< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
Efter Josuas Død adspurgte Israelitterne HERREN og sagde: "Hvem af os skal først drage op til Kamp mod Kana'anæerne?"
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
HERREN svarede: "Det skal Juda; se, jeg giver Landet i hans Hånd!"
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
Juda sagde da til sin Broder Simeon: "Drag op med mig i min Lod og lad os sammen kæmpe med Kana'anæerne, så skal jeg også drage med dig ind i din Lod!" Så gik da Simeon med ham.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
Juda drog nu op, og HERREN gav Kana'anæerne og Perizziterne i deres Hånd, så de slog dem i Bezek, 10000 Mand.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
Og da de stødte på Adonibezek i Bezek, angreb de ham og slog Kana'anæerne og Perizziterne.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
Adonibezek flygtede, men de satte efter ham, og da de havde grebet ham, huggede de Tommelfingrene og Tommeltæerne af ham.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Da sagde Adonibezek: "Halvfjerdsindstyve Konger med afhugne Tommelfingre og Tommeltæer havde jeg stadig til at sanke Smuler under mit Bord; hvad jeg har gjort, gengælder Gud mig!" Derpå førte man ham til Jerusalem, og der døde han.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
Og Judæerne angreb og indtog Jerusalem, huggede Indbyggerne ned og stak Ild på Byen.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
Senere drog Judæerne ned til Kamp mod Kana'anæerne i Bjergene, i Sydlandet og i Lavlandet.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Og Juda drog mod Kana'anæerne i Hebron - Hebron hed fordum Kirjat Arba og slog Sjesjaj, Ahiman og Talmaj.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
Derfra drog han op mod Indbyggerne i Debir, der fordum hed Kirjaf-Sefer.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Da sagde Kaleb: "Den, som slår Kirjat Sefer og indtager det, ham giver jeg min Datter Aksa til Hustru!"
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Og da Kenizziten Otniel, Kalebs yngre Broder, indtog det, gav han ham sin Datter Aksa til Hustru.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Men da hun kom til ham, æggede han hende til at bede sin Fader om Agerland. Hun sprang da ned af Æselet, og Kaleb spurgte hende: "Hvad vil du?"
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
Hun svarede: "Giv mig en Velsignelse! Siden du har bortgiftet mig i det tørre Sydland, må du give mig Vandkilder!" Da gav Kaleb hende de øvre og de nedre Vandkilder.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
Moses's Svigerfaders, Keniten Kobabs, Sønner, drog sammen med Judæerne op fra Palmestaden til Arads Ørken og bosatte sig hos Amalekiterne.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
Juda drog derpå ud med sin Broder Simeon, og de slog Kana'anæerne, som boede i Zefat, og lagde Band på Byen; derfor blev den kaldt Horma.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
Og Juda indtog Gaza med dets Område, Askalon med dets Område og Ekron med dets Område.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
Og HERREN var med Juda, så han tog Bjerglandet i Besiddelse; Lavlandets Indbyggere kunde han nemlig ikke drive bort, fordi de havde Jernvogne.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
Haleb gav de Hebron, som Moses havde sagt. Og han drev de tre Anaksønner bort derfra.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
Men Jebusiterne, som boede i Jerusalem, fik Judæerne ikke drevet bort, og Jebusiterne bor den Dag i Dag i Jerusalem sammen med Judæerne.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
Men også Josefs Hus drog op og gik mod Betel; og HERREN var med dem.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
Da Josefs Hus udspejdede Betel Byen hed fordum Luz
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
fik Spejderne Øje på en Mand, der gik ud af Byen; og de sagde til ham: "Vis os, hvor vi kan komme ind i Byen, så vil vi skåne dig!"
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
Da viste han dem, hvor de kunde komme ind i Byen. Derpå huggede de dens Indbyggere ned, men Manden og hele hans. Slægt lod de drage bort,
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
og Manden begav sig til Hetiternes Land og byggede en By, som han kaldte Luz; og det hedder den endnu den Dag i Dag.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
Men Indbyggerne i Bet-Sjean og dets Småbyer og i Ta'anak og dets Småbyer, Indbyggerne i Dor og dets Småbyer, i Jibleam og dets Småbyer og i Megiddo og dets Småbyer fik Manasse ikke drevet bort; det lykkedes Kana'anæerne at blive boende i disse Egne.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
Da Israelitterne blev de stærkeste, gjorde de Kana'anæerne til Hoveriarbejdere, men drev dem ikke bort.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Efraim fik ikke Kana'anæerne, som boede i Gezer, drevet bort; men Kana'anæerne blev boende midt iblandt dem i Gezer.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Zebulon fik ikke Indbyggerne i Kitron og Nahalol drevet bort; men Kana'anæerne blev boende midt iblandt dem og blev Hoveriarbejdere.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Aser fik ikke Indbyggerne i Akko drevet bort, ej heller Indbyggerne i Zidon, Mahalab, Akzib, Afik og Rehob.
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
Men Aseriterne bosatte sig midt iblandt Kana'anæerne, der boede i Landet, thi de magtede ikke at drive dem bort.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Naftali fik ikke Indbyggerne i Bet Sjemesj og Bet-Anat drevet bort, men bosatte sig midt iblandt Kana'anæerne, der boede i Landet: Men Indbyggerne i Bet Sjemesj og Bet Anat blev deres Hoveriarbejdere.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
Amoriterne trængte Daniterne op i Bjergene og lod dem ikke komme ned i Lavlandet;
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
og det lykkedes Amoriterne at blive boende i Har-Heres, Ajjalon og Sja'albim. Men senere, da Josefs Hus fik Overtaget, blev de Hoveriarbejdere.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
Edomiternes Landemærke strakte sig fra Akrabbimpasset til Sela og højere op.

< Waamuzi 1 >