< Yoshua 9 >
1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
Lorsque tous les rois qui étaient de l'autre côté du Jourdain, dans la montagne et dans la plaine, et sur tout le rivage de la grande mer devant le Liban, le Héthien, l'Amoréen, le Cananéen, le Phérézien, le Hévien et le Jébusien, en eurent connaissance
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
ils se rassemblèrent pour combattre Josué et Israël, d'un commun accord.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
Mais lorsque les habitants de Gabaon apprirent ce que Josué avait fait à Jéricho et à Aï,
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
ils eurent aussi recours à une ruse, ils allèrent se faire passer pour des ambassadeurs, ils prirent de vieux sacs sur leurs ânes, de vieilles peaux de vin déchirées et ficelées,
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
ils portèrent à leurs pieds de vieilles sandales rapiécées et de vieux vêtements. Tout le pain de leur réserve de nourriture était sec et moisi.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
Ils allèrent trouver Josué au camp de Gilgal et lui dirent, ainsi qu'aux hommes d'Israël: « Nous venons d'un pays lointain. Fais donc maintenant une alliance avec nous. »
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
Les hommes d'Israël dirent aux Hivvites: « Et si vous viviez parmi nous? Comment pourrions-nous faire une alliance avec vous? »
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
Ils dirent à Josué: « Nous sommes tes serviteurs. » Josué leur dit: « Qui êtes-vous? D'où venez-vous? »
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
Ils lui dirent: « Tes serviteurs sont venus d'un pays très lointain à cause du nom de Yahvé ton Dieu, car nous avons entendu parler de sa renommée, de tout ce qu'il a fait en Égypte,
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
et de tout ce qu'il a fait aux deux rois des Amoréens qui étaient au-delà du Jourdain, à Sihon, roi de Heshbon, et à Og, roi de Basan, qui était à Ashtaroth.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
Nos anciens et tous les habitants de notre pays nous ont parlé en disant: « Prenez en main des provisions pour le voyage et allez à leur rencontre. Dites-leur: « Nous sommes vos serviteurs. Fais maintenant une alliance avec nous ».
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
Voici notre pain que nous avons pris chaud pour nos provisions dans nos maisons le jour où nous sommes sortis pour aller vers vous; mais maintenant, voici, il est sec et il a moisi.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
Ces outres à vin, que nous avons remplies, étaient neuves; et voici qu'elles sont déchirées. Ces vêtements et nos sandales sont devenus vieux à cause du très long voyage. »
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
Les hommes goûtèrent à leurs provisions, et ne demandèrent pas conseil à la bouche de Yahvé.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
Josué fit la paix avec eux et conclut une alliance avec eux, pour les laisser vivre. Les princes de l'assemblée leur jurèrent.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
Au bout de trois jours, après qu'ils eurent fait alliance avec eux, ils apprirent qu'ils étaient leurs voisins et qu'ils vivaient parmi eux.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
Les enfants d'Israël partirent et arrivèrent dans leurs villes le troisième jour. Ces villes étaient Gabaon, Chephira, Beeroth et Kiriath Jearim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
Les enfants d'Israël ne les frappèrent pas, car les chefs de l'assemblée le leur avaient juré par l'Éternel, le Dieu d'Israël. Toute l'assemblée murmura contre les princes.
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
Mais tous les chefs dirent à toute l'assemblée: « Nous leur avons juré par l'Éternel, le Dieu d'Israël. Nous ne pouvons donc pas les toucher.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
Nous leur ferons cela, et nous les laisserons vivre, de peur que la colère ne s'abatte sur nous, à cause du serment que nous leur avons fait. »
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
Les princes leur dirent: « Laissez-les vivre. » Ils devinrent donc des coupeurs de bois et des puiseurs d'eau pour toute l'assemblée, comme les princes le leur avaient dit.
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Josué les fit venir et leur parla ainsi: « Pourquoi nous avez-vous trompés en disant: « Nous sommes très loin de vous », alors que vous habitez au milieu de nous?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
Maintenant, vous êtes donc maudits, et certains d'entre vous ne manqueront jamais de devenir des esclaves, aussi bien des coupeurs de bois que des puisatiers pour la maison de mon Dieu. »
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
Ils prirent la parole et dirent à Josué: « Parce que tes serviteurs ont certainement appris comment Yahvé ton Dieu a ordonné à Moïse, son serviteur, de te donner tout le pays et de détruire devant toi tous les habitants du pays. C'est pourquoi nous avons eu très peur pour nos vies à cause de vous, et nous avons fait cette chose.
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
Maintenant, voici, nous sommes entre tes mains. Fais de nous ce qu'il te semblera bon et juste de faire. »
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
Il leur fit ainsi et les délivra de la main des enfants d'Israël, afin qu'ils ne les tuent pas.
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
Ce jour-là, Josué les fit couper du bois et tirer de l'eau pour l'assemblée et pour l'autel de Yahvé jusqu'à ce jour, dans le lieu qu'il devait choisir.