< Yuda 1 >
1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
Juda, služabnik Jezusa Kristusa in Jakobov brat, tem, ki so posvečeni po Bogu Očetu in ohranjeni v Jezusu Kristusu in poklicani:
2 Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
›Usmiljenje in mir in ljubezen naj se vam pomnožijo.‹
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Ljubljeni, ko sem posvetíl vso marljivost, da vam pišem o skupni rešitvi duš, je bilo zame nujno, da vam pišem in vas spodbujam, da se resno borite za vero, ki je bila enkrat [za vselej] izročena svetim.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
Kajti ne-sluteč so se prikradli določeni ljudje, ki so bili že od davno odrejeni za to obsodbo, brezbožni ljudje, ki milost našega Boga sprevračajo v opolzkost in zanikajo edinega Gospoda Boga in našega Gospoda Jezusa Kristusa.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
Hočem vas torej spomniti, čeprav ste nekoč to vedeli, da je Gospod, ki je ljudi rešil iz egiptovske dežele, potem uničil te, ki niso verovali.
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios )
In angele, ki niso obdržali svojega prvega stanja, temveč so zapustili svoje prebivališče, je ohranil v večnih verigah pod temo, do sodbe vélikega dne. (aïdios )
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios )
Celó kakor so Sódoma in Gomóra in na podoben način mesta okoli njiju, ki so same sebe predajala v prešuštvo in hodila za tujim mesom, postavljena kot zgled, trpeč maščevanje večnega ognja. (aiōnios )
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
Podobno tudi ti umazani sanjači omadežujejo meso, prezirajo gospostvo in hudobno govorijo o dostojanstvih.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
Vendarle si nadangel Mihael, ko se je pričkal s hudičem in prerekal glede Mojzesovega telesa, ni drznil zoper njega udrihati obtožbe, temveč je rekel: »Gospod te ošteje.«
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
Toda ti govorijo hudobno o teh stvareh, ki jih ne poznajo; toda kar naravno vedo kot brezčutne živali, v teh stvareh sami sebe kvarijo.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
Gorje jim! Kajti odšli so na Kajnovo pot in lakomno tekli za Bileámovo zmoto po nagrado in propadli v Korahovem uporu.
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
Ti so madeži na vaših dobrodelnih pojedinah, ko se zabavajo z vami in se hranijo brez strahu. Oblaki so brez vode, ki jih vetrovi nosijo okoli; drevesa, katerih sad vene, brez sadu, dvakrat mrtva, izruvana s koreninami;
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn )
besneči morski valovi, ki se penijo od svoje lastne sramote; blodeče zvezde, ki jim je za vedno prihranjena črna temà. (aiōn )
14 Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
In tudi Henoh, sedmi od Adama, je prerokoval o njih, rekoč: ›Glej, Gospod prihaja z deset tisoči svojih svetih,
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
da izvrši sodbo nad vsemi in da prepriča vse, ki so med njimi brezbožni, o vseh njihovih brezbožnih dejanjih, ki so jih brezbožno zagrešili in o vseh njihovih trdih govorih, ki so jih brezbožni grešniki govorili zoper njega.‹
16 Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
To so godrnjači, pritoževalci, ki hodijo za svojimi lastnimi poželenji; in njihova usta govorijo velike napihnjene besede, ker zaradi koristi občudujejo človeško zunanjost.
17 Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
Toda ljubljeni, spominjajte se besed, ki so vam jih prej govorili apostoli našega Gospoda Jezusa Kristusa,
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
kako so vam povedali, da bodo v poslednjem času zasmehovalci, ki naj bi hodili za svojimi lastnimi brezbožnimi poželenji.
19 Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
Ti so tisti, ki se oddvojijo, čutni, ki nimajo Duha.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
Toda vi, ljubljeni, se izgrajujte v svoji najsvetejši veri, moleč v Svetem Duhu,
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios )
ohranite se v Božji ljubezni, pričakujte usmiljenje našega Gospoda Jezusa Kristusa, za večno življenje. (aiōnios )
22 Wahurumieni walio na mashaka;
In do nekaterih imejte sočutje, s tem da delate razliko;
23 wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
druge pa rešite s strahom in jih potegnite iz ognja; in sovražite celó obleko, omadeževano z mesom.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
Torej njemu, ki vas je zmožen varovati pred padcem in vas s silno radostjo predstaviti brezhibne pred prisotnost svoje slave,
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn )
edinemu modremu Bogu, našemu Odrešeniku, bodi slava in veličanstvo, gospostvo in oblast, tako sedaj kot na veke. Amen. (aiōn )