< Yuda 1 >
1 Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo na nduguye Yakobo: Kwa wale walioitwa, wapendwa katika Mungu Baba na kuhifadhiwa salama ndani ya Yesu Kristo:
Юда, слуга Исус Христов, и брат Яковов, до призваните, възлюбени от Бога Отца и пазени в Исуса Христа:
2 Rehema, amani na upendo viwe kwenu kwa wingi.
Милост, мир и любов да ви се умножат.
3 Wapendwa, ingawa nilikuwa ninatamani sana kuwaandikia kuhusu wokovu ambao tunaushiriki sisi sote, niliona imenipasa kuwaandikia na kuwasihi kwamba mwitetee imani iliyokabidhiwa watakatifu kwa nafasi moja itoshayo.
Възлюбени, като показвах всяко усърдие да ви пиша за нашето общо спасение, счетох за нужно да ви пиша и да ви овещая да се подвизаете за вярата, която еднаж за винаги бе предадена на светиите.
4 Kwa kuwa kuna watu waliojipenyeza kwa siri katikati yenu, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, waovu, wapotoshao neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi wakimkana yeye aliye Bwana wetu wa pekee, Bwana Yesu Kristo.
Защото са се вмъкнали някои човеци, които отдавна са били посочени, че подлежат на това осъждане, нечестивци, които обръщат благодатта на нашия Бог в похотливост и се отричат от единствения Владетел и Господ наш Исус Христос.
5 Ingawa mmekwisha kujua haya yote, nataka niwakumbushe kuwa Bwana akiisha kuwaokoa watu wake kutoka nchi ya Misri, baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
А искам да ви напомня, (тъй като сте узнали вече всичко това), че Господ, като избави веднаж Своя народ от египетската земя, после погуби ония, които не повярваха,
6 Nao malaika ambao hawakulinda nafasi zao, lakini wakayaacha makao yao, hawa amewaweka katika giza, wakiwa wamefungwa kwa minyororo ya milele kwa ajili ya hukumu Siku ile kuu. (aïdios )
и че ангели, които не упазиха своето достойнство, но напуснаха собственото си жилище, - Той ги държи под мрак във вечни връзки за съда на великия ден; (aïdios )
7 Vivyo hivyo, Sodoma na Gomora na pia ile miji iliyokuwa kandokando, ambayo kwa jinsi moja na hao, walijifurahisha kwa uasherati na kufuata tamaa za mwili zisizo za asili, waliwekwa wawe mfano kwa kuadhibiwa katika moto wa milele. (aiōnios )
както и Содом, Гомор и околните им градове, които, подобно на тях, се предадоха на блудство и изпаднаха в противоестествени пороци (Гръцки: И следваха след чужда плът. Бит. 19:5), са поставени за пример, като носят наказанието на вечния огън. (aiōnios )
8 Vivyo hivyo, hawa waotao ndoto huutia mwili unajisi, hukataa kuwa chini ya mamlaka na kunena mabaya juu ya wenye mamlaka.
При все това, по същия начин и тия с бълнуванията си оскверняват плътта, презират властта и хулят славните същества.
9 Lakini hata malaika mkuu Mikaeli alipokuwa anashindana na ibilisi juu ya mwili wa Mose, hakuthubutu kumlaumu, bali alimwambia, “Bwana na akukemee!”
Но архангел Михаил, когото в борба с дявола се препираше за Моисеевото тяло, не смея да произнесе против него хулителна присъда, но рече: Господ да те смъмри.
10 Lakini watu hawa hunena mabaya dhidi ya mambo wasiyoyafahamu. Na katika mambo yale wanayoyafahamu kwa hisia kama wanyama wasio na akili, hayo ndiyo hasa yanayowaharibu.
Тия, обаче, хулят всичко, което не знаят; а което знаят естествено, както животните без разум, в това развращават себе си.
11 Ole wao! Kwa kuwa wanaifuata njia ya Kaini, wamekimbilia faida katika kosa la Balaamu na kuangamia katika uasi wa Kora.
Горко им! защото ходят по Каиновия път, заради печалба се впускат във Валаамовата заблуда, и погиват в Кореевото упорство.
