< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
پس از مرگ یوشع، بنی‌اسرائیل از خداوند سؤال کردند: «خداوندا، کدام یک از قبیله‌های ما اول باید به جنگ کنعانی‌ها برود؟»
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
خداوند به ایشان فرمود: «قبیلهٔ یهودا برود. من زمین کنعانی‌ها را به تصرف آنها در خواهم آورد.»
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
رهبران قبیلهٔ یهودا از قبیلهٔ شمعون خواستند تا ایشان را در این جنگ یاری نمایند، و به ایشان گفتند: «کمک کنید تا کنعانی‌ها را از سرزمینی که به قبیلهٔ ما تعلق دارد، بیرون کنیم. ما نیز به شما کمک خواهیم کرد تا زمین خود را تصاحب نمایید.» پس قبیلهٔ شمعون همراه قبیلهٔ یهودا عازم جنگ شدند.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
خداوند ایشان را در شکست دادن کنعانی‌ها و فرزی‌ها کمک کرد به طوری که ده هزار تن از دشمنان را در بازق کشتند. پادشاه آنها، ادونی بازق گریخت ولی طولی نکشید که اسرائیلی‌ها او را دستگیر نموده، شستهای دست و پای او را بریدند.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
ادونی بازق گفت: «هفتاد پادشاه با دست و پای شست بریده از خرده نانهای سفرهٔ من می‌خوردند. اکنون خدا مرا به سزای اعمالم رسانیده است.» ادونی بازق را به اورشلیم بردند و او در آنجا مرد.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
قبیلهٔ یهودا شهر اورشلیم را گرفته، اهالی آنجا را قتل عام نمودند و شهر را به آتش کشیدند.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
بعد از آن، آنها با کنعانی‌هایی که در نواحی کوهستانی و صحرای نِگِب و کوهپایه‌های غربی ساکن بودند وارد جنگ شدند.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
آنگاه قبیلهٔ یهودا بر کنعانی‌های ساکن حبرون (که قبلاً قریهٔ اربع نامیده می‌شد) حمله بردند و طایفه‌های شیشای، اخیمان و تلمای را شکست دادند.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
سپس به شهر دبیر (که قبلاً به قریهٔ سفر معروف بود) هجوم بردند.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
کالیب به افراد خود گفت: «هر که برود و قریۀ سفر را تصرف نماید، دخترم عکسه را به او به زنی خواهم داد.»
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
عتن‌ئیل، پسر قناز (قناز برادر کوچک کالیب بود) شهر را تصرف نمود و کالیب عکسه را به او به زنی داد.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
عتن‌ئیل وقتی عکسه را به خانهٔ خود می‌برد، او را ترغیب نمود تا از پدرش قطعه زمینی بخواهد. عکسه از الاغش پیاده شد تا در این باره با پدرش کالیب صحبت کند. کالیب از او پرسید: «چه می‌خواهی؟»
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
عکسه گفت: «یک هدیهٔ دیگر هم به من بده! آن زمینی که در نِگِب به من داده‌ای، زمین بی‌آبی است. یک قطعه زمین که چشمه در آن باشد به من بده.» پس کالیب چشمه‌های بالا و پایین را به او بخشید.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
وقتی که قبیلهٔ یهودا به ملک تازهٔ خود واقع در بیابان نگب، نزدیک عراد، وارد شدند، قبیلهٔ قینی (از نسل پدرزن موسی) نیز به آنها پیوستند. آنها خانه‌های خود را در اریحا (معروف به شهر نخلستان) ترک نموده، از آن پس در میان قبیلهٔ یهودا ساکن شدند.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
آنگاه قبیلهٔ یهودا همراه قبیلهٔ شمعون، کنعانی‌هایی را که در شهر صَفَت زندگی می‌کردند شکست دادند و شهرشان را به کلی نابود کرده، آن را حُرما نامیدند.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
همچنین قبیلهٔ یهودا شهرهای غزه، اشقلون، عقرون و روستاهای اطراف آنها را فتح کردند.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
خداوند به قبیلهٔ یهودا یاری نمود تا نواحی کوهستانی را تصرف کنند؛ اما موفق نشدند ساکنان دشتها را بیرون رانند، چون ساکنان آنجا دارای ارابه‌های آهنین بودند.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
همان‌طور که موسی قول داده بود شهر حبرون به کالیب داده شد و کالیب اهالی این شهر را که از نسل سه پسر عناق بودند، بیرون راند.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
قبیلهٔ بنیامین، یبوسی‌هایی را که در اورشلیم سکونت داشتند بیرون نکردند بنابراین آنها تا به امروز در آنجا در میان قبیلهٔ بنیامین زندگی می‌کنند.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
خداوند با قبیلهٔ یوسف بود، و آنها توانستند بیت‌ئیل را (که قبلاً لوز نامیده می‌شد) تصرف کنند. آنها نخست جاسوسانی به شهر فرستادند.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
آن جاسوسان مردی را که از شهر بیرون می‌آمد گرفتند و به او گفتند که اگر به آنها راه نفوذ به شهر را نشان دهد جان او و خانواده‌اش در امان خواهد بود.
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
او راه نفوذ به شهر را به آنها نشان داد. پس وارد شده، اهالی شهر را قتل عام نمودند، ولی آن مرد و خانواده‌اش را نکشتند.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
بعد این مرد به سرزمین حیتی‌ها رفت و در آنجا شهری بنا کرد و آن را لوز نامید که تا به امروز به همان نام باقی است.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
قبیلهٔ منسی نتوانستند ساکنان شهرهای بیت‌شان، تعنک، دُر، یبلعام، مجدو و اهالی روستاهای اطراف آنها را بیرون کنند. پس کنعانی‌ها همچنان در آنجا ماندند.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
وقتی اسرائیلی‌ها نیرومندتر شدند، کنعانی‌ها را مثل برده به کار گرفتند ولی آنها را به کلی از آن سرزمین بیرون نکردند.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
قبیلهٔ افرایم نیز کنعانی‌های ساکن جازر را بیرون نکردند و آنها هنوز هم در میان قبیلهٔ افرایم زندگی می‌کنند.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
قبیلهٔ زبولون نیز اهالی فطرون و نهلول را بیرون نراندند، پس این کنعانی‌ها در میان قبیلهٔ زبولون باقی ماندند و به صورت برده به کار گرفته شدند.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
همچنین قبیلهٔ اشیر، ساکنان عکو، صیدون، احلب، اکزیب، حلبه، عفیق و رحوب را بیرون نراندند. بنابراین قبیلهٔ اشیر در میان کنعانی‌های آن سرزمین زندگی می‌کنند.
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
قبیلهٔ نفتالی هم ساکنان بیت‌شمس و بیت‌عنات را بیرون نکردند، بنابراین ایشان مثل برده در میان این قبیله به زندگی خود ادامه می‌دهند.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
اما قبیلهٔ دان توسط اموری‌ها به کوهستان رانده شدند و نتوانستند از آنجا پایین بیایند و در دشت ساکن شوند.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
اموری‌ها قصد داشتند، اَیَلون، شَعَلُبیم و کوه حارس را تصرف کنند ولی قبیلهٔ یوسف آنها را مغلوب ساخته، به بردگی گرفتند.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
سرحد اموری‌ها از گردنهٔ عقربها شروع شده، به سالع می‌رسید و از آنجا نیز فراتر می‌رفت.

< Waamuzi 1 >