< Yoshua 9 >
1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
Lorsque ces nouvelles parvinrent aux rois des Amorrhéens de la rive droite du fleuve, à ceux de la montagne, à ceux du plat pays, à ceux de la côte de la grande mer, à ceux qui avoisinent l'Anti-Liban et aux Hettéens, aux Chananéens, aux Phérézéens, aux Evéens, aux Amorrhéens, aux Gergéeens et aux Jébuséens,
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
Ils se réunirent à la fois pour combattre Josué et Israël.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
En ce temps-là, les habitants de Gabaon ouïrent ce que le Seigneur avait fait de Jéricho et d'Haï.
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
Eux aussi usèrent d'artifice; ils se pourvurent de vivres, se tinrent prêts et partirent, ayant lié sur leurs épaules de vieux sacs, de vieilles outres de vin déchirées.
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
Le tour de leurs chaussures ainsi que leurs sandales étaient usés et rapiécés; leurs vêtements montraient la corde, et le pain de leur approvisionnement était desséché, moisi, rongé.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
Ils vinrent ainsi auprès de Josué, au camp d'Israël en Galgala, et ils dirent à Josué et à Israël: Nous arrivons d'une contrée lointaine, et maintenant faites avec nous une alliance.
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
Aussitôt, les fils d'Israël dirent à l'Horréen: Prenez garde; n'habitez- vous pas notre territoire? En ce cas, comment pourrions-nous faire alliance avec vous?
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
Mais ils répondirent à Josué: Nous sommes tes esclaves. Et Josué leur dit: D'ou êtes-vous? et d'ou venez-vous?
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
Ils reprirent: Tes esclaves arrivent d'une contrée très-lointaine, au nom du Seigneur ton Dieu; car nous avons ouï son nom, nous avons appris tout ce qu'il a fait en Egypte,
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
Et comment il a traité les rois des Amorrhéens qui étaient au delà du fleuve: Séhon, roi des Amorrhéens, et Og, roi de Basan, qui demeurait en Astaroth et en Edraïn.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
A ces nouvelles, nos anciens et tous ceux qui habitent notre contrée nous ont dit: Prenez avec vous des vivres pour la route, allez à leur rencontre, et dites-leur: Nous sommes vos esclaves, et maintenant faites avec nous une alliance.
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
Voici nos pains qui étaient chauds quand nous nous en sommes approvisionnés, le jour où nous sommes partis pour venir près de vous; ils sont maintenant desséchés et rongés.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
Et ces outres de vin que nous avons remplies neuves, vous les voyez déchirées; cependant, nos vêtements et nos chaussures se sont usés durant notre bien long voyage.
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
Alors, les chefs d'Israël prirent de ces provisions, et ils n'interrogèrent point le Seigneur.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
Josué leur accorda donc la paix; il fit avec eux une alliance qui les préserva de tout dommage, et les chefs de la synagogue leur prêtèrent serment.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
Trois jours après la conclusion de l'alliance, on leur apprit que c'étaient des voisins, et qu'ils habitaient leur territoire.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
Ensuite, les fils d'Israël levèrent leur camp, et eux allèrent à leurs villes; or, leurs villes étaient Gabaon, Caphira, Beroth et Cariathiarim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
Mais les fils d'Israël ne les combattirent point, parce que tous les chefs leur avaient prêté serment, au nom du Seigneur Dieu d'Israël. Et tout le peuple se prit à murmurer contre les chefs.
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
Et les chefs dirent à tout le peuple: Nous leur avons prêté serment au nom du Seigneur Dieu d'Israël, et maintenant nous ne pouvons les toucher.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
Voici ce que nous ferons: accordons-leur la vie et réservons-les, et il n'y aura point contre nous de colère, à cause du serment que nous leur avons prêté.
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
Ils vivront et ils seront les fendeurs de bois, les porteurs d'eau de toute la synagogue, comme les chefs le leur ont dit.
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Et Josué, les ayant appelés auprès de lui, leur dit: Pourquoi m'avez-vous trompé, disant: Nous sommes très-éloignés de toi; tandis que vous êtes de ceux qui habitent le territoire qui nous appartient?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
Maintenant, vous voici nappés de malédiction; jamais vous ne cesserez d'être esclaves, fendeurs de bois, porteurs d'eau à mon service et au service de mon Dieu.
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
Et ils répondirent à Josué, disant: On nous a rapporté que le Seigneur ton Dieu a prescrit à Moïse, son serviteur, de prendre possession de cette terre et d'exterminer devant vous, nous et tous ceux qui l'habitent; à votre approche, nous avons donc été remplis de crainte pour notre vie, et nous avons fait cette chose.
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
Maintenant, voilà que nous sommes en vos mains; faites de nous ce qui vous sera agréable, ce que vous jugerez à propos.
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
Or, voilà ce qu'on fit à leur égard: ce jour-là même, Josué les retira des mains des fils d'Israël, et ceux-ci ne les tuèrent point;
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
Et ce jour-là même, Josué en fit des fendeurs de bois, des porteurs d'eau pour tout le peuple, et pour l'autel du Seigneur. A cause de cela, les Gabaonites devinrent fendeurs de bois et porteurs d'eau pour l'autel du Seigneur; ils le sont encore de nos jours, et ils doivent servir au lieu qu'aura choisi le Seigneur.