< Yuda 1 >

1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
Jude a servant of Jesus Christ, and brother of James, to them that are sanctified in God the Father, and who are preserved and called in Jesus Christ;
2 Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
mercy, and peace, and love be multiplied unto you.
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Beloved, having an earnest desire to write to you concerning the common salvation, I was under a necessity of writing to exhort you that ye would strive earnestly for the faith which was once delivered to the saints.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
For there have crept in some men, who have been of old described as under this condemnation, impious people, that turn the grace of our God into lasciviousness, and deny God the only Lord, and our Lord Jesus Christ.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
But I would remind you of this, which ye know already, that though the Lord saved the people out of the land of Egypt, yet He afterwards destroyed those that believed not:
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios g126)
and the angels that kept not their primitive state, but left their proper abode, hath He reserved in everlasting chains, under darkness, to the judgement of the great day: (aïdios g126)
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
as Sodom and Gomorrha, and the cities about them, in like manner with them committing lewdness, and going after strange flesh, are set forth as an example, suffering the vengeance of perpetual fire. (aiōnios g166)
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
So these vile dreamers also defile the flesh, despise authority, and speak evil of dignities.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
Whereas Michael the archangel, when contending with the devil he disputed about the body of Moses, did not presume to bring against him a railing accusation, but said, "The Lord rebuke thee."
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
But these men speak evil of what they know not: and what they know naturally, as brute animals, in these things they are corrupt.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
Wo unto them; for they have gone in the way of Cain, and been carried away by Balaam's error, the love of lucre, and perished as in the contradiction of Korah.
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
These are spots in your love-feasts, feeding themselves without fear, when they are feasting with you: clouds without water, carried about by the winds; trees withered and without fruit, twice dead and rooted up; raging waves of the sea, foaming out their own shame;
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn g165)
wandering stars, for whom blackness of darkness is reserved for ever. (aiōn g165)
14 Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
And Enoch the seventh from Adam prophesied against these, saying, Behold the Lord cometh with his holy myriads,
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
to pass judgement upon all, and to convict all the ungodly among them of all their wicked works, which they have impiously committed, and of all the hard things which impious sinners have spoken against Him.
16 Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
These are murmurers, complainers, who walk according to their own irregular desires; and their mouth speaketh great swelling words, with admiration of certain persons for some advantage of their own.
17 Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
But, beloved, remember the words which were formerly spoken by the apostles of our Lord Jesus Christ; for they told you,
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
that in the latter days there will be scoffers, walking according to their own impious lusts.
19 Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
These are they who separate themselves, sensualists, not having the Spirit.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
But ye, beloved, edifying yourselves in your most holy faith, and praying in the holy Spirit, keep yourselves in the love of God,
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios g166)
looking for the mercy of our Lord Jesus Christ unto eternal life. (aiōnios g166)
22 Wahurumieni walio na mashaka;
And on some have compassion, making a difference; others save with fear,
23 wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
as snatching them out of the fire: hating even the garment spotted by the flesh.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
Now unto Him that is able to keep you from falling, and to present you blameless before the presence of his glory with exceeding joy:
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn g165)
to the only wise God our Saviour be glory and majesty, dominion and power, both now and for ever. Amen. (aiōn g165)

< Yuda 1 >