Kánaance, da se bori zoper njih?«
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
Gospod je rekel: »Juda bo šel gor. Glejte, deželo sem izročil v njegovo roko.«
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
Juda je svojemu bratu Simeonu rekel: »Pridi gor z menoj v moj žreb, da se bova lahko borila zoper Kánaance in prav tako bom tudi jaz šel s teboj v tvoj žreb.« Tako je Simeon odšel z njim.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
Juda je odšel gor in Gospod je Kánaance in Perizéjce izročil v njuno roko in izmed njih sta v Bezeku usmrtila deset tisoč mož.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
V Bezeku sta našla Adoní Bezeka in se borila zoper njega ter usmrtila Kánaance in Perizéjce.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
Toda Adoní Bezek je pobegnil in sledila sta za njim, ga ujela ter odsekala njegova palca in velika prsta na njegovih stopalih.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Adoní Bezek je rekel: »Sedemdeset kraljev, ki imajo odsekane svoje palce in svoje palce na stopalih, je svojo hrano pobiralo pod mojo mizo. Kakor sem jaz storil, tako mi je Bog poplačal.« In odvedla sta ga v Jeruzalem in tam je umrl.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
Torej Judovi otroci so se borili zoper Jeruzalem, ga zavzeli, udarili z ostrino meča in zažgali mesto.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
Potem so Judovi otroci odšli dol, da se borijo zoper Kánaance, ki prebivajo na gori, na jugu in v dolini.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Juda je odšel zoper Kánaance, ki prebivajo v Hebrónu (torej ime Hebróna je bilo prej Kirját Arba) in usmrtili so Šešája, Ahimána in Talmája.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
Od tam je odšel zoper prebivalce Debírja. Ime Debírja pa je bilo prej Kirját Sefer.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Kaléb je rekel: »Kdor udari Kirját Sefer in ga zavzame, njemu bom dal svojo hčer Ahso za ženo.«
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Zavzel ga je Kenázov sin Otniél, Kalébov mlajši brat in dal mu je svojo hčer Ahso za ženo.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Ko je prišla k njemu se je pripetilo, da ga je primorala, da prosi od svojega očeta polje in razjahala je svojega osla in Kaléb ji je rekel: »Kaj hočeš?«
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
Rekla mu je: »Daj mi blagoslov, kajti dal si mi južno deželo; daj mi tudi vodne izvire.« In Kaléb ji je dal gornje izvire in spodnje izvire.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
Otroci Kenéjca, Mojzesovega tasta, so z Judovimi otroki odšli gor iz mesta palmovih dreves v Judovo divjino, ki leži na jugu Aráda in odšli so ter prebivali med ljudstvom.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
Juda je odšel s svojim bratom Simeonom in usmrtili so Kánaance, ki naseljujejo Cefát in ga popolnoma uničili. Ime mesta se je imenovalo Horma.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
Juda je zavzel tudi Gazo z njenimi pokrajinami, Aškelón z njegovimi pokrajinami in Ekrón z njegovimi pokrajinami.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
Gospod je bil z Judom in napodil je prebivalce gore, toda ni mogel napoditi prebivalcev doline, ker so imeli železne vozove.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
Hebrón so dali Kalébu, kakor je rekel Mojzes, in od tam je izgnal tri Anákove sinove.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
Benjaminovi otroci pa niso napodili Jebusejcev, ki so naseljevali Jeruzalem, temveč Jebusejci prebivajo z Benjaminovimi otroki v Jeruzalemu do današnjega dne.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
Jožefova hiša, tudi oni so se dvignili zoper Betel in Gospod je bil z njimi.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
Jožefova hiša je poslala, da razišče Betel. (Torej ime mesta je bilo prej Luz.)
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
Ogledniki so videli moža priti iz mesta in mu rekli: »Pokaži nam, prosimo te, vhod v mesto, mi pa ti bomo izkazali usmiljenje.«
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
Ko jim je ta pokazal vhod v mesto, potem so mesto udarili z ostrino meča, toda spustili so moža in vso njegovo družino.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
Mož je odšel v deželo Hetejcev, zgradil mesto in njegovo ime imenoval Luz, kar je njegovo ime do današnjega dne.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
Niti Manáse ni napodil prebivalcev Bet Šeána in njegovih mest, niti Taanáha in njegovih mest, niti prebivalcev Dora in njegovih mest, niti prebivalcev Jibleáma in njegovih mest, niti prebivalcev Megída in njenih mest, temveč so Kánaanci hoteli prebivati v tej deželi.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
Pripetilo se je, ko je bil Izrael močan, da so Kánaance podvrgli davku, niso pa jih popolnoma pognali ven.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Niti ni Efrájim napodil Kánaancev, ki prebivajo v Gezerju, temveč Kánaanci prebivajo med njimi v Gezerju.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Niti ni Zábulon napodil prebivalcev Kitróna niti prebivalcev Nahalóla, temveč so Kánaanci prebivali med njimi in postali so davkoplačevalci.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Niti ni Aser napodil prebivalcev Aka, niti prebivalcev Sidóna, niti Ahalaba, niti Ahzíba, niti Helbe, niti Aféke, niti Rehóba,
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
temveč so Aserjevci prebivali med Kánaanci, prebivalci dežele, kajti niso jih pognali ven.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Niti ni Neftáli napodil prebivalcev Bet Šemeša niti prebivalcev Bet Anáta, temveč je prebival med Kánaanci, prebivalci dežele. Kljub temu so jim prebivalci Bet Šemeša in Bet Anáta postali davkoplačevalci.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
Amoréjci pa so Danove otroke potisnili na goro, kajti niso jim hoteli pustiti, da pridejo dol k dolini,
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
temveč so Amoréjci hoteli prebivati na gori Heres v Ajalónu in v Šaalbímu. Vendar je roka Jožefove hiše prevladala, tako da so postali davkoplačevalci.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
Pokrajina Amoréjcev je bila od vzpona k Akrabímu, od skale in navzgor.

< Waamuzi 1 >