< Yoshua 9 >
1 Basi ikawa wafalme wote waliokuwa magharibi mwa Yordani waliposikia juu ya haya yote, wale waliokuwa katika nchi ya vilima, upande wa magharibi mwa vilima na katika pwani yote ya hiyo Bahari Kuu, hadi kufikia Lebanoni (wafalme wa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi),
And when all the Kings that were beyonde Iorden, in the mountaines and in the valleis, and by all the coastes of the great Sea ouer against Lebanon (as the Hittites, and the Amorites, the Canaanites, the Perizzites, the Hiuites, and the Iebusites) heard thereof,
2 wakajiunga pamoja ili kupigana vita dhidi ya Yoshua na Israeli.
They gathered themselues together, to fight against Ioshua, and against Israel with one accord.
3 Hata hivyo, watu wa Gibeoni waliposikia juu ya hayo yote Yoshua aliyowatendea watu wa Yeriko na Ai,
But the inhabitants of Gibeon heard what Ioshua had done vnto Iericho, and to Ai.
4 nao wakaamua kufanya hila: Wakajifanya kama wajumbe wakiwa na punda waliobebeshwa mizigo wakiwa na magunia yaliyochakaa na viriba vya mvinyo vikuukuu vyenye nyufa zilizozibwa.
And therefore they wrought craftily: for they went, and fayned themselues ambassadours, and tooke olde sackes vpon their asses, and olde bottels for wine, both rent and bound vp,
5 Walivaa miguuni mwao viatu vilivyoraruka na kushonwa kisha wakavaa nguo kuukuu. Chakula chao kilikuwa mkate uliokauka na kuingia koga.
And olde shoes and clouted vpon their feete: also the raiment vpon them was old, and all their prouision of bread was dried, and mouled.
6 Ndipo wakamwendea Yoshua kambini huko Gilgali wakamwambia yeye pamoja na watu wa Israeli, “Tumetoka katika nchi ya mbali, fanyeni mkataba nasi.”
So they came vnto Ioshua into the hoste to Gilgal, and said vnto him, and vnto the men of Israel, Wee be come from a farre countrey: nowe therefore make a league with vs.
7 Basi watu wa Israeli wakawaambia hao Wahivi, “Lakini huenda mnakaa karibu nasi, twawezaje basi kufanya mapatano nanyi?”
Then the men of Israel said vnto the Hiuites, It may be that thou dwellest among vs, how then can I make a league with thee?
8 Wakamwambia Yoshua, “Sisi ni watumishi wako.” Yoshua akawauliza, “Ninyi ni nani, nanyi mnatoka wapi?”
And they said vnto Ioshua, We are thy seruants. Then Ioshua saide vnto them, Who are ye? and whence come ye?
9 Nao wakamjibu: “Watumishi wako wametoka nchi ya mbali sana kwa ajili ya umaarufu wa Bwana Mungu wenu. Kwa kuwa tumesikia taarifa zake: hayo yote aliyofanya huko Misri,
And they answered him, From a very farre countrey thy seruants are come for the Name of the Lord thy God: for we haue heard his fame and all that he hath done in Egypt,
10 pia yale yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani; huyo Sihoni mfalme wa Heshboni na Ogu mfalme wa Bashani, aliyetawala huko Ashtarothi.
And all that he hath done to the two Kings of the Amorites that were beyonde Iorden, to Sihon King of Heshbon, and to Og King of Bashan, which were at Ashtaroth.
11 Basi wazee wetu na wale wote wanaoishi katika nchi yetu walituambia, ‘Chukueni chakula cha safari; nendeni mkakutane na watu hao na kuwaambia, “Sisi tu watumishi wenu, fanyeni mapatano nasi.”’
Wherefore our elders, and all the inhabitants of our countrey spake to vs, saying, Take vitailes with you for the iourney, and go to meete them, and say vnto them, Wee are your seruants: now therefore make ye a league with vs.
12 Mkate huu wetu ulikuwa wa moto tulipoufunga siku tulipoanza safari kuja kwenu, lakini sasa angalia jinsi ulivyokauka na kuota ukungu.
This our bread we tooke it hote with vs for vittailes out of our houses, the day we departed to come vnto you: but nowe beholde, it is dried, and it is mouled.
13 Viriba hivi vya mvinyo vilikuwa vipya tulipovijaza, lakini ona jinsi vilivyo na nyufa. Nguo zetu na viatu vimechakaa kwa ajili ya safari ndefu.”
Also these bottels of wine which we filled, were newe, and lo, they be rent, and these our garments and our shooes are olde, by reason of the exceeding great iourney.
