< Yoshua 9 >
1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
A gdy usłyszeli o tym wszyscy królowie, którzy byli po tej stronie Jordanu w górach, na równinach i nad całym brzegiem Morza Wielkiego aż po Liban: Chetyci, Amoryci, Kananejczycy, Peryzzyci, Chiwwici i Jebusyci:
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
Zebrali się razem, aby jednomyślnie walczyć przeciw Jozuemu i Izraelowi.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
Lecz mieszkańcy Gibeonu, gdy usłyszeli o tym, co Jozue uczynił z Jerychem i Aj;
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
Użyli podstępu i wyruszyli, udając posłów, i wzięli stare wory na swoje osły i stare, popękane i połatane bukłaki na wino;
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
I stare, i połatane obuwie na nogi, stare szaty na siebie, a cały chleb, który ze sobą zabrali w drogę, był suchy i spleśniały.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
Wtedy przybyli do Jozuego, do obozu w Gilgal, i powiedzieli do niego i do mężczyzn Izraela: Przyszliśmy z dalekiego kraju. Zawrzyjcie więc teraz przymierze z nami.
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
Lecz mężczyźni Izraela odpowiedzieli Chiwwitom: A może mieszkacie wśród nas, jakże więc możemy zawrzeć z wami przymierze?
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
A oni powiedzieli Jozuemu: Jesteśmy twoimi sługami. I Jozue zapytał ich: Kim jesteście i skąd przybywacie?
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
Odpowiedzieli mu: Twoi słudzy przybyli z bardzo dalekiego kraju ze względu na imię PANA, twego Boga. Usłyszeliśmy bowiem o jego sławie oraz o wszystkim, co uczynił w Egipcie;
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
I o wszystkim, co uczynił dwom królom amoryckim, którzy byli za Jordanem, Sichonowi, królowi Cheszbonu, i Ogowi, królowi Baszanu, który [był] w Asztarot.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
I nasi starsi i wszyscy mieszkańcy naszego kraju nakazali nam: Weźcie ze sobą żywność na drogę, wyjdźcie im naprzeciw i powiedzcie im: Jesteśmy waszymi sługami, zawrzyjcie więc teraz przymierze z nami.
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
Ten nasz chleb był jeszcze ciepły, gdy wzięliśmy go z naszych domów w dniu, kiedy wyruszyliśmy do was; a teraz jest suchy i spleśniały.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
I te bukłaki na wino, które napełniliśmy, były nowe, a oto popękały. Także nasze szaty i obuwie zniszczyły się z powodu bardzo długiej podróży.
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
A mężczyźni [Izraela] wzięli z ich żywności, lecz nie radzili się PANA.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
Wtedy Jozue zawarł z nimi pokój i ustanowił z nimi przymierze, że zachowa ich przy życiu. Także naczelnicy zgromadzenia im przysięgli.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
Lecz po trzech dniach, po zawarciu z nimi przymierza, usłyszeli, że są oni sąsiadami i że mieszkają wśród nich.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
Wtedy synowie Izraela wyruszyli i po trzech dniach dotarli do ich miast. Miastami ich były: Gibeon, Kefira, Beerot i Kiriat-Jearim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
I nie wytracili ich synowie Izraela, gdyż naczelnicy zgromadzenia przysięgli im na PANA, Boga Izraela. I całe zgromadzenie szemrało przeciw naczelnikom.
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
I wszyscy naczelnicy powiedzieli do całego zgromadzenia: Przysięgliśmy im na PANA, Boga Izraela, dlatego teraz nie możemy ich tknąć.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
Tak więc postąpimy z nimi: zachowamy ich przy życiu, żeby nie spadł na nas gniew z powodu przysięgi, którą im złożyliśmy.
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
Ponadto naczelnicy powiedzieli im: Niech pozostaną przy życiu, ale niech rąbią drewno i noszą wodę dla całego zgromadzenia – zgodnie z tym, co obiecali naczelnicy.
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Potem Jozue wezwał ich i zapytał: Dlaczego nas oszukaliście, mówiąc: Jesteśmy z bardzo daleka, skoro mieszkacie wśród nas?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
Teraz więc jesteście przeklęci i nie przestaniecie być niewolnikami rąbiącymi drewno i noszącymi wodę dla domu mego Boga.
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
Oni odpowiedzieli Jozuemu: Oznajmiono dokładnie twoim sługom, że PAN, twój Bóg, rozkazał swemu słudze Mojżeszowi dać wam całą ziemię i zgładzić przed wami wszystkich mieszkańców tej ziemi. Dlatego bardzo się baliśmy o nasze życie z waszego powodu i dlatego tak postąpiliśmy.
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
A teraz oto jesteśmy w twoich rękach. Uczyń z nami to, co uważasz za dobre i słuszne.
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
I postąpił tak z nimi, i wybawił ich z rąk synów Izraela, żeby ich nie zabili.
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
I w tym dniu Jozue nakazał im narąbać drewna i nosić wodę dla zgromadzenia oraz dla ołtarza PANA w miejscu, które miał wybrać. I jest tak aż do dziś.