12 Watu hawa ni dosari katika karamu zenu za upendo, wakila pamoja nanyi bila hofu, wakijilisha pasipo hofu. Wao ni mawingu yasiyokuwa na maji, yakichukuliwa na upepo, miti isiyo na matunda wakati wa mapukutiko, ambayo hunyauka, iliyokufa mara mbili na kungʼolewa kabisa.
Тия са подводни скали, когато пируват с вас в дружелюбните ви гощавки, и без страх напасват себе си; безводни облаци, носени от ветровете; есенни дървета, безплодни, дваж умрели, изкоренени;
13 Wao ni mawimbi makali ya bahari, yakitoa povu la aibu yao wenyewe, ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba waliowekewa milele. (aiōn )
свирепи морски вълни; които изпущат като пяна своите безсрамни дела; скитащи звезди, за които се пази мрачна тъмнина до века. (aiōn )
14 Enoki, mtu wa saba kuanzia Adamu alitoa unabii kuhusu watu hawa, akisema: “Tazama, Bwana anakuja pamoja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
За тях пророкува и Енох, седмият от Адама, като рече: Ето Господ иде с десетки хиляди Свои светии,
15 ili kumhukumu kila mmoja na kuwapatiliza wote wasiomcha Mungu kwa matendo yao yote ya uasi waliyoyatenda, pamoja na maneno yote ya kuchukiza ambayo wenye dhambi wamesema dhidi yake.”
да извърши съдба на всички, и да обяви за виновни всичките нечестиви дела, които в нечестие са сторили, и за всичките жестоки думи, които нечестивите грешници са говорили против Него.
16 Watu hawa ni wenye kunungʼunika na wenye kutafuta makosa; wao hufuata tamaa zao mbaya, hujisifu kwa maneno makuu kuhusu wao wenyewe na kuwasifu mno watu wenye vyeo kwa ajili ya kujipatia faida.
Тия са роптатели, оплаквачи, които ходят по страстите си, (и устата им говорят надуто), и заради печалба ласкаят човеците.
17 Lakini ninyi wapenzi, kumbukeni yale mitume wa Bwana Yesu Kristo waliyonena zamani.
Но, вие, възлюбени, помнете думите изговорени по-напред от апостолите на нашия Господ Исус Христос, как ви казваха:
18 Kwa kuwa waliwaambia, “Siku za mwisho kutakuwa na watu wenye kudhihaki, watakaofuata tamaa zao wenyewe za upotovu.”
В последно време ще има присмивачи, които ще ходят по своите нечестиви страсти.
19 Hawa ndio watu wanaowagawa ninyi, wafuatao tamaa zao za asili, wala hawana Roho.
Тия са, които правят разцепления, плътски, които нямат Духа.
20 Lakini ninyi wapendwa, jijengeni katika imani yenu iliyo takatifu sana tena ombeni katika Roho Mtakatifu.
А вие възлюбени, като назидавате себе си в нашата пресвята вяра и се молите на Святия Дух,
21 Jilindeni katika upendo wa Mungu mkitazamia kwa furaha rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ili awalete katika uzima wa milele. (aiōnios )
пазете себе си в Божията любов, ожидайки милостта на нашия Господ Исус Христос за вечен живот. (aiōnios )
22 Wahurumieni walio na mashaka;
И към едни, които са в съмнение, бивайте милостиви;
23 wengine waokoeni kwa kuwanyakua kutoka kwenye moto; nao wengine wahurumieni mkiwa na hofu, mkichukia hata vazi lenye mawaa na kutiwa unajisi na mwili.
други спасявайте, като ги изтръгвате из огъня; а към други показвайте милост, със страх, като се гнусите даже и от осквернената от плътта дреха.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda ninyi msianguke na kuwaleta mbele za utukufu wake mkuu bila dosari na kwa furaha ipitayo kiasi:
А на Онзи, Който може да ви предпази от препъване, и да ви постави непорочни в радост пред Своята слава,
25 kwake yeye Mungu pekee Mwokozi wetu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu, ukuu, uweza na mamlaka ni vyake tangu milele, sasa na hata milele! Amen. (aiōn )
на единствения Бог наш Спасител, чрез Исуса Христа нашия Господ, да бъде слава и величие, и преди всичките векове, и сега, и до всичките векове. Амин. (aiōn )