< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
Et après la mort de Josué les enfants d'Israël consultèrent l'Éternel en disant: Lequel d'entre nous doit marcher le premier contre les Cananéens pour les attaquer?
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
Et l'Éternel dit: Juda marchera. Voici, j'ai livré le pays entre ses mains.
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
Et Juda dit à Siméon, son frère: Accompagne-moi pour une expédition dans mon lot, et attaquons les Cananéens; à mon tour je t'accompagnerai pour une expédition dans ton lot. Alors Siméon se mit en campagne avec lui.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
Et Juda s'avança, et l'Éternel livra entre leurs mains les Cananéens et les Perizzites, et ils les défirent à Bézek au nombre de dix mille hommes.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
Et ils trouvèrent Adoni-Bézek à Bézek, et l'ayant attaqué ils battirent les Cananéens et les Perizzites.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
Et Adoni-Bézek s'enfuit et ils le poursuivirent et le prirent, et ils lui coupèrent les pouces aux mains et aux pieds.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Alors Adoni-Bézek dit: Soixante-dix Rois ayant les pouces coupés aux mains et aux pieds en étaient à ramasser sous ma table: ce que j'ai fait, Dieu me le rend. Et ils l'emmenèrent à Jérusalem, et il mourut là.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
Et les enfants de Juda attaquèrent Jérusalem, et la prirent, et la frappèrent avec le tranchant de l'épée et livrèrent la ville aux flammes.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
Ensuite les fils de Juda descendirent pour attaquer les Cananéens habitant la Montagne et le Midi et le Pays-bas.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Et Juda marcha contre les Cananéens établis à Hébron (or le nom de Hébron était jadis Ville d'Arba), et ils défirent Sesaï et Ahiman et Thalmaï.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
Et de là ils marchèrent contre les habitants de Debir; or le nom de Debir était jadis Kiriath-Sépher.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Et Caleb dit: A celui qui réduira et prendra Kiriath-Sépher, je donnerai pour femme Achsa ma fille.
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Et Othniel, fils de Kénaz, frère cadet de Caleb, la prit; et il lui donna pour femme sa fille Achsa.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Et à son entrée chez lui elle l'incita à demander un champ à son père; et de dessus l'âne qu'elle montait, elle mit pied à terre. Alors Caleb lui dit: Qu'as-tu à dire?
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
Et elle lui dit: Accorde-moi un bienfait! puisque tu m'as donné une terre du midi, donne-moi aussi des sources d'eau. Alors Caleb lui donna les sources supérieures et les sources inférieures.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
Et les fils de Kéni, beau-père de Moïse, firent depuis la Ville des Palmiers avec les fils de Juda une campagne dans le désert de Juda situé au midi d'Arad, et ils allèrent s'établir avec le peuple.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
Et Juda se mit en marche avec Siméon, son frère, et ils défirent les Cananéens qui habitaient Tséphath, et ils la dévouèrent, et donnèrent à la ville le nom de Horma (anathème).
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
Et Juda prit Gaza et son territoire, et Askalon et son territoire, et Ekron et son territoire.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
Et l'Éternel fut avec Juda de sorte qu'il se rendit maître de la montagne, car il ne put expulser les habitants de la plaine qui avaient des chars ferrés.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
Et ils donnèrent Hébron à Caleb, d'après ce que Moïse avait dit, et il en chassa les trois fils de Anak.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
Et les fils de Benjamin n'expulsèrent point les Jébusites établis à Jérusalem; et les Jébusites ont habité Jérusalem avec les fils de Benjamin jusqu'aujourd'hui.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
Et la maison de Joseph aussi fit sa campagne contre Béthel, et l'Éternel fut avec eux.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
Et la maison de Joseph fit faire une reconnaissance à Béthel (or le nom de la ville était jadis Luz).
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
Et les vedettes aperçurent un homme qui sortait de la ville, et lui dirent: Indique-nous l'accès de la ville et nous te montrerons de la bonté.
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
Et il leur indiqua l'accès de la ville. Et ils frappèrent la ville avec le tranchant de l'épée; mais ils laissèrent échapper cet homme et toute sa famille.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
Et cet homme passa dans le pays des Héthiens et bâtit une ville qu'il appela du nom de Luz; tel a été son nom jusqu'aujourd'hui.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
Et Manassé ne déposséda point Beth-Séan et ses annexes, ni Thaanach et ses annexes, ni Dor et ses annexes, ni Jibléam et ses annexes, ni Megiddo et ses annexes, et les Cananéens persistèrent à se maintenir dans cette contrée.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
Et lorsque Israël se fut consolidé, il soumit les Cananéens à la corvée, mais quant à les chasser, il ne le fit pas.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Et Ephraïm n'expulsa point les Cananéens établis à Gézer, les Cananéens demeurèrent donc parmi eux à Gézer.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Zabulon n'expulsa point les habitants de Kitron, ni les habitants de Nahalol; les Cananéens demeurèrent donc parmi eux, mais ils devinrent corvéables.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Asser n'expulsa point les habitants de Acco, ni les habitants de Sidon et d'Ahelab et d'Achsib et de Helba et d'Aphik et de Rehob;
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
et ainsi les Assérites demeurèrent au milieu des Cananéens, habitants du pays, car ils ne les expulsèrent pas.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Nephthali n'expulsa point les habitants de Beth-Semès, ni les habitants de Beth-Anath, et il demeura au milieu des Cananéens, habitants du pays. Mais les habitants de Beth-Semès et de Beth-Anath furent soumis par lui à la corvée.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
Et les Amoréens repoussèrent les Danites dans la montagne, car ils ne leur permirent pas de descendre dans la vallée.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
Et les Amoréens persistèrent à habiter Har-Herès, Ajalon et Saalbim; mais ils sentirent le poids de la main de la maison de Joseph et devinrent corvéables.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
Et le territoire des Amoréens s'étendait de la hauteur des Scorpions, de Séla en haut.

< Waamuzi 1 >