< Yoshua 1 >

1 Baada ya kifo cha Mose mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Mose:
And after the death of Moses, the servant of the Lord, it happened that the Lord spoke to Joshua, the son of Nun, the minister of Moses, and he said to him:
2 “Mtumishi wangu Mose amekufa. Sasa basi, wewe pamoja na watu wote hawa, jiandaeni kuvuka huu Mto Yordani kuingia nchi ambayo karibu nitawapa wana wa Israeli.
“Moses, my servant, has died. Rise up, and cross this Jordan, you and all the people with you, into the land which I will give to the sons of Israel.
3 Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga nimewapa, kama vile nilivyomwahidi Mose.
I will deliver to you every place that the step of your foot will tread upon, just as I said to Moses.
4 Nchi yenu itaenea kuanzia jangwa hili hadi Lebanoni, tena kuanzia mto mkubwa wa Frati, yaani nchi yote ya Wahiti, hadi Bahari ile Kubwa iliyoko upande wa magharibi.
From the desert and from Lebanon, even to the great river Euphrates, all the land of the Hittites, as far as the great sea opposite the setting of the sun, shall be your border.
5 Hakuna mtu yeyote atakayeweza kushindana na wewe siku zote za maisha yako. Kama vile nilivyokuwa pamoja na Mose, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakuacha wala sitakupungukia.
No one will be able to resist you during all the days of your life. Just as I was with Moses, so will I be with you. I will not leave you, nor will I forsake you.
6 “Uwe hodari na shujaa, kwa sababu wewe ndiwe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia baba zao kuwapa.
Be strengthened and be steadfast. For you shall divide by lot, to this people, the land about which I swore to their fathers that I would deliver it to them.
7 Uwe hodari na uwe na ushujaa mwingi. Uwe na bidii kutii sheria yote aliyokupa Mose mtumishi wangu, usiiache kwa kugeuka kuelekea kuume au kushoto, ili upate kufanikiwa popote uendako.
Therefore, be strengthened and be very steadfast, so that you may observe and accomplish the entire law, which Moses, my servant, instructed to you. You may not turn aside from it to the right, nor to the left. So may you understand all that you should do.
8 Usiache Kitabu hiki cha Sheria kiondoke kinywani mwako; yatafakari maneno yake usiku na mchana, ili upate kuwa mwangalifu kufanya kila kitu sawasawa na yote yaliyoandikwa ndani yake. Ndipo utakapofanikiwa na kisha utastawi.
The book of this law shall not depart from your mouth. Instead, you shall meditate upon it, day and night, so that you may observe and do all the things that are written in it. Then you shall direct your way and understand it.
9 Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakuwa pamoja nawe kokote uendako.”
Behold, I am instructing you. Be strengthened, and be steadfast. Do not dread, and do not fear. For the Lord your God is with you in all things, wherever you may go.”
10 Ndipo Yoshua akawaagiza maafisa wa watu akisema,
And Joshua instructed the leaders of the people, saying: “Cross through the midst of the camp, and command the people, and say:
11 “Pitieni katika kambi yote mkawaambie watu, ‘Wekeni tayari mahitaji yenu. Siku tatu kuanzia sasa mtavuka hii Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa iwe yenu wenyewe.’”
‘Prepare your food supplies. For after the third day, you shall cross the Jordan, and you shall enter so as to possess the land, which the Lord your God will give to you.’”
12 Lakini kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, Yoshua akasema,
Likewise, he said to the Reubenites and to the Gadites, and to the one half tribe of Manasseh:
13 “Kumbukeni agizo lile Mose mtumishi wa Bwana alilowapa: ‘Bwana Mungu wenu anawapa ninyi raha, naye amewapa nchi hii.’
“Remember the words, which Moses, the servant of the Lord, instructed to you, saying: ‘The Lord your God has given you rest, and has given you all the land.’
14 Wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu watakaa katika nchi ile Mose aliyowapa mashariki ya Yordani, lakini mashujaa wenu wote, wakiwa wamevikwa silaha kikamilifu lazima wavuke mbele ya ndugu zenu. Imewapasa kuwasaidia ndugu zenu hadi
Your wives and sons, as well as the cattle, shall remain in the land which Moses delivered to you beyond the Jordan. But as for you, pass over with weapons, before your brothers, all you who are strong of hand, and fight on their behalf,
15 Bwana awape nao raha, kama alivyokwisha kufanya kwa ajili yenu hadi wao pia watakapokuwa wamemiliki nchi ile Bwana Mungu wenu anayowapa. Baada ya hilo, mwaweza kurudi na kukalia nchi yenu wenyewe, ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa mashariki mwa Yordani kuelekea linakochomoza jua.”
until the Lord gives rest to your brothers, just as he has given to you, and until they also possess the land, which the Lord your God will give to them. And so shall you be returned to the land of your possession. And you shall live in the land, which Moses, the servant of the Lord, gave to you beyond the Jordan, opposite the rising of the sun.”
16 Ndipo wakamjibu Yoshua, “Chochote ambacho umetuagiza tutafanya na popote utakapotutuma tutakwenda.
And they responded to Joshua, and they said: “All that you have instructed to us, we shall do. And wherever you will send us, we shall go.
17 Kama vile tulivyomtii Mose kikamilifu, ndivyo tutakavyokutii wewe. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama vile alivyokuwa pamoja na Mose.
Just as we obeyed Moses in all things, so shall we obey you also. But may the Lord your God be with you, just as he was with Moses.
18 Yeyote atakayeasi neno lako na kuacha kuyatii maneno yako, au chochote utakachowaamuru, atauawa. Uwe imara na hodari tu!”
Whoever will contradict your mouth, and whoever will not obey all of your words, which you will instruct to him, let him die. But may you be strengthened, and may you act manfully.”

< Yoshua 1 >