14 Basi watu wa Israeli wakavikagua vyakula vyao bila kupata shauri kutoka kwa Bwana.
And the men accepted their tale concerning their vittailes, and counselled not with the mouth of the Lord.
15 Ndipo Yoshua akafanya mapatano ya amani pamoja nao kuwaacha waishi, nao viongozi wa kusanyiko wakathibitisha kwa kiapo.
So Ioshua made peace with them, and made a league with them, that he would suffer them to liue: also the Princes of the Congregation sware vnto them.
16 Siku ya tatu baada ya hao kufanya mapatano na Wagibeoni, Waisraeli wakapata habari kuwa hao watu ni jirani zao waliokuwa wanaishi karibu nao.
But at the end of three dayes, after they had made a league with them, they heard that they were their neighbours, and that they dwelt among them.
17 Ndipo wana wa Israeli wakasafiri na siku ya tatu wakafika kwenye miji yao ya Gibeoni, Kefira, Beerothi na Kiriath-Yearimu.
And the children of Israel tooke their iourney, and came vnto their cities the third day, and their cities were Gibeon, and Chephirah, and Beeroth and Kiriath-iearim.
18 Lakini Waisraeli hawakuwashambulia kwa kuwa viongozi wa kusanyiko walikuwa wamewaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Kusanyiko lote likanungʼunika dhidi ya hao viongozi,
And the children of Israel slewe them not, because the Princes of the Congregation had sworne vnto them by the Lord God of Israel: wherefore all the Congregation murmured against the Princes.
19 lakini viongozi wote wakawajibu, “Tumeshawaapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, kwa hiyo hatuwezi kuwagusa sasa.
Then all the Princes said vnto all the Congregation, We haue sworne vnto them by the Lord God of Israel: nowe therefore we may not touch them.
20 Hivi ndivyo tutakavyowafanyia: Tutawaacha waishi, ili ghadhabu isije juu yetu kwa kuvunja kiapo tulichowaapia.”
But this we wil doe to them, and let them liue, least the wrath be vpon vs because of the othe which we sware vnto them.
21 Wakaendelea kusema, “Waacheni waishi, lakini wawe wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii yote.” Hivyo ahadi waliyoweka viongozi kwao ikawa hivyo.
And the Princes sayd vnto them againe, Let them liue, but they shall hewe wood, and drawe water vnto all the Congregation, as the Princes appoint them.
22 Kisha Yoshua akawaita Wagibeoni na kuwaambia, “Kwa nini mmetudanganya kwa kutuambia, ‘Tunaishi mbali nanyi,’ wakati ambapo ninyi mnaishi karibu nasi?
Ioshua then called them, and talked with them, and sayd, Wherefore haue ye beguiled vs, saying, We are very farre from you, when ye dwel among vs?
23 Sasa mko chini ya laana: Daima mtakuwa wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu.”
Now therefore ye are cursed, and there shall none of you be freed from being bondmen, and hewers of wood, and drawers of water for the house of my God.
24 Wakamjibu Yoshua, “Watumwa wako waliambiwa waziwazi jinsi Bwana Mungu wenu alivyomwamuru mtumishi wake Mose kuwapa ninyi nchi hii yote na kuwaangamiza wakazi wake wote toka mbele zenu. Kwa hiyo tuliogopa mno kwa ajili ya uhai wetu kwa sababu yenu, ndiyo maana tukafanya neno hili.
And they answered Ioshua, and sayd, Because it was tolde thy seruants, that the Lord thy God had commanded his seruant Moses to giue you all the land, and to destroy all the inhabitants of the land out of your sight, therefore we were exceeding sore afraid for our liues at the presence of you, and haue done this thing:
25 Sasa tupo mikononi mwako. Tufanyieni lolote mnaloona kuwa jema na haki kwako.”
And beholde nowe, we are in thine hand: doe as it seemeth good and right in thine eyes to doe vnto vs.
26 Kwa hiyo Yoshua akawaokoa mikononi mwa Waisraeli, nao hawakuuawa.
Euen so did he vnto them, and deliuered them out of the hand of the children of Israel, that they slewe them not.
27 Siku hiyo Yoshua akawafanya Wagibeoni wapasua kuni na wachota maji kwa ajili ya jamii na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana mahali pale ambapo Bwana angepachagua. Hivyo ndivyo walivyo hadi hivi leo.
And Ioshua appointed them that same day to be hewers of wood, and drawers of water for the Congregation, and for the altar of the Lord vnto this day, in the place which he should chuse.