< Yoshua 9 >

1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
Ces événements appris, tous les rois d’au-delà du Jourdain, qui demeuraient dans les montagnes, dans les plaines, dans les lieux maritimes et sur le rivage de la grande mer; ceux aussi qui habitaient près du Liban, l’Héthéen, et l’Amorrhéen, le Chananéen, le Phérézéen, l’Hévéen et le Jébuséen,
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
Se réunirent tous ensemble pour combattre contre Josué et Israël, d’un même cœur et d’un même esprit.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
Mais ceux qui habitaient à Gabaon, apprenant tout ce qu’avait fait Josué à Jéricho et à Haï,
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
Et imaginant une ruse, prirent avec eux des vivres, mettant de vieux sacs sur leurs ânes et des outres de vin rompues et recousues,
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
Et des chaussures très vieilles, et qui, pour preuve de leur vétusté, étaient couvertes de pièces; ils étaient eux-mêmes vêtus de vieux habits: les pains aussi qu’ils portaient pour provisions de voyage, étaient durs et brisés en morceaux.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
C’est ainsi qu’ils vinrent vers Josué, qui alors se trouvait au camp de Galgala, et qu’ils lui dirent et en même temps à tout Israël: Nous sommes venus d’une terre lointaine, désirant faire la paix avec vous. Et les hommes d’Israël leur répondirent et dirent:
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
Peut-être que vous habitez dans la terre qui nous est due par le sort, et que nous ne pouvons faire alliance avec vous.
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
Mais eux à Josué: Nous sommes vos serviteurs, dirent-ils. Et Josué leur demanda: Qui êtes-vous? Et d’où venez-vous?
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
Ils répondirent: C’est d’une terre très lointaine que sont venus vos serviteurs, au nom du Seigneur ton Dieu; car nous avons appris la renommée de sa puissance, tout ce qu’il a fait en Egypte,
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
Et aux deux rois des Amorrhéens, qui étaient au-delà du Jourdain, Séhon, roi d’Hésébon, et Og, roi de Basan, qui était à Astaroth.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
Et les anciens et tous les habitants de notre terre nous ont dit: Prenez en vos mains des provisions pour ce très long voyage, et allez au-devant d’eux, et dites: Nous sommes vos serviteurs, faites alliance avec nous.
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
Voyez ces pains, quand nous sommes sortis de nos maisons, pour venir vers vous, nous les avons pris chauds; maintenant ils sont devenus secs et réduits en poudre par une excessive vétusté.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
Et ces outres de vin, nous les avons remplies neuves, maintenant elles sont rompues et décousues; et les vêtements que nous portons, et les chaussures que nous avons aux pieds, sont usés à cause de la longueur d’un trop long chemin, et presque entièrement détruits.
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
Ils prirent donc de leurs vivres et ils n’interrogèrent point l’oracle du Seigneur.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
Et Josué fit la paix avec eux, et, l’alliance contractée, il promit qu’ils ne seraient pas tués: les princes de la multitude aussi le leur jurèrent.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
Mais après trois jours de l’alliance faite, ils apprirent qu’ils habitaient dans le voisinage, et qu’ils allaient se trouver au milieu d’eux.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
Et les enfants d’Israël levèrent le camp, et ils arrivèrent le troisième jour dans leurs villes, dont les noms sont, Gabaon, Caphira, Béroth et Cariathiarim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
Cependant ils ne les tuèrent point, parce que les princes de la multitude le leur avait juré au nom du Seigneur Dieu d’Israël. C’est pourquoi tout le peuple murmura contre les princes,
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
Qui leur répondirent: Nous leur avons juré au nom du Seigneur Dieu d’Israël, et c’est pour cela que nous ne pouvons les toucher.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
Seulement, voici ce que nous leur ferons: Qu’à la vérité ils soient conservés à la vie, de peur que la colère du Seigneur ne s’élève contre nous, si nous nous parjurons;
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
Mais qu’ils vivent de telle sorte qu’ils coupent du bois et qu’ils portent de l’eau pour l’usage de toute la multitude. Pendant que les princes disaient ces choses,
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Josué appela les Gabaonites, et leur dit: Pourquoi avez-vous voulu nous surprendre par fraude, jusqu’à dire: Nous habitons fort loin de vous, tandis que vous êtes au milieu de nous?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
C’est pourquoi vous serez sous la malédiction, et jamais il ne manquera quelqu’un de votre race pour couper du bois et porter de l’eau dans la maison de mon Dieu.
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
Ceux-ci répondirent: Il a été annoncé à vos serviteurs, que le Seigneur votre Dieu avait promis à Moïse, son serviteur, qu’il vous livrerait toute cette terre, et qu’il en détruirait tous les habitants. Nous avons donc beaucoup craint, et nous avons pourvu à notre vie, poussés par la terreur de votre nom, et nous avons formé ce dessein.
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
Mais maintenant nous sommes en ta main, fais-nous ce qui te paraît bon et juste.
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
Josué fit donc comme il avait dit; et il les délivra de la main des enfants d’Israël, afin qu’ils ne fussent pas tués.
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
Et en ce jour-là il déclara qu’ils étaient au service de tout le peuple et de l’autel du Seigneur, pour couper du bois et porter de l’eau dans le lieu que le Seigneur aurait choisi; ce qu’ils ont fait jusqu’au présent temps.

< Yoshua 9